Video vixen kutoka nchini Kenya, Vera Sidika ameweka wazi majibu aliyoyapata mara baada ya kwenda kupima Ukimwi.

Mrembo huyo amepima ugonjwa huo hatari duniani akiwa na mpenzi wake Otile Brown ambaye ni msanii wa muziki nchini humo.
Vera Sidika ametumia mtandao wa Snapchart kuonyesha majibu ya vipimo vyao ambayo yanaonyesha wote wawili kutohathirika.
Utakumbuku kipindi cha nyuma mrembo Huddah Monroe aliwahi kudai kuwa Vera Sidika ana Ukimwi, ni kipindi ambacho bifu lao lilikuwa limepamba moto.
Vera Sidika alipata umaarufu mkubwa na kuweza kujulikana na wengi mara baada ya kutokea katika video ya kundi la P-Unit ‘You Guy’ iliyotoka mwaka 2012.
Share To:

msumbanews

Post A Comment: