Na Heri Shaaban
MKUU wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda , ameipongeza Manispaa ya Ilala kwa kushika nafasi ya kwanza Kitaifa ,katika ukusanyaji wa Mapato ya Serikali.
Makonda alitoa pongezi hizo kwa Watendaji wa Ilala Dar es Salaam jana,wakati wa kikao cha Majumuisho ya ziara yake Mkoa wa Dar es Salaam wakati alipokuwa akiongea na Watendaji wa manispaa zote.
"Nimefarijika sana katika Mkoa wangu Manispaa ya Ilala imevuka lengo la ukusanyaji mapato robo ya mwaka wamefikia asilimia 78 naziomba halmashauri zingine muongeze juhudi mkoa wetu ufanye vizuri zaidi " alisema Makonda
Aliwataka Manispaa ya Ilala kuendelea katika ukusanyaji wa fedha za serikali speed hiyo isirudi nyuma
Alimwagia sifa *wakurugenzi* wa Halmashauri na watendaji kwa *kusimamia vizuri ukusanyaji wa Mapato* jambo lililopelekea *Dar es salaam kuibuka namba moja kitaifa* katika Makusanyo ya mapato katika *Robo ya Mwaka.
Alisema mpaka sasa wamefanikiwa kukusanya kiasi cha silingi *Bilioni 118.4* ukifuatiwa na Mkoa wa Dodoma uliokusanya Shilingi Bilioni 57.3, wilaya iliyoongoza Kitaifa Ilala ikifuatiwa na
Kinondoni pamoja na Temeke iliyoshika nafasi ya Tatu kitaifa.
Aidha Makonda amewahimiza Watendaji kuendelea kusimamia vyema makusanyo ya kodi pasipo kuwabugudhi wananchi ili kuwezesha Mkoa huo kuendelea kushika namba moja.
Wakati huo huo Makonda alimwagia sifa Wilaya ya Ilala kwa kufanya vizuri katika utoaji wa mikopo vikundi vya halmashauri ya Ilala hadi Wajane wamepata.
Katika hatua nyingine aliwagiza Wakuu wa Wilaya kuweka mkakati wa kuorodhesha viwanda vyote vipya ambayo vipo katika wilaya yao.
Mwisho
Arnatogluo Dar es Salaam April 30/2019
Post A Comment: