Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya
Makamu wa Rais Balozi Joseph Sokoine
(katikati) akifungua kikao kazi cha Wakurugenzi wa Sera na Mipango wa Wizara za
Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (SMT). Kikao hicho kimejadili
uratibu wa masuala ya Muungano ikiwa ni pamoja na upatikanaji wa taarifa kutoka
katika kila Wizara na kimefanyika katika
Ukumbi wa Mikutano katika Jengo la Bima ya Afya Jijini Dodoma. Kulia ni Kaimu
Mkurugenzi Idara ya Muungano Bw. Sifuni Msangi na Bi. Lupi Mwaikambo Mkurugeni
Msaidizi Idara ya Muungano.
Bi. Mariam Silim Mkurugenzi
Msaidizi Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi na Bw. Ezekiel Chundu
Mchumi, Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Ujenzi) wakifuatilia maelezo
ya Naibu Katibu Mkuu (hayupo pichani) katika Kikao cha Wakurugenzi wa Sera na
Mipango, Tanzania Bara. Kikao hicho kimefanyika hii leo Jijini Dodoma.
Sehemu ya wajumbe
wakifuatilia kikao hicho kilichofanyika hii leo Jijini Dodoma.
Post A Comment: