Na Ferdinand Shayo,Iringa .
Wakulima wa nyanya  mkoani Iringa wamesambaziwa mbegu bora za nyanya aina ya Firenze F1 ambazo ni mkombozi wa mkulima zinatoa mazao mengi na kuhimili magonjwa ya nyanya ambayo yamekua yakiwasumbua wakulima wengi kupata hasara na kushindwa kunufaika na kilimo.
Mwakilishi wa kampuni ya Bayer Crop Science zamani ikijulikana kama Monsanto, William Macha, amesema kuwa nyanya hiyo inaweza kudumu kwa muda mrefu bila kuharibika baada ya kuvunwa na kusafirishwa katika masoko ya ndani na nje ili kuwafikia walaji ikiwa kwenye hali nzuri.
“Mbegu hizi  za Firenze FD1 Nyanya “Dum Dum” ukiwa na gramu 25 inatosha kwa ekari moja kwasababu inaota kwa asilimia 99%  ,kutoka mche mmoja kwenda mwingine tuweke 45 cm ili uweze kupata mazao ya kutosha na kuvuna kwa awamu  mara 8 mpaka 12”
Anasema kuwa mbegu hizo zinazaa mara tatu zaidi ya mbegu za kawaida  na pia inakomaa ndani ya siku 75 na inaweza kuongeza pato la mkulima na kuboresha maisha yake.
Mwenyekiti wa Shirikisho la Wakulima wa nyanya na mboga mboga Mtokambali Mrisho amesema kuwa kwa mara ya kwanza mbegu ya Firenze F1 kuingia, ilifanyiwa majaribio katika kijiji cha Tanangozi Iringa na kufanya vizuri sana baada ya hapo ilipendekezwa kuwa mbegu bora zaidi na wakulima walianza kuitumia na kupata matokea makubwa.
Mtokambali amesema kuwa kwa sasa wakulima kutoka mikoa ya Dodoma na Morogoro wanafika kujifunza kwenye shamba darasa la mbegu hizo ambazo  zimeleta mavuno pesa kwa wakulima wengi mko wa Iringa na viunga  .
Share To:

Post A Comment: