Mbunge wa Misungwi, Charles Kitwanga (CCM), amedai vitambulisho vya wabunge vina kamba ambazo baadhi ya wabunge wanaweza kuzitumia kujinyonga hivyo viondolewe.

Akiomba mwongozo bungeni leo Ijumaa Aprili 6, Kitwanga amesema kutokana na hali hiyo ni kwanini Bunge lisione umuhimu wa kutumia vitambulisho vya kisasa badala ya hivyo.

“Maana hivi vina kamba ambazo nina wasiwasi watani wangu kama Lukuvi (Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi) na wahehe wanaweza kujinyonga,” amesema Kitwanga.

Akijibu mwongozo huo, Mwenyekiti wa Bunge, Andrew Chenge amesema ni lazima waende na wakati kwa kutumia vitambulisho vya kisasa ambavo ni hivyo
Share To:

msumbanews

Post A Comment: