Mke wa Marehemu Jacline akiwa pamoja na watoto katika katisa la KKKT usharika wa moshi mjini
 Mtoto wa Marehemu Regina Mengi akiwa kanisani tayari kwa ibada katika Kanisa la KKKT usharika wa Moshi mjini Mkoani Kilimanjaro
 Waombolezaji wakiwa kanisani tayari kwa ibada

Kanisa la KKKT Dayosisi ya Kaskazini Usharika wa Moshi mjini mahali ambapo wenyeji wa Mkoa wa kilimanjaro,wageni mbalimbali wanapouaga Mwili wa Dkt.Regnald Mengi 

Watu mbalimbali wakiendelea kuuaga Mwili wa Dkt.Regnald Mengi KKKT Usharika wa Moshi Mjij
 Waombolezaji wakiwa kwenye foleni kwaajili ya kuagana na mpendwa wao Regnald Mengi
 Waombolezaji wakiwa kwenye foleni
 Waombolezaji wakiingia kanisani
 Lango kuu la Kanisa kama linavyoonekana
 Wakazi wa Mkoa wa Kilimanjaro wakiwa katika foleni kwaajili ya kuingia kanisani kuuagana na mpendwa wao Regnald Mengi leo.
Na Vero Ignatus,Moshi

MAELFU ya wakazi wa  mikoa ya Kilimanjaro,Arusha,Manyara na maeneo jirani wamejitokeza kuaga mwili wa aliyekuwa Mwenyekiti wa Kampuni tanzu za IPP Regnald Mengi,kwenye ibada ya mazishi katika kanisa la kiinjili la Kilutheri usharika wa Moshi Mjini.

Mwili wa marehemu Dkt Regnald Mengi,umewasili katika kanisa Hilo majira ya saa 2:00 asubuhi,ambapo ulipokelewa na na baadhi ya viongozi mbalimbali ambao ni wabunge Nape Mnauye,Godbles Lema,Freeman Mbowe,Luhaga Mpina,Anna Kilango na James Mbatia.

Hata hivyo Mara baada ya mwili huo kuwasili pia ulipokewa na vilio,simanzi na majonzi kwa wanachi ambao walionekana wamefurika katika maeno yote ya viunga vya kanisa hilo.

Kutokana na umati wa watu kuzidi skauti ambao walikuwa katika lango kuu la kuingilia watu  polisi walilazimika kuingilia katika ili kunisuru Hali iliyokuwepo ambayo ilihatarisha usalama.

Hata hivyo baada ya zoezi la kutoa heshima za mwisho,Mwili wa Mengi,safari ya kuelekea machame Kijiji Nkuu Sinde kuulaza mwili huo utaanza,ambapo Waziri Mkuu anatarajiwa kuongoza maelfu ya wanachi katika mazishi hayo.

Mwisho

Share To:

Vukatz Blog

Post A Comment: