Askofu wa kanisa la kiinjili la kilutheri Tanzania (KKKT) dayosisi ya Iringa Mchungaji Blaston Gavile akitoa salamu za mkuu wa kanisa hilo
Waimbaji wa Kwaya kuu KKKT usharika wa kanisa kuu Iringa wakiwa katika ibada ya Krismasi
Wanakwaya wa Kwaya kuu
Wanaimbaji kwaya ya watoto na vijana
Mwalimu Jimson Sanga akiongoza kwaya Kuu
Askofu Blaston Gavile akisalimiana na muumini wake
Mwalimu Lupyana Samweli akiongoza kwaya ya vijana
Balozi wa Tanzania nchini Kenya Dkt Pindi Chana akinunua kitabu
Askofu Gavile akisalimiana na waumini wa kanisa kuu
Maandamano ya waumini wa kanisa kuu wakiongozwa na kwaya kuu
Balozi Pindi akisalimiana na waumini Iringa
Balozi Dkt Pindi akisalimiana na muumini wa kanisa kuu
Msaidizi wa askofu KKKT dayosisi ya Iringa Askali Mgeyekwa
Waumini wakisalimiana
Kwaya ya tarumbeta
Askofu wa kanisa la kiinjili kilutheri Tanzania (KKKT) dayosisi ya Iringa Blaston Gavile akimpongeza mkurugenzi mpya wa muziki dayosisi ya Iringa Jimson Sanga
Askofu Gavile akisoma ujumbe wa mkuu wa kanisa hilo
Mahubiri yakiendelea
Askofu Gavile akisisitiza jambo wakati wa mahubiri
Waumini wakifuatilia mahubiri ya Krismasi
Askofu Gavile kulia akizungumza na mmoja wa waumini wake pamoja na wasaidizi wake
Kanisa la kiinjili la kilutheri Tanzania (KKKT) limesema kutokana na sintofahamu iliyojitokeza katika uchaguzi wa serikali za mitaa uliofanyika bila kuwepo muafaka wa pamoja kwa wadau mbali mbali muhimu vikiwemo vyama vya siasa na taasisi nyingine kwa sasa kila mmmoja anahitaji habari njema ya furaha kuu
Huku balozi wa Tanzania katika jamhuri ya watu wa Kenya Dkt Pindi Chana akiwataka watanzania kuendelea kulinda amani na uzalendo kwa Taifa kwani kazi inayofanywa na Rais Dkt John Magufuli ya kuliletea Taifa maendeleo ni kubwa kila mmoja azidi kumuombea Rais ili taifa liendelee kuwa ni taifa la mfano kwa nchi za Afrika kwa amani na kasi ya maendeleo .
Akiwasilisha jana mbele ya waumini wa usharika wa kanisa kuu salamu za mkuu wa kanisa hilo Dkt Frederick Shoo ka usharika wa kanisa kuu ,askofu wa KKKT Dayosisi ya Iringa Blaston Gavile alisema kuwa salamu hizo anazisoma kama zilivyotumwa na mkuu huyo wa kanisa kwa nchi nzima .
“Malaika akawaambia ,msiogope kwa kuwa mimi ninawaletea habari njema ya furaha kuu itakayokuwa kwa watu wote ( Luka 2;10) kwanza kabisa naomba tuungane wote kwa unyenyekevu na kuimba sifa na shukrani nyingi kwa Mungu wetu aliyetulinda tangu tulipouanza mwaka huu wa 2019 na sasa tunaelekea mwisho wake hakika tumeona mkono wa Mungu ukitenda kazi katika maisha yetu ni kwa neema ya Mungu kwamba tumevushwa katika mengi magumu hadi kufikia kipindi cha majira haya wakati huu wa mwaka “ alisoma askofu Gavile .
Kuwa katika mwaka huu ambao unakwenda kumalizika sasa ni wazi kwamba haukuwa mteremko na raha tu ,bali kumekuwa na changamoto nyingi za kimaisha na wapo waliouguliwa sana na wengine hata kuondokewa na wapendwa wao na baadhi yao kupata wakati mngumu hata jinsi ya kulipa gharama za elimu ya watoto pamoja na kuwapatia mahitaji mengine muhimu imekuwa ngumu kutokana na changamoto za kiuchumi .
Alisema mwaka huu pia tumepata kushuhudia uchaguzi wa serikali za mitaa na vijiji ukifanyika kama kawaida ilivyo kwa nchi nyingi za Afrika uchaguzi huo haukupita bila changamoto kwani wamepata kushuhudia sintofahamu kadhaa katika mchakato mzima jambo lililosababisha kuingia katika uchaguzi huo bila changamoto hizo kufikiwa muafaka .
“ Mwaka huu nimechagua neno kutoka injili ya Luka inayosema tunamsikia malaika akitangaza habari njema ya furaha kuu ,habari hii hakika ni ya furaha kuu
maana ni ya kweli na haina ubaguzi ni kwa watu wote “
Alisema habari ya kuzaliwa kwa Mwokozi wetu Yesu Kristo ni habari njema nay a furaha kuu kwa watu wote yaani matajiri na masikini yatima na wajane ,wasomi na wasio wasomi ,tangazo la malaika linatutaka wote kusahau changamoto na magumu yote tuliyokutana nayo mwaka huu na kumtazama yesu Kristo mwakozi wetu anayetuletea furaha kuu mioyoni mwetu na maishani mwetu kwa ujumla .
Kuwa furaha kuu ya kwanza ambayo inapaswa kupokelewa katika neon ni kwamba Mungu anatupenda na ndiyo maana amemtuma mwanae wa pekee aje kutukomboa toka dhambini kuwa hiyo ni furaha yakweli kwa watu wote na sasa hakuna atakayepotea tena kwani nuru imekuja ulimwenguni na kupitia hiyo Nuru yaani Yesu kristo ni wazi tumeahidiwa uzima wa milele baada ya kusafishwa dhambi zetu ilieleza barua hiyo ya Dkt Shoo.
Kwa upande wake balozi wa Tanzania nchini Kenya Dkt Pindi Chana alisema kuwa Tanzania imekuwa ni nchi ya kuigwa na mfano miongoni mwa nchi za Afrika kwani kwa Kenya wengi wanafurahia sana demokrasia ya Tanzania na uzalendo wa watanzania katika nchi yao .
Dkt Chana alisema watanzania waliopo Kenya wanampongeza sana Rais Dkt John Magufuli kwa kuisimamia nchi vizuri na hata kuifanya nchi kuwa na maendeleo makubwa jambo ambalo linawavutia wengi .
“ watu wengi wanajifunza mambo mengi sana kutoka Tanzania hasa juu ya amani na Imani kwa kila mmoja kuabudu kwa uhuru Zaidi ikumbukwe mwalimu baba wa Taifa aliweza kuliunganisha Taifa vizuri na kulifanya kuwa taifa lenye amani na upendo ila pia Rais Dkt Magufuli ameendelea kuenzi yote ya baba wa Taifa “
Dkt Chana alisema ujumbe wake kwa niaba ya watanzania wanaoishi nchini Kenya ni kuendelea kuhimiza watanzania kutunza mazingira kama ambavyo serikali ya Tanzania ilivyoweza kuthibiti matumizi ya mifuko ya plastiki kuwa kampeni hiyo itawezesha mazingira kuwa safi na bora .
Post A Comment: