Mkuu wa mkoa wa Iringa Ally Hapi akiteta na mwakilishi wa CCM mkoa wa Iringa katika kikao cha bodi ya barabara mara baada ya kikao kumalizika 
wabunge wa viti maalum mkoa wa Iringa Suzana Mgonakulima (Chadema ) na Zainabu Mwamwindi wakiwa kwenye kikao 
Mkuu wa wilaya ya Iringa Richard Kasesela kulia akiwa na mstahiki meya Iringa Alex Kimbe na mwenyekiti wa Halmashauri ya Iringa Stephen Mhapa wakati wa kikao cha bodi ya barabara 
Mkuu wa wilaya ya Mufindi Jamhuri Wiliam ,mkuu wa wilaya ya Kilolo Asia Abdallah na Mbunge wa Mufindi Kusini wakiwa katika kikao 


MKUU  wa  mkoa  wa Iringa  Ally  Hapi  amesema   serikali ya  awamu ya  tano chini ya  Rais Dkt  John Magufuli  imepania  kuuboresha   uwanja  wa ndege  wa  Nduli  mjini  Iringa  ili  kuwezesha  ndege   kubwa kama bombardier na airbus zianze  kutua katika uwanja  huo mwandishi Francis Godwin anaripoti kutoka Iringa 

Akizungumza jana wakati  wa  ufunguzi wa  kikao  cha bodi ya  barabara  mkoa  kilichofanyika katika  ukumbi wa Siasa ni  Kilimo mjini  Iringa  mkuu  huyo wa mkoa  alisema   serikali  imeendelea na uboreshaji wa uwanja  huo na ipo  mbioni  kuuboresha  zaidi   ili  kuwezesha  ndege nyenye ukubwa   wowote  na hata  ndege  za mizigo  kuutumia  uwanja  huo  kutua na kuruka  na mazao ya  wakulima wa mkoa wa Iringa kama Parachichi na mengine .

Alisema  kuwa  serikali ya waamu ya  tano  ndani ya  mkoa wa Iringa  imeanza  utekelezaji wa miradi  mikubwa ya miundo  mbinu  ikiwemo  barabara ya Mafinga kwenda  Kibao Mufindi  kwa  kiwango  cha lami ,barabara ya Iringa  - Hifadhi ya  Ruaha   na  kuboresha  uwanja wa ndege wa Nduli .

" Rais  wetu  mpendwa  Dkt  John Magufuli  ameamua  kutufanyia mambo makubwa  zaidi  mkoa wa Iringa  pamoja na ujenzi wa  barabara  zinazoelekea  katika maeneo ya  uwekezaji wa viwanda na  hifadhi  yetu ya Taifa ya  Ruaha   ameamua  kutenga  fedha  kwa  ajili ya upanuzi wa uwanja  wa  Nduli  ili  kuweza  kuwa na ubora  wa kimataifa   utakaowezesha  ndege  kubwa  zote  kutua  katika uwanja   huo "  alisema Hapi 

Alisema   kuwa  tayari taratibu  za  manunuzi katika   upanuzi wa  ujenzi wa uwanja  huo  zimeanza  na  kuwa  tayari  mfumo  wa viwanja vya ndege  wa  kuweza  kuongoza  ndege  kubwa kama  aibus  kutumia uwanja   huo  kutua na kuruka  bila  tatizo  lolote .

Akizungumzia  kuhusu  hali  halisi ya miundo mbinu ya barabara  mkoa wa Iringa  alisema mkoa  una mtandao wa barabara wenye  urefu  wa  jumla ya Kilometa 5,810.30  ambapo  wakala wa barabara nchini ( TANROADS ) unasimamia  kilometa 1,212.36  na  wakala wa barabara vijijini na mijini  (TARURA) unasimamia kilometa 4,597.94

 Alisema   upande wa barabara  zinazosimamiwa na TANROADS  kilometa 426.5 ni lami  sawa na asilimia 35.1 ya barabara  za  TANROADS  na kilometa 786.87 ni changarawe  sawa na asilimia  64.9 ya barabara  zote za TANROADS  wakati  kwa upande wa  TARURA  kilometa 97.30 ni lami  sawa na asilimia 2.11 ya  barabara zake  na kilometa 1,318.62 ni changarawe   sawa na asilimia 28.67 ya barabara zote  na  Kilometa 3,182.02  ni udongo  sawa na asilimia 69.2 ya barabara  za  TARURA .

Hapi  alisema  kuwa  katika  kuhakikisha  mkoa unakuwa na barabara  zinazopitika   muda  wote  serikali inayoongozwa na Rais Dkt Magufuli  imekuwa  ikitoa fedha  kwa ajili ya matengenezo mbali mbali ya barabara ili kuhakikisha  zinapitika   muda  wote  ikiwemo  wakati wa mvua  nyingi .

Alisema  kwa  mwaka wa fedha  2018/2019 serikali  ilitoa  jumla ya  shilingi 20,138,711,144.79  ambapo  kiasi cha  shilingi 14,346,000 zilitolewa   kwa  TANROADS  na na shilingi 5,779,365,144.79 zilitolewa kwa TARURA kwa  ajili ya matengenezo  na ujenzi  wa barabara  katika  mkoa wa  Iringa .

Katika  hatua  nyingine  mkuu  wa mkoa  ameuagiza  uongozi wa Halmashauri ya Manispaa ya  Iringa kutowatoza  wananchi gharama  ya greda  la Manispaa kwa  ajili ya kutengeneza  barabara za mitaa kwani kazi hiyo inapaswa  kufanywa na Manispaa  sio  wananchi .

MWISHO 
Share To:

Francis Godwin Mzee wa matukiodaima

Post A Comment: