NA HERI SHAABAN
UMOJA wa Wazalishaji Sabuni wadogo Tanzania (UWASWATA) wamechangia SERIKALI ya Mkoa Dar es Salaam, sabuni lita mia nne hamsini kwa ajili ya kujikinga na janga la COVID 19 corona .
Sabuni hizo zimepokelewa na Ofisa Katibu Tawala Msaidizi Utawala na Rasirimali Watu Lawrence Malangwa
Akizungumza wakati wa kukabidhi Sabuni hizo Katibu wa Umoja huo wa UWASWATA Maria Lucas alisema umoja wao wa UWASWATA umeguswa wamelazimika kuungana na juhudi za serikali katika kupambana na janga ili.
"Umoja huu uliundwa chini ya ofisi ya Mkemia Mkuu na SIDO ndio walezi wetu ambapo mpaka sasa jumla ya wanachama mia wa Umoja huu" alisema Maria .
Maria alisema misaada hiyo wanaendelea kuisaidia serikali ni endelevu hatua kwa hatua dhumuni kusaidia jamii na kutoa elimu kuhusiana na ugonjwa huo wa covid 19 corona.
Alimpongeza Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam kwa juhudi zake kubwa anazochukua katika kupambana na kutokomeza covid 19 katika Mkoa wa Dar es Salaam.
Kwaupande wake Katibu Tawala Msaidizi Utawala na Rasirimali Watu Lawrence Malangwa alisema sabuni zitapelekwa maeneo muhimu ili kusaidia jamii katika mapambano ya Corona.
Malangwa aliwataka wadau wa Mkoa wa Dar es Salaam kuendelea kujitokeza kusaidia Serikali katika mapambano hayo .
Naye Mkufunzi na sabuni na vipodozi SIDO Mkoa Dar es Salaam George Buchafwe aliwataka wafanyabiashara na Wajasiriamali kujiunga na SIDO katika kuunga mkono juhudi za Rais John Magufuli ili kujenga Tanzania ya Uchumi wa Viwanda .
George alisema nchi yetu inapokuwa na viwanda vingi uchumi pia unakuwa na upatikanaji wa masoko unaongezeka .
Mwisho
Post A Comment: