AMAZING! Hiyo ndiyo kauli pekee unayoweza kuitamka kuakisi shoo baab’kubwa aliyoifanya mkali wa wimbo wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’, jijini Nairobi nchini Kenya usiku wa kuamkia leo.

Bonge hilo la shoo iliyojulikana kama Safaricom Private Party, Chibu alikimbiza vibaya jukwaani huku warembo wakipagawishwa na performance yake na kujikuta wakizama jukwaani kucheza naye.

Diamond ameacha gumzo la aina yake nchini humo kutokana na kupata idadi kubwa ya mashabiki, huku burudani zikibamba vilivyo.
 


Share To:

msumbanews

Post A Comment: