Msanii wa kike wa filamu bongo Shamsa Ford ambaye ameolewa na mfanyabiashara maarufu wa nguo Chidi Mapenzi, amesema kwamba kwa anavyofahamu yeye hapa duniani hakuna mwanaume ambaye yupo kwenye mahusiano na mwanamke mmoja pekee na ambaye hasaliti.

Akizungumza kwenye Friday Night Live ya East Africa Television, Shamsa amesisitiza kwamba mwanaume kusaliti ni jambo la kwaida, ila kwenye suala la usaliti kuna kiwango ambacho hakiwezi kuvumilika.

“Mimi ninanvyojua hakuna mwanadamu ambaye yuko perfect, mwanaume kucheat ndivyoa alivyomubwa na Mungu, hamna mwanaume ambaye hacheat, hakuna mwanaume mwenye mwanamke mmoja, Bill Clinton alikuwaga na kesi alicheat, Jay Z alikiri amemcheat Beyonce na uzuri wake na ustar wake, ila kuna utofauti wa cheating, kuna kucheat mtu anamleta mpaka ndani, hiyo haivumiliki”, amesema Shamsa.

Kauli hii ya Shamsa sio mara ya kwanza kusikika akiitamka, ambapo mara ya kwanza aliibua mjadala baada ya tetesi za mume wake kuwa na mchepuko, na kusema kwamba hawezi kumuacha kwa sababu ya  kuchepuka kwani ndio uanaume.
Share To:

msumbanews

Post A Comment: