Madiwani wawili  wa Chadema, katika Mkoa wa Mara  wametangaza kujiuzulu na kujiunga na Chama cha Mapinduzi ( CCM).

Diwani wa kata ya Ikoma Ndg. Michael Machaba na Diwani wa kata ya Machira Ndg. Joseph Paulo  wamejiuzulu uanachama na udiwani leo hii na kutangaza kujiunga na ccm kwa kile walichoeleza kuwa wamefanya hivyo ili kuunga mkono juhudi za Mh Rais Magufuli. 

Msumbanews Blog ilipomtafufa Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo kwa njia ya simu ili kuzungumzia swala la madiwani hao alisema halitambui swala hilo maana madiwani hao wamekwenda kutangazia kujiuzulu kwao Nje ya Mkoa huo.
Share To:

msumbanews

Post A Comment: