Mwanamke mmoja aliyefahamika kwa jina la Mary Miyombo (32), mkazi wa Kata ya Hombolo, Bwawani mkoani Dodoma   amenusurika kufa baada ya kukatwa koromeo na mumewe wake akiyejulikana kwa jina la Mgowela Anderson.

Chanzo cha kisa hicho kilichotokea Mei 16, mwaka huu kinaelezwa ni wivu wa kimapenzi ambapo inadaiwa mwanamke huyo alikutwa na mwanamume mwingine ndipo mumewe akamjeruhi kwa kumkata na panga kwenye koromeo na kukimbia.

Akizungumza kwa tabu huku akilia, Mary ambaye kwa sasa amelazwa katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Dodoma   amesema siku ya tukio akiwa ametoka kuuza pombe kilabuni kijijini hapo alifika nyumbani kwake na kwenda anapoweka fedha zake ambapo aligundua 1,000 haipo jambo lililosababisha kumuuliza mume wake huyo.

“Nilipomuuliza tu kama amechukua hiyo hela ndipo kipigo kilipoanza hadi kufikia hatua ya kunikata na panga shingoni, yaani simtaki tena yule mwanamume kwani hii ni mara ya tatu ananipiga na kunijeruhi na nimekuwa nikimsamehe lakini kwa hili simtaki tena,” amesema Mary.

Mganga Mfawidhi wa hiyo, Caroline Damian amethibitisha kumpokea mgonjwa huyo hospitalini ambaye alilazwa wodi namba 10 na tayari amesharuhusiwa.

Hata hivyo, Kamanda wa polisi Mkoani Dodoma Gilles Muroto alipotafutwa kuzungumzia tukio hilo hakupatikana.
Share To:

msumbanews

Post A Comment: