Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Manendeleo (CHADEMA), Freeman Mbowe amefunguka na kuonyesha wasiwasi juu ya Jeshi la polisi kutaka kuwabambikizia kesi za mauaji au uhaini ili waweze kuwekwa mahabusu muda mrefu. 
Mbowe amesema hayo leo Machi 22, 2018 ikiwa ni siku ambayo yeye pamoja na viongozi wengine wa chama hicho wanatakiwa kufika katika kituo cha polisi kusikiliza wito wa jeshi hilo na kusema kuwa wamepata taarifa zingine kuwa Mbunge wa Iringa Mjini Mchungaji Peter Msigwa anataka kuhusishwa katika shauri hilo ambalo wao wanalo. 
"Tuna taarifa pia ya kusudio la kumuunganisha Mhe. Peter Msigwa, Mb, Mwenyekiti wa CHADEMA Kanda ya Nyasa (Rukwa, Songwe, Mbeya, Njombe na Iringa) na Mjumbe wa Kamati Kuu katika shauri hili. Lakini pia katika wakati nenda rudi hii ikiendelea, tuna taarifa (asante teknolojia) kuwa zinapangwa njama mahususi za kutubambikia viongozi wa Chadema kesi za mauaji au Uhaini ili kuhalalisha azma ya Watawala kutuweka mahabusu kwa muda mrefu, wakidhani kwa kufanya hivyo watakuwa wamefanikisha kufifisha na hata kuua kabisa uwepo wa Upinzani katika Taifa" alisema Mbowe 
Share To:

msumbanews

Post A Comment: