Mwanzilishi wa Taasisi ya Tony Elumelu Foundation, Tony
Elumelu, akiwa katika moja ya mikutano
ya wajasiriamali wa Afrika nchini Nigeria.
*Kukutanisha
wajasiriamali 5,000 wa Bara la Afrika
Washiriki wa moja ya mikutano iliyopita wakiwa katika picha ya pamoja na mwasisi wa Tony Elumelu Foundation. |
Na
MWANDISHI WETU
-Abuja,
Nigeria
Taasisi
ya Tony Elumelu Foundation (TEF) ambayo inapambania wajasiriamali kutoka Afrika
itakuwa mwenyeji wa awamu ya 5 ya mkusanyiko mkubwa wa wajasiriamali kutoka
Afrika itakayofanyika Julai 26 na 27, 2019, ambapo mkutano huo wa siku mbili utafanyika
Hoteli ya Transcorp Hilton, Abuja nchini Nigeria.
Mkutano
huo wa kila mwaka huandaliwa kupitia Programu
ya Tony Elumelu Foundation Entrepreneurship ambayo imewapa mafunzo Waafrika
chipukizi 3,000 ambao walichaguliwa kutoka zaidi ya waombaji 216,000.
Tukio
hilo linawapa nafasi wanawake na wanaume chipukizi kutoka nchi zote 54 za
Afrika kukutana, kujifunza na kubadilishana mawazo yenye mlengo wa kuwa
wawekezaji bora Afrika na duniani.
Pia ni
fursa muhimu kwa viongozi wanasiasa na watunga sera kukutana uso kwa uso na
kizazi kipya cha wafanyabiashara viongozi Wafrika ambao wanabadilisha uchumi wa
Afrika.
Wazungumzaji
wakuu katika warsga hiyo muhimu ni Rais wa Rwanda, Paul Kagame, na Rais wa
Senegal, Macky Sall, ambao wataungana na Mwanzilishi wa TEF ambaye pia ni Mwenyekiti
wa Heirs Holdings na United Bank for Africa (UBA), Tony O. Elumelu, katika
majadiliano ya wazi.
Uwepo wa
marais hao unawapa fursa wajasiriamali kutoka Afrika wanaohudhuria kuwa na
mjadala wa kina na kutoa ushuhuda namna serikali inavyoweza kufanya kuchochea
ukuwaji wa biashara.
Ajenda ya
mkutano huo inahusisha majadiliano na wataalamu kutoka Afrika na duniani ambao
watawapa mafunzo washiriki kuongeza ujuzi katika biashara yao. Aidha warsha
hiyo itawapa fursa baadhi wajasiriamali wateuli kuelezea bidhaa na huduma
wanazotoa mbele ya jopo la majaji.
Kwa mara
ya kwanza, warsha hiyo itafanyika Abuja, Nigeria na kuwaleta pamoja watunga
sera wakubwa, wafanyabiashara wakubwa na wale waliowahi kufaidi Programu hiyo.
Mwaka
jana, tukio muhimu lilikuwa uzinduzi wa TEFConnect ambayo ni sehemu ya
wajasiriamali kutoka Afrika kubadilishana mawazo kupitia mfumo wa digitali.
Mikutano
hiyo imewahi kuhudhuriwa na marais
kadhaa wakiwamo Rais wa Ghana, Nana Akufo-Addo, Rais wa Kenya, Uhuru Kenyatta, Rais
wa Mstaafu wa Nigeria, Olusegun Obasanjo, Waziri Mkuu wa mstaafu wa Benin na
Mjumbe wa Bodi ya Ushauri, Lionel Zinsou na Makamu wa Rais wa Nigeria, Profesa
Yemi Osinbajo.
Taasisi
ya Tony Elumelu imedhamiria kuleta mabadiliko Afrika nzima kupitia ujasiriamali
kwa kutaka zaidi Waafrika kujitegemea, Africapitalism, chini ya mwanzilishi
huku akitambua zaidi kuwawezesha vijana wa Afrika kiuchumi hususan karne hii ya
21.
Mwaka 2015,
taasisi hiyo ilijitolea dola za Marekani milioni 100 million kuwawezesha
wajasiriamali 10,000 kutoka kote barani kwa zaidi ya miaka 10 ambapo kwa sasa
inakwenda kutimiza miaka mitano.
Pia Tony
Elumelu Foundation imetoa mchango wa kushauri na kutoka mafunzo ya menejementi kwa
zaidi ya watu 7,500 wanaoanzisha na wenye biashara ndogo kwa nchi zote 54 za
Afrika.
“Warsha
ya TEF Entrepreneurship haitaleta tu watu wadau muhimu katika mabadiliko ya
ujasiriamali wa Afrika lakini pia kumpa nafasi kila mtu kupanua biashara yake
kwa nia ya kuleta maendeleo barani.
“Tunafarijika
kupokea habari kutoka kwa wajasiriamali wetu ambao wanatengeneza ajira,
wanaajiri watu na kubadilisha maisha ya jamii inayowazunguka barani Afrika.
Tunaamini hawa wajasiriamali ni tegemeo wetu wa baadaye. Wekezeni kwao sasa na
kuvuna ndoto ya kesho ya Afrika,” alisema Mkurugenzi Mtendaji wa TEF.Ifeyinwa
Ugochukwu.
Mwisho
Post A Comment: