Rais John Magufuli jana amewapandisha vyeo maofisa wa Jeshi la Ulinzi wa Wananchi (JWTZ) akiwamo Meja Jenerali Peter Massao aliyepandishwa kuwa Luteni Jenarali.

Taarifa iliyosomwa na Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Tanzania, Jenerali Venance Mabeyo jana Aprili 12, Ikulu Jijini Dar es Salaam imeeleza kuwa Meja Jenerali Massao ni Mkuu wa Chuo cha Mafunzo ya Maaofisa Wanafunzi wa Jeshi Monduli (TMA) na kwa uteuzi huo, sasa JWTZ itakuwa na maluteni jenerali wawili.

Wengine waliopandishwa vyeo na Rais Magufuli ni Brigedia Jenerali Henry Kamunde aliyepandishwa na kuwa meja jenerali.

Pia amewapandisha vyeo maofisa 27 wa JWTZ kutoka cheo cha kanali na kuwa brigedia jenerali na ofisa mmoja kutoka luteni kanali na kuwa kanali.

Waliopandishwa vyeo hivyo ni D.D.M Mullugu, J.J Mwaseba, A.S Mwamy, R.K Kapinda, C.D Katenga, Z.S Kiwenge, M.A Mgambo, A.M Alphonce, A.P Mutta, A.V Chakila, M.G Mhagama, V.M Kisiri, C.E Msolla na S.M Mzee.

Wengine ni C.J Ndiege, I.M Mhona, R.C Ng’umbi, S.J Mnkande, A.C Sibuti, M.M Mumanga, I.S Ismail, M.N Mkeremy, G.S Mhidze, M.A Machanga, S.B Gwaya, P.K Simuli na M.E Gaguti.
Share To:

msumbanews

Post A Comment: