MUIGIZAJI wa Bongo Muvi ambaye pia ni mkali wa Bongo Fleva, Baby Madaha amefunguka kuwa ukitaka kujitia nuksi utoke na mwanaume wa Kibongo kwani wengi wanakupotezea wakati na kukuacha hewani.

Akizungumza na Showbiz Xtra, Madaha alisema kuwa watu wengi hawamuelewi kwa nini hawajawahi kumuona na mwanaume au kumnadi mpenzi wake mitandaoni kwa sababu hapendi kabisa kutoka kimapenzi na Mbongo.

“Watakuja kunisikia tu nimeolewa huko nje ndio watajua ninachomaanisha, sipendi kabisa kumpa penzi Mmbongo kwa sababu wengi wababaishaji na wanajua kutiana nuksi sana kwakweli alisema
Share To:

msumbanews

Post A Comment: