Rais Magufuli amesema kuwa hatoongeza mshahara mwaka huu, kwani ahadi yake ya kupandisha mishahara katika uongozi wake haijaisha kwa sababu bado hajamaliza muda wake madarakani.
 
Rais Magufuli ametoa kauli hiyo leo May 1, 2019 mara baada ya hapo awali TUCTA kumuomba atimize  ahadi yake ya kuwaongeza wafanyakazi mishahara.

"Niwaambie ndugu zangu, Katibu mkuu TUCTA alinikumbusha kuhusu ahadi yangu, ninaikumbuka na ninasema muda wangu bado nipo madarakani, ninachoomba muwe na subira.

“Ni kweli kwenye sherehe kama hizi mwaka jana niliahidi kuwa nitaongeza mishahara ya wafanyakazi kabla sijaondoka madarakani, ndugu zangu tuvumilie tu sikutaka kuwadanganya hapa kuwa nimewaongezea mishahara halafu fedha mtakazozipata hazipo, nyinyi endeleeni kuvumilia tupo katika muelekeo mzuri wa suala hili”, Amesema Rais Magufuli na kuongeza;

“Ningeweza kuwaongezea elfu 5 au 10, kesho tu bidhaa zingeanza kupanda hivyo lazima kwanza tujenge uchumi imara. Mimi mwenyewe nilikuwa mwalimu na nikaenda kuoa mwalimu anayejua shida zetu Serikali inawapenda wafanyakazi.
Share To:

msumbanews

Post A Comment: