Naibu Katibu Mkuu Dk. Avemaria Semakafu amewataka walimu wanaofundisha wanafunzi wenye mahitaji maalumu Kuacha vitendo vya unyanyapaa kwa wanafunzi hao, kwa kuwa taaluma waliyonayo inahitaji upendo na uvumilivu.

Dk. Semakafu ametoa kauli hiyo mkoani Mwanza wakati akizungumza na walimu hao ambao wanashiriki mafunzo maalumu ya ya siku 10 ya kuchambua mtaala uliobireshwa yenye lengo la kuwajengea uwezo walimu wanaofundisha wanafunzi wenye ulemavu wa akili, wasioona na wanafunzi viziwi.

Dk. Semakafu pamoja na mambo mengine amewataka walimu kuacha masuala vitengo na badala yake walimu wafanye Kazi zao kwa weledi, ikiwa ni pamoja na kuwa wanaharakati katika masuala ya Elimu.

“ Walimu naomba niwaambie ukweli huko kwenye shule zetu tumeanzisha vitengo ambavyo havina sababu yoyote na tumekuwa hatufanyi Kazi zetu kwa weledi, wengine hatufundishi kwa visingizo vya kuwa tunasimamia vitengo, tuache mara moja na badala yake tufundishe watoto wetu kwa weledi,”alisisitiza Dk. Semakafu.

Katika mafunzo hayo baadhi ya Walimu wakata kufahamu kuhusu suala la wanafunzi kuishia Darasa la Sita ambapo Dk. Semakafu alieleza kuwa Elimu inaongozwa na Sheria na Sheria yetu Elimu Msingi ni miaka Saba hivyo Sheria ya Elimu haijabadilika.

Mafunzo hayo yanashirikisha walimu 132 wanaofundisha wanafunzi wenye mahitaji maalumu kutoka mikoa wa Kagera, Geita , Kigoma,Mara,Mwanza, Shinyanga, Simiyu, Rukwa na Tabora.

Imetolewa na:
Kitengo Cha Mawasiliano Serikalini
WIZARA  YA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA
18/8/2018
Share To:

msumbanews

Post A Comment: