Wakala wa Mabasi Yaendayo Haraka (Dart), imesema kuna uhaba wa mabasi yanayotoa huduma na kusababisha usumbufu kwa watumiaji wa usafiri huo.

Taarifa iliyotolewa leo, Jumatano Aprili 10, 2019 kwa vyombo vya habari  na Meneja Uhusiano wa Umma wa Dart, William Gatambi imesema uhaba huo unatokana na mabasi hayo kupata hitilafu mbalimbali.

“Idadi ya mabasi yanayotoa huduma leo katika mfumo wa Dart ni 85, huku 58 yakifanyiwa matengenezo makubwa na madogo.

“Tunawaomba wateja wetu kuwa na subira wakati mabasi hayo yakifanyiwa matengenezo. Tunawaomba radhi kwa usumbufu unaojitokeza,”amesema Gatambi.

Share To:

msumbanews

Post A Comment: