Waziri wa mifugo na uvuvi Luhaga Mpina ameongoza zoezi la kuchoma nyavu haramu za uvuvi  aina ya KOKOLO na NJENGA zinazokadiriwa kuwa na thamani ya zaidi ya  shilingi milioni miamoja na hamsini zilizokamatwa kwenye operesheni ya uvuvi haramu  katika  bwawa la Nyumba ya Mungu wilayani  Mwanga Mkoani Kilimanjaro.

Akizungumza na wananchi kabla ya kuongoza  zoezi la kuchoma vyavu hizo katika kijiji cha Kagongo wilayani mwanga waziri wa mifugo na uvuvi  Luhaga Mpina anasema serikali haitamvumilia mwananchi wala kiongozi atakayebainika kuhusika na uvuvi haramu na kuwaita  watu hao kuwa ni wahujumu wa uchumi.
Mkuu wa wilaya ya Mwanga Thomas Apson anasema suala la uvuvi haramu   mbali na wananchi kuendelea na uhalifu huo pia limegubikwa na sintofahamu hata kwa watendaji wa serikali na kuahidi kuwashughulika bila huruma.


Baadhi ya wananchi walioshudia tukio ilo nao wakapaza sauti zao mbele ya waziri huyo kuhusiana na changamoto wanazokumbana nazo katika mapambano dhidi ya uvuvi huo  haramu.

Baadhi ya picha mbalimbali





Share To:

msumbanews

Post A Comment: