Mchekeshaji kutoka kundi la Timamu, Ebitoke amejibu tuhuma kuwa amekuwa akitoka kimapenzi na mume wa Mamaa Ashura.
Muigizaji huyo amesema kuwa tuhuma hizo hazina ukweli wowote ni stori tu za kupikwa.
“Kwa wale wanaosema mimi nimempindua si kweli wakati yupo tumemficha sehemu, tutamleta,” Ebitoke ameiambia Bongo5.
“Mama Ashura yupo na anaendelea na mambo mengine, atarudi kama mwanzo na wataendelea kumuona ila sasa hivi hayupo kidogo, kuna mambo ambayo anayafanya,” ameongeza.
Hapo awali kulikuwa na taarifa kuwa baada ya Ebitoke kuanza kutoka kimapenzi na mume wa Mamaa Ashura ndipo kumepelekea muigizaji huyo kutoonekana tena katika kundi hilo.
Share To:

msumbanews

Post A Comment: