Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Selemani Jafo ametembelea Shule ya Jangwani Sekondari Dar es salaam ambayo imetajwa juzi kuwa miongoni mwa Shule 10 zilizoshika nafasi za mwisho katika matokeo ya kidato cha sita mwaka 2018.

Jafo amesema Shule hiyo ni miongoni mwa Shule chache zenye Walimu wengi lakini imekuwa katika kundi la mwisho 

“Shule ya Jangwani ina walimu 87, Shule ya Kibaha ina Walimu 52, yenye Walimu 52 inakua ya kwanza kitaifa lakini yenye Walimu 87 inakua ya tatu kutoka mwisho kitaifa”

Waziri Jafo ametoa maagizo kwa Katibu Tawala wa Mkoa Afisa wa  Dar abadilishe uongozi lakini pia mabadiliko ya Walimu yafanyike.

“Badilisheni Walimu wa Jangwani, waleteni Walimu wengine waje wafanye mabadiliko hapa, nimepata taarifa kuwa kuna Walimu hawafundishi, watoto wanajipinda wanaandika notes wenyewe, wengine wana moyo wa kusoma lakini Walimu wenye moyo hakuna,”
Share To:

msumbanews

Post A Comment: