.
Hapi ametoa agizo hilo leo wakati akifungua kikao cha tathimini ya utekelezaji wa mkabata wa lishe kwa kipindi cha julai hadi Disemba 2019 ,mkuu wa mkoa wa Iringa Ally Hapi alisema kuwa iwapo mikakati ya kupunguza kasi ya udumavu ambayo mkoa umeweka ikatekelezwa kwa wakati na kwa uhakika upo uwezekano mkubwa wa asilimia za udumavu zikapungua zaidi.
Pia alitaka Halmashauri Halmashauri kutenga fedha katika mipango yake ya maendeleo angalau shilingi 1000 kwa kila mtoto chini ya miaka mitano na kuhakikisha fedha zinazotolewa kutekeleza afua za lishe .
Alisema kuwa tatizo la lishe katika jamii ya mkoa wa Iringa bado ni kubwa na kutokana na hali hiyo serikali imeendelea na jitihada mbali mbali za kutafuta tatizo la lishe mkoa ikiwa ni pamoja na kusimamia uwajibikaji wa afua za lishe .
" Ikumbukwe kuwa mwaka 2017 mkoa ulisaini mkataba wa utekelezaji wa masuala ya lishe na mwaka 2019 mikataba hii imeshushwa hadi ngazi ya kata na vijiji lengo likiwa ni kuhakikisha utekelezaji ,usiamizi na uwajibikaji wa afua mbali mbali za lishe unaratibiwa kuanzia ngazi za vijiji na mkitaa na juhudi za utekelezaji wa mikataba hiyo zilete matokeo katika kupunguza tatizo la utapiamlo hasa udumavu katika mkoa wa Iringa " alisema Hapi
Mkuu huyo alisema kuwa udumavu kwa mkoa ni asilimia 47 kiwango ambacho ni kikubwa kisichokubalika ndani ya mkoa wa Iringa ambao ni mmoja kati ya mikoa ambayo inaongoza kwa uzalishaji wa mazao ya chakula nchini .
" watoto wa miezi 6 hadi 23 milo inayotakiwa kulingana na umri wa wtoto ni asilimia 23 tu ,watoto wa miezi 6 hadi 23 wanaopewa mlo wenye mchanganyiko wa vyakula tofauti zikiwemo mboga mboga ,matunda na vyakula vyenye jamii ya kunde na nyama ni asilimia 25 tu "
Hivyo alisema lazima kuendelea mkushirikiana kupambana na hali mbaya ya udumavu mkoani Iringa kwani athari zinazosababishwa na lishe duni ni nyingi kama kuchelewesha ukuaji wa ubongo na kupungua uwezo wa kujifunza,kushindwa kuchangamkia fursa ,uwezo mdogo wa kupambanjua mambo na kufanya maamuzi .
Pia kupungua kwa uzalishaji kutokana na vifo ,maradhi na miili dhaifu ,kupungua kinga ya mwili hivyo kuruhusu mashambulizi ya magonjwa mbali mbali pamloja na vifo vya watoto chini ya miaka mitano na akina mama .
Alisema kuwa baadhi ya sababu za kuwepo kwa tatizo la utapiamlo katika mkoa ni pamoja na uelewa mdogo wa baadhi ya wazazi na walezi katika maandalizi na matumizi sahihi ya chakula kwa mfano kutokula na kutokuwalisha watoto chakula mchanganyiko ,kutumia nafaka zaidi kuandaa vyakula vya watoto na sababu nyingine nyingi .
Katika kuhakikisha mkoa unaendelea kutekeleza malengo iliyojiwekea ya kutokomeza udumavu kwa watoto alitaka tathimini ya utekelezaji wa mkakaba wa lishe ifanyike kila kipindi cha robo mwaka katika halmashauri zote,kila Halmashauri ihakikishe inawatambua wahudumu wa afya ya jamii (WAJA) waliopo katika katika Halmashauri na kuweka utaratibu wa kuwapa vitendea kazi na motisha ili wawe na mazingira mazuri ya utendaji kazi
Mkuu wa mkoa wa Iringa Ally Hapi akifungua kikao cha tathimini ya utekelezaji wa mkataba wa lishe ngazi ya mkoa ,kulia ni mkuu wa wilaya ya Kilolo Asia Abdallah na kushoto ni katibu tawala mkoa wa Iringa Happines Seneda
Mdau wa Lishe mkoa wa Iringa Lediana Mng'ong'o akichangia katika kikao hicho .
.....................
Mkuu wa mkoa wa Iringa Ally Hapi amewataka viongozi wa Halmashauri na wadau kushirikiana kupunguza kasi ya udumavu kwa watoto wenye umri wa miaka chini ya 5 kutoka asilimia 47 kwa sasa hadi kufikia angalau asilimia 35 ifikapo mwaka 2021.Hapi ametoa agizo hilo leo wakati akifungua kikao cha tathimini ya utekelezaji wa mkabata wa lishe kwa kipindi cha julai hadi Disemba 2019 ,mkuu wa mkoa wa Iringa Ally Hapi alisema kuwa iwapo mikakati ya kupunguza kasi ya udumavu ambayo mkoa umeweka ikatekelezwa kwa wakati na kwa uhakika upo uwezekano mkubwa wa asilimia za udumavu zikapungua zaidi.
Pia alitaka Halmashauri Halmashauri kutenga fedha katika mipango yake ya maendeleo angalau shilingi 1000 kwa kila mtoto chini ya miaka mitano na kuhakikisha fedha zinazotolewa kutekeleza afua za lishe .
Alisema kuwa tatizo la lishe katika jamii ya mkoa wa Iringa bado ni kubwa na kutokana na hali hiyo serikali imeendelea na jitihada mbali mbali za kutafuta tatizo la lishe mkoa ikiwa ni pamoja na kusimamia uwajibikaji wa afua za lishe .
" Ikumbukwe kuwa mwaka 2017 mkoa ulisaini mkataba wa utekelezaji wa masuala ya lishe na mwaka 2019 mikataba hii imeshushwa hadi ngazi ya kata na vijiji lengo likiwa ni kuhakikisha utekelezaji ,usiamizi na uwajibikaji wa afua mbali mbali za lishe unaratibiwa kuanzia ngazi za vijiji na mkitaa na juhudi za utekelezaji wa mikataba hiyo zilete matokeo katika kupunguza tatizo la utapiamlo hasa udumavu katika mkoa wa Iringa " alisema Hapi
Mkuu huyo alisema kuwa udumavu kwa mkoa ni asilimia 47 kiwango ambacho ni kikubwa kisichokubalika ndani ya mkoa wa Iringa ambao ni mmoja kati ya mikoa ambayo inaongoza kwa uzalishaji wa mazao ya chakula nchini .
" watoto wa miezi 6 hadi 23 milo inayotakiwa kulingana na umri wa wtoto ni asilimia 23 tu ,watoto wa miezi 6 hadi 23 wanaopewa mlo wenye mchanganyiko wa vyakula tofauti zikiwemo mboga mboga ,matunda na vyakula vyenye jamii ya kunde na nyama ni asilimia 25 tu "
Hivyo alisema lazima kuendelea mkushirikiana kupambana na hali mbaya ya udumavu mkoani Iringa kwani athari zinazosababishwa na lishe duni ni nyingi kama kuchelewesha ukuaji wa ubongo na kupungua uwezo wa kujifunza,kushindwa kuchangamkia fursa ,uwezo mdogo wa kupambanjua mambo na kufanya maamuzi .
Pia kupungua kwa uzalishaji kutokana na vifo ,maradhi na miili dhaifu ,kupungua kinga ya mwili hivyo kuruhusu mashambulizi ya magonjwa mbali mbali pamloja na vifo vya watoto chini ya miaka mitano na akina mama .
Alisema kuwa baadhi ya sababu za kuwepo kwa tatizo la utapiamlo katika mkoa ni pamoja na uelewa mdogo wa baadhi ya wazazi na walezi katika maandalizi na matumizi sahihi ya chakula kwa mfano kutokula na kutokuwalisha watoto chakula mchanganyiko ,kutumia nafaka zaidi kuandaa vyakula vya watoto na sababu nyingine nyingi .
Katika kuhakikisha mkoa unaendelea kutekeleza malengo iliyojiwekea ya kutokomeza udumavu kwa watoto alitaka tathimini ya utekelezaji wa mkakaba wa lishe ifanyike kila kipindi cha robo mwaka katika halmashauri zote,kila Halmashauri ihakikishe inawatambua wahudumu wa afya ya jamii (WAJA) waliopo katika katika Halmashauri na kuweka utaratibu wa kuwapa vitendea kazi na motisha ili wawe na mazingira mazuri ya utendaji kazi
Post A Comment: