Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma na Utawala Bora Dkt. Mary Mwanjelwa akiwahutubia watumishi na wanachuo wa Chuo cha Utumishi wa Umma Tawi la Tabora wakati wa ziara ya siku moja jana chuoni hapo.
Mkuu wa Mkoa wa Tabora Aggrey Mwanri akitoa maneno ya utangulizi wakati wa ziara ya Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Dkt. Mary Mwanjelwa, Balozi wa Sweden Nchini Anders Sjober walipotembelea Chuo cha Utumishi wa Umma.

Mkuu wa Mkoa wa Tabora Aggrey Mwanri(kushoto) akimkaribisha Balozi wa Sweden nchin Anders Sjober wakati wa ziara ya Balozi huyo Mkoani Tabora jana.
Mkuu wa Mkoa wa Tabora Aggrey Mwanri akimkaribisha Naibu Waziri Ofisi ya Rais , Ututumishi na Utawala bora Dkt. Mary Mwanjelwa (kulia) wakati alipoongozana na Balozi wa Sweden nchini alipotembelea Chuo cha Utumishi wa Umma Tawi la Tabora jana
Mkuu wa Mkoa wa Tabora Aggrey , Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Dkt. Mary Mwanjelwa, Balozi wa Sweden Nchini Anders Sjober na viongozi mbalimbali na wanachuo wa Uhazili wakicheza wimbo maalumu wakati wa ziara yao ya siku moja ya kukagua Chuo cha Utumishi wa Umma.


Mkuu wa Mkoa wa Tabora Aggrey , Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Dkt. Mary Mwanjelwa, Balozi wa Sweden Nchini Anders Sjober na viongozi mbalimbali wakiwa katika picha ya pamoja jana mbele ya jengo la Mkoa wa Tabora wakati wa ziara yao ya siku moja ya kukagua Chuo cha Utumishi wa Umma.

*****************************



KIASI cha shilingi bilioni 3.417 zinahitajika kwa ajili ya ukarabati na uboreshaji wa miundo mbinu ya Chuo cha Utumishi wa Umma Tawi la Tabora(Uhazili)

Kauli hiyo imetolewa jana na Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Utumishi wa Umma na Utawala Bora Dkt Mary Mwanjelwa wakati wa ziara ya Balozi wa Sweden Nchi Anders Sjober alipotembelea Chuo hicho.

Alisema fedha hizo ni kwa ajili ya ukarabati wa majengo kama vile Mabweni , madarasa, jengo la utawala , uboreshaji wa miundo mingine , ukakamilishaji wa jengo jipya na ununuzi vifaa vya kujifunzia.

Dkt. Mwanjelwa alisema hatua hiyo itasaidia kukirejesha chuo hicho katika ubora wake wa awali na kukifanya kuendelea kuwa sehemu nzuri ya kuwaandaa watumishi kwa ajili ya kutoa huduma nzuri kwa wananchi.

Aidha Naibu Waziri huyo aliwataka watumishi wa umma kuhakikisha watoa huduma nzuri kwa wananchi ambayo itakwenda sanjari na maendeleo ya tekonolojia yaliyo hivi sasa.

Kwa upande wa Balozi wa Sweden Nchini Sjober alisema Tanzania na nchi yake zina uhusiano mzuri wa muda mrefu na ndio maana walishiriki kujenga chuo hicho kwa asilimia 80.

Aidha aliipongeza Serikali kwa jitihada zake kujenga jengo jipya ambalo limeshagharimu shilingi bilioni 2.7 ambazo zinatokana na fedha za ndani za mapato ya Tanzania.

Naye Mkuu wa Mkoa wa Tabora Aggrey Mwanri alisema Chuo cha Utumishi wa Umma Tawi la Tabora kinaomchango mkubwa katika utumishi ndani na nje ya Tanzania kwa kuzalisha viongozi mbalimbali. 

Aliwataja baadhi ya viongozi wakubwa ambao wamepita katika Chuo hicho ni pamoja na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan na Mke wa Rais wa kwanza wa Zimbabwe mama Mugabe.
Share To:

msumbanews

Post A Comment: