Tanzania na Zambia zimekubaliana kutumia kituo kimoja cha forodha kilichojengwa mjini Tunduma.

Lengo na ushirikiano huo ni kupunguza na kudhibiti msongamano wa magari  na uingizwaji wa mizigo kwa njia za magendo.

Makubaliano hayo yamefanyika jana Ijumaa Julai 20, 2018  baina ya naibu kamishna wa forodha  wa mamlaka ya mapato  Tanzania (TRA),  Qamdiyay  Akonaay na kamishina wa forodha  wa mamlaka ya mapato Zambia (ZRA),  Sydney Chibbabbuka  baada ya kukagua miundombinu ya majengo katika mpaka wa  Tunduma na Nakonde.

Akizungumzia na waandishi wa habari mjini Tunduma, Akonaay amesema wamefikia makubaliano hayo  kwa  lengo la kupunguza msongano wa magari na usimamizi wa usafirishaji wa mizigo ili kuongeza mapato  na kuthibiti njia za magendo  za kupitisha bidhaa katika mipaka ya nchi hizo.

"Kituo cha pamoja cha forodha kitaanza kufanya kazi Julai 26 mwaka huu. Wafanyakazi wa ZRA na TRA watafanya kazi katika ofisi moja. Ushirikiano huu utakuwa  chachu ya kukuza uchumi wa mapato  hususani kwa upande wa Tanzania," amesema.

Naye  Chibbabbuka amesema ushirikiano huo utakuwa na faida nyingi katika usafirishaji wa mizigo na kupunguza msongamano uliokuwepo.

Amesema nchini Zamziba tayari wamepata eneo la maegesho ya magari kutoka Tanzania, wanatarajia kuanza ujenzi wa uzio katika eneo hilo mwakani.
Share To:

msumbanews

Post A Comment: