Waziri wa nchi ofisi ya Waziri Mkuu Uwekezaji Angela Kairuki akizungumza  na waandishi wa habari wakati wa kutembelea kiwanda cha kuzalisha magunia Mkoani Morogoro.

 
 Waziri wa nchi ofisi ya Waziri Mkuu Uwekezaji Angela Kairuki akipata maelezo kutoka kwa meneja uzalishaji Benjamini Masinde baada ya kutembelea kiwanda cha kuzalisha magunia Mkoani Morogoro

Mawaziri 12 kutoka wizara mbalimbali wamefanua ziara ya kusikiliza na kuzitafutia ufumbuzi kero zinazowakabili wawekezaji wa kada zote katika mikoa ya Morogoro, Pwani na Dar es Salaam.

Akizungumza na wanahabari baada ya kuwasili mkoani Morogoro Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu,Uwekezaji Angela Kairuki amesema lengo la ziara hiyo ni kuhakikisha migogoro hasa ya wananchi na wawekezaji pamoja na changamoto zinazowakabili wawekezaji zinafanyiwa kazi ,nyingine papo hapo na ambazo ni za kiujumla zitaenda kufanyiwa kazi na Mawaziri wote 12 na utatuzi utapatikana.

Baada ya mkutano huo na waandishi wa habari Mh Waziri aalitembelea baadhi ya viwanda zaidi ya 10 na kujionea hali halisi ya uzalishaji wa viwanda hivyo na kuzungumza na uongozi wake pamoja na kusikiliza changamoto zao.

Aidha amewaeleza watendaji wa umma kuwa wana deni kubwa la kuhakikisha wanawatumikia wananchi kikamilifu pamoja na kushughulikia changamoto za wafanyabiashara na wawekezaji ili kutekeleza majukumu yao bila vikwazo kwa maendeleo ya Taifa.
Share To:

msumbanews

Post A Comment: