Halmashauri ya Manispaa ya Mpanda Mkoani Katavi imefanikiwa Kutoa Mikopo vikundi 43 vya Wajasiliamali kwa makundi ya Wanawake,Vijana na Walemavu kiasi cha shilingi milioni 148 huku mkuu wa Mkoa huo Juma Zuberi Homera akiliagiza Jeshi la Polisi kuwakamata na kuwaweka ndani walioshindwa kurejesha mikopo kiasi cha zaidi ya Milioni 40.

Homera ametoa maagizo hayo kwa Jeshi la Polisi Wilaya ya Mpanda kuhakikisha linawakamata na kuwaweka mahabusu walioshindwa kurejesha fedha walizokopeshwa na Halmashauri ya Manispaa ya Mpanda.
Share To:

Post A Comment: