Mke wa Marehemu Jacline akiwa pamoja na watoto katika katisa la KKKT usharika wa moshi mjini
Mtoto wa Marehemu Regina Mengi akiwa kanisani tayari kwa ibada katika Kanisa la KKKT usharika wa Moshi mjini Mkoani Kilimanjaro
Waombolezaji wakiwa kanisani tayari kwa ibada
Kanisa la KKKT Dayosisi ya Kaskazini Usharika wa Moshi mjini mahali ambapo wenyeji wa Mkoa wa kilimanjaro,wageni mbalimbali wanapouaga Mwili wa Dkt.Regnald Mengi
Waombolezaji wakiwa kwenye foleni
Waombolezaji wakiingia kanisani
Lango kuu la Kanisa kama linavyoonekana
Wakazi wa Mkoa wa Kilimanjaro wakiwa katika foleni kwaajili ya kuingia kanisani kuuagana na mpendwa wao Regnald Mengi leo.
Na Vero Ignatus,Moshi
MAELFU ya wakazi wa mikoa ya Kilimanjaro,Arusha,Manyara na maeneo jirani wamejitokeza kuaga mwili wa aliyekuwa Mwenyekiti wa Kampuni tanzu za IPP Regnald Mengi,kwenye ibada ya mazishi katika kanisa la kiinjili la Kilutheri usharika wa Moshi Mjini.
Mwili wa marehemu Dkt Regnald Mengi,umewasili katika kanisa Hilo majira ya saa 2:00 asubuhi,ambapo ulipokelewa na na baadhi ya viongozi mbalimbali ambao ni wabunge Nape Mnauye,Godbles Lema,Freeman Mbowe,Luhaga Mpina,Anna Kilango na James Mbatia.
Hata hivyo Mara baada ya mwili huo kuwasili pia ulipokewa na vilio,simanzi na majonzi kwa wanachi ambao walionekana wamefurika katika maeno yote ya viunga vya kanisa hilo.
Kutokana na umati wa watu kuzidi skauti ambao walikuwa katika lango kuu la kuingilia watu polisi walilazimika kuingilia katika ili kunisuru Hali iliyokuwepo ambayo ilihatarisha usalama.
Hata hivyo baada ya zoezi la kutoa heshima za mwisho,Mwili wa Mengi,safari ya kuelekea machame Kijiji Nkuu Sinde kuulaza mwili huo utaanza,ambapo Waziri Mkuu anatarajiwa kuongoza maelfu ya wanachi katika mazishi hayo.
Mwisho
Mtoto wa Marehemu Regina Mengi akiwa kanisani tayari kwa ibada katika Kanisa la KKKT usharika wa Moshi mjini Mkoani Kilimanjaro
Waombolezaji wakiwa kanisani tayari kwa ibada
Kanisa la KKKT Dayosisi ya Kaskazini Usharika wa Moshi mjini mahali ambapo wenyeji wa Mkoa wa kilimanjaro,wageni mbalimbali wanapouaga Mwili wa Dkt.Regnald Mengi
Watu mbalimbali wakiendelea kuuaga Mwili wa Dkt.Regnald Mengi KKKT Usharika wa Moshi Mjij
Waombolezaji wakiwa kwenye foleni kwaajili ya kuagana na mpendwa wao Regnald MengiWaombolezaji wakiwa kwenye foleni
Waombolezaji wakiingia kanisani
Lango kuu la Kanisa kama linavyoonekana
Wakazi wa Mkoa wa Kilimanjaro wakiwa katika foleni kwaajili ya kuingia kanisani kuuagana na mpendwa wao Regnald Mengi leo.
Na Vero Ignatus,Moshi
MAELFU ya wakazi wa mikoa ya Kilimanjaro,Arusha,Manyara na maeneo jirani wamejitokeza kuaga mwili wa aliyekuwa Mwenyekiti wa Kampuni tanzu za IPP Regnald Mengi,kwenye ibada ya mazishi katika kanisa la kiinjili la Kilutheri usharika wa Moshi Mjini.
Mwili wa marehemu Dkt Regnald Mengi,umewasili katika kanisa Hilo majira ya saa 2:00 asubuhi,ambapo ulipokelewa na na baadhi ya viongozi mbalimbali ambao ni wabunge Nape Mnauye,Godbles Lema,Freeman Mbowe,Luhaga Mpina,Anna Kilango na James Mbatia.
Hata hivyo Mara baada ya mwili huo kuwasili pia ulipokewa na vilio,simanzi na majonzi kwa wanachi ambao walionekana wamefurika katika maeno yote ya viunga vya kanisa hilo.
Kutokana na umati wa watu kuzidi skauti ambao walikuwa katika lango kuu la kuingilia watu polisi walilazimika kuingilia katika ili kunisuru Hali iliyokuwepo ambayo ilihatarisha usalama.
Hata hivyo baada ya zoezi la kutoa heshima za mwisho,Mwili wa Mengi,safari ya kuelekea machame Kijiji Nkuu Sinde kuulaza mwili huo utaanza,ambapo Waziri Mkuu anatarajiwa kuongoza maelfu ya wanachi katika mazishi hayo.
Mwisho
Post A Comment: