vlcsnap-2020-09-20-11h48m00s617.png
Askofu Kiongozi wa Kanisa la Abundant Blessing Centre (ABC) lililopo Tabata Mandela , jijini Dar e Salaam, Flaston Ndabila, akiongoza maombi kwenye kongamano la maombi ya kuliombea Taifa kuelekea Uchaguzi Mkuu lililofanyika kanisani hapo jana.


IMG_3725.JPG
Maombi yakiendelea kwenye kongamano hilo.
IMG_3686.JPG
Kushono ni Bendera ya Tanzania iliombewa na maaskofu na Katikati ni Bendera Nyeupe ya Taifa la Israel ikiombewa na Kulia ni  Wachungaji wa Madhehebu wa Huduma ya Maombi wakiiombea Bendera ya Africa.
IMG_3661.JPG

 Mchungaji wa Huduma ya Maombi Tanzania, .Alice Kopwe akizungumza kwenye Kongamano hilo.

Maombi yakiendelea kwenye kongamano hilo.
Maombi yakiendelea kwenye kongamano hilo.
Maombi yakiendelea kwenye kongamano hilo.



Na Dotto Mwaibale.

KANISA la Abundant Blessing Centre (ABC) lililopo Tabata Mandela , jijini Dar e Salaam limefanya maombi ya kuliombea Taifa liwe na amani wakati huu wa kampeni hadi utakapofanyika uchaguzi Mkuu Oktoba 28, mwaka huu.

Kongamano la maombi hayo liliongozwa na Askofu Kiongozi wa Kanisa hilo, Flaston Ndabila akishirikiana na wachungaji, maaskofu na waumini kutoka jijini Dar es Salaam na mikoani.

Akifungua kongamano hilo, Ndabila alisema wameamua kufanya maombi hayo kwa sababu unapofanyika uchaguzi kunakuwa na changamoto mbalimbali.

Alisema kufuatia kuwepo kwa changamoto hizo, anahitajika mtu au watu wa kuzitatua kwa kuziombea na kuelimisha wagombea.

Ndabila alisema kanisa lina hekima ya kuvielekeza vyama vya siasa njia iliyonyooka ili viwe na busara ya kufanya uchaguzi bila ya umwagaji damu.

Aliongeza kuwa wao kama kanisa wanamuombea mama Janeth Magufuli Mungu ampe hekima ya kumshauri mumewe azidi kuliongoza taifa letu kwa busara kuepuka umwagikaji wa damu wakati huu wa uchaguzi.

Ndabila aliwapongeza wagombea wa vyama vya siasa kwa kuanza kuimba wimbo wa taifa kwenye kampeni zao huku wakimtanguliza Mungu.

Ndabila alisema vita ikitokea wa kulaumiwa litakuwa kanisa kwa sababu halikumuomba Mungu atuepushe na machafuko wakati wa uchaguzi.

"Wagombea wote ni watoto wa kanisa hivyo wanapaswa kumtii Mungu ili wasilete machafuko katika nchi yetu," alisema Ndabila.

Naye Mchungaji Evelyne Mayengo akizungumza kwenye kongamano hilo alimshukuru Mungu kwa kulilinda taifa letu tangu lilipoanzishwa kwa kulifanya taifa lenye umoja na mshikamano ingawa lina makabila mengi.

“Tumshukuru Mungu kwa viongozi wetu wakuu kubadilishana kijiti cha uongozi kwa amani bila kumwaga damu wala kuligawa taifa,” alisema mchungaji huyo.

Aidha, alimshukuru Mungu kuliponya taifa letu na maradhi ya Corona na kutuwezesha kufanya kampeni na uchaguzi mwaka huu.

Mchungaji Alistidia Modest wa Kanisa la MPC akizungumza kwenye kongamano hilo alimshukuru Mungu kwa kuliwezesha taifa letu kuingia kwenye uchumi wa kati kabla ya Mwaka 2025 uliokadiriwa.

Alimshukuru pia Mungu kwa kuifanya nchi yetu kuwa na rasilimali nyingi kama bahari, maziwa, madini yakiwemo ya Tanzanite yanayopatikana nchini mwetu pekee, gesi, milima, mbuga za wanyama na maendeleo ya kijamii, kiuchumi na kiroho.

Naye Mchungaji Alice Kopwe wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), amemuomba Mungu aiwezeshe NEC kusambaza vifaa vya kupigia kura vifike vituoni kwa wakati,  vitosheleze na kuwataka watanzania kujitokeza kwa wingi kupiga kura siku ya Oktoba 28.

Maombi yaliyojiri kwenye kongamano hilo pia yalihusu kuwaombea viongozi wa NEC, vyombo vya dola vitende haki na wote wawe na hofu ya Mungu ili uchaguzi uwe huru na haki. 

Kwa upande wake Bishop Sendrich Ndonde aliliombea baraka taifa la tanzania, taifa la Israel na kuwabariki waombaji waliohudhuria katika  kongamano hilo ambapo naye Mchungaji Dkt.  William Kopwe wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) amemuomba Mungu atupe Rais kutoka kwake.

Share To:

Post A Comment: