Naibu Waziri wa Fedha, Mhe.Mshamu Munde,akimkabidhi tuzo Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano cha FCC, Bi. Roberta Feruzi kwa niaba ya Waziri wa Fedha tuzo hiyo imetolewa kwa Tume ya  Ushindani (FCC)  kutambua mchango wake katika maendeleo ya Sekta ya Manunuzi na Ugavi nchini.Hafla ya utoaji wa tuzo hiyo ilifanyika katika Kongamano la 16 la Wataalamu wa Manunuzi na Ugavi,lililoandaliwa na Bodi ya Wataalamu na Mafundi wa Ununuzi na Ugavi (PSPTB)   jijini Arusha.

....

TUME ya Ushindani (FCC) imetunukiwa tuzo maalum ya kutambua mchango wake katika maendeleo ya Sekta ya Manunuzi na Ugavi nchini.

Tuzo hiyo imekabidhiwa na Naibu Waziri wa Fedha, Mhe. Mshamu Munde, kwa niaba ya Waziri wa Fedha, na kupokelewa na Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano cha FCC, Bi. Roberta Feruzi.

Hafla ya utoaji wa tuzo hiyo ilifanyika katika Kongamano la 16 la Wataalamu wa Manunuzi na Ugavi, lililofanyika katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Arusha (AICC), jijini Arusha lililoandaliwa na Bodi ya Wataalamu na Mafundi wa Ununuzi na Ugavi (PSPTB).

FCC imeshiriki kongamano hilo kama mdau muhimu wa sekta ya manunuzi na ugavi, ambapo iliwasilisha mada kuhusu umuhimu wa ushindani wa haki katika masuala ya manunuzi na ugavi, hususan katika kulinda mnyororo wa thamani.

Kupitia kongamano hilo, Tume pia ilitoa elimu kwa wadau mbalimbali kuhusu majukumu na kazi zake, ikisisitiza nafasi yake katika kuhakikisha mazingira ya ushindani yanayochochea uwazi, ufanisi na maendeleo endelevu ya sekta ya manunuzi na ugavi nchini.

Naibu Waziri wa Fedha, Mhe.Mshamu Munde,akimkabidhi tuzo Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano cha FCC, Bi. Roberta Feruzi kwa niaba ya Waziri wa Fedha tuzo hiyo imetolewa kwa Tume ya  Ushindani (FCC)  kutambua mchango wake katika maendeleo ya Sekta ya Manunuzi na Ugavi nchini.Hafla ya utoaji wa tuzo hiyo ilifanyika katika Kongamano la 16 la Wataalamu wa Manunuzi na Ugavi,lililoandaliwa na Bodi ya Wataalamu na Mafundi wa Ununuzi na Ugavi (PSPTB)  jijini Arusha.

Naibu Waziri wa Fedha, Mhe.Mshamu Munde,akimkabidhi tuzo Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano cha FCC, Bi. Roberta Feruzi kwa niaba ya Waziri wa Fedha tuzo hiyo imetolewa kwa Tume ya  Ushindani (FCC)  kutambua mchango wake katika maendeleo ya Sekta ya Manunuzi na Ugavi nchini.Hafla ya utoaji wa tuzo hiyo ilifanyika katika Kongamano la 16 la Wataalamu wa Manunuzi na Ugavi,lililoandaliwa na Bodi ya Wataalamu na Mafundi wa Ununuzi na Ugavi (PSPTB)   jijini Arusha.

 Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Ushindani (FCC) Bi. Khadija Ngasongwa,akizungumza katika Kongamano la 16 la Wataalamu wa Manunuzi na Ugavi, lililoandaliwa na Bodi ya Wataalamu na Mafundi wa Ununuzi na Ugavi (PSPTB)   jijini Arusha.

Meneja Huduma za Sheria FCC Bw. Josephat Mkizungo, akitoa mada katika Kongamano la 16 la Wataalamu wa Manunuzi na Ugavi,lililoandaliwa na Bodi ya Wataalamu na Mafundi wa Ununuzi na Ugavi (PSPTB)   jijini Arusha.

 Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Ushindani (FCC) Bi. Khadija Ngasongwa,akifuatilia mada mbalimbali wakati wa Kongamano la 16 la Wataalamu wa Manunuzi na Ugavi,lililoandaliwa na Bodi ya Wataalamu na Mafundi wa Ununuzi na Ugavi (PSPTB)   jijini Arusha.

 Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Ushindani (FCC) Bi. Khadija Ngasongwa (kushoto),akifuatilia mada mbalimbali wakati wa Kongamano la 16 la Wataalamu wa Manunuzi na Ugavi, lililofanyika  jijini Arusha .Katikati ni Afisa Mtendaji Mkuu wa BRELA, Bw. Godfrey Nyaisa na Kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Missenyi Bw. John Paul Wanga.lililoandaliwa na Bodi ya Wataalamu na Mafundi wa Ununuzi na Ugavi (PSPTB) .

Naibu Waziri wa Fedha, Mhe.Mshamu Munde,akiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kukabidhi tuzo kwa  Tume ya  Ushindani (FCC) ya kutambua mchango wake katika maendeleo ya Sekta ya Manunuzi na Ugavi nchini.Hafla  ilifanyika katika Kongamano la 16 la Wataalamu wa Manunuzi na Ugavi, lililoandaliwa na Bodi ya Wataalamu na Mafundi wa Ununuzi na Ugavi (PSPTB)   jijini Arusha.

 

Na Mwandishi Wetu, Handeni TC

Mkuu wa Wilaya ya Handeni, Mhe. Salum Nyamwese, amesema wilaya hiyo imejipanga kikamilifu kuhakikisha wananchi wanahamasika kujiunga na Bima ya Afya kwa Wote ili kuwa na uhakika wa kupata huduma bora za matibabu.

Akizungumza mjini Handeni, Mhe. Nyamwese amesema kuwa katika wilaya hiyo yenye Halmashauri ya Mji Handeni na Halmashauri ya Wilaya ya Handeni, Serikali imewekeza kwa kiasi kikubwa katika ujenzi wa miundombinu ya kisasa ya kutolea huduma za afya.

Amesema kuwa katika kuhakikisha wananchi wananufaika na bima ya afya kwa wote, wilaya imejiandaa kikamilifu kwa kuweka mazingira wezeshi ya utoaji huduma ikiwemo upatikanaji wa vituo vya afya, vifaa tiba, dawa pamoja na rasilimali watu.

“Wilaya yetu tumejipanga na tuna mikakati madhubuti ya kuhakikisha tunamsaidia Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan, kutimiza ahadi yake kwa Watanzania ya kuhakikisha wanapata huduma bora za afya kupitia bima ya afya kwa wote,” amesema Mhe. Nyamwese.

Amebainisha kuwa ndani ya wilaya ya Handeni kuna jumla ya vituo 84 vya kutolea huduma za afya ambavyo vimepatiwa vifaa tiba kulingana na ngazi ya utoaji huduma.

Aidha amesema huduma za kibingwa zinatolewa katika hospitali za wilaya kwa kushirikiana na wataalamu kutoka hospitali za rufaa za kikanda, hatua inayolenga kuhakikisha wananchi wanapata huduma karibu na maeneo yao.

Kuhusu upatikanaji wa dawa, Mkuu wa Wilaya amesema kuwa kwa sasa hali ni nzuri kwani zaidi ya asilimia 90 ya dawa zinapatikana katika hospitali zote za wilaya.

Ameongeza kuwa wilaya inatarajia kupokea wataalamu zaidi wa afya ili kuimarisha utoaji wa huduma, kutokana na Serikali tayari kuwekeza katika miundombinu na vitendea kazi.

“Nitoe wito kwa wananchi kutumia fursa ya bima ya afya kwa wote. Tusiiache itupite. Tutatangaziwa utaratibu wa kujiunga nayo na ni muhimu sisi wananchi kuwa mstari wa mbele kunufaika na fursa hii, kwani ina faida kubwa katika kupanua wigo wa upatikanaji wa huduma za afya,” amesisitiza Mhe. Nyamwese.

 


Na Munir Shemweta, WANMM TABORA

 

Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Dkt Leonard Akwilapo amewataka wahitimu wa chuo cha ardhi Tabora (ARITA) kuingia kwenye dunia ya kazi kwa moyo wa uadilifu, uzalendo na ubunifu. 

 

Amesema, Taifa linawategemea wahitimu hao sambamba na kuhitaji wataalamu wanaoweza kutumia elimu kwa manufaa ya wote na si kwa maslahi binafsi.

 

"Tumieni utaalamu wenu kwa weledi, uadilifu na kufuata sheria. Epukeni kabisa mambo ya rushwa na ufisadi". Amesema.

 

Mhe. Dkt Akwilapo ametoa kauli hiyo leo tarehe 19 Desemba 2025 katika Mahafali ya 43 Chuo cha Ardhi Tabora (ARITA) yaliyofanyika chuoni hapo mkoani Tabora.

 

Aidha, amewataka wahitimu hao wa chuo cha ARITA kuendelea kujifunza kwa kuwa  elimu haina mwisho na kusisitiza kuwa anataka kuona elimu waliyoipata inakuwa  na manufaa kwa Taifa na sio machungu kwa Taifa.

 

"Muwe mabalozi wema wa Chuo. Msidanganyike na yanayoandikwa kwenye mitandao kwamba nyie ni kundi la wanajamii wenye ukaidi, wasio na utii, wala heshima kwa wazazi, viongozi na Serikali,  Nyinyi ni hazina ya Taifa". Amesema

 

Mkuu wa wilaya ya Tabora Bi. Upendo Wella amewataka wahitimu wa chuo hicho kutumia vizuri utaalamu na ujuzi walioupata kwa kushirikiana na jamii katika kutatua changamoto za sekta ya ardhi.

 

"Wahitimu kama hamna ajira mkajiunge katika vikundi na muanzishe shughuli,elimu mliyopata mkaitumie vyema". Amesema

 

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Bodi ya Ushauri ya Chuo cha Ardhi Tabora Dkt Lucy Shule amesema, chuo hicho kinaendelea kufanya maboresho mbalimbali yatakayokiwezesha chuo kuwa na miundombinu ya kisasa ya kufundishia na kujifunza.

 

Kwa mujibu wa Dkt Shule, maboresho hayo yatakiwezesha chuo cha Ardhi Tabora kuwa na uwezo wa kuongeza udahili na kozi mpya.

 

Mkuu wa chuo cha Ardhi Tabora Bw. Jeremiah  Minja amesema, chuo chake ni miongoni mwa vyuo vichache nchini vinavyotoa mafunzo ya uchapishaji wa nyaraka nchini.

 

"Kutokana na kuongezeka kwa mahitaji ya kazi za uchapishaji katika ngazi ya Wizara na wateja wengine na  kutokana na Wizara kukipa Chuo mtambo mkubwa wa uchapishaji uliopo Dar es Salaam chuo kina nia ya kuanzisha karakana nyingine ya uchapishaji katika Jiji la Dar es Salaam".Amesema Bw. Minja.

 

Katika risala yao iliyosomwa na Yohana Mhendi wahitimu wa chuo hicho wameishukuru Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa kuboresha mazingira ya chuo ikiwemo miundombinu ya kujifunzia kama vile kumbi za Mihadhara na Maktaba.

 

Katika mahafali hayo ya 43 ya chuo  cha Ardhi Tabora, jumla ya wanafunzi 688 walihitimu ambapo kati ya hao kozi za Sanaa, Ubunifu na Uchapishaji ni 28, Kozi za Urasimu Ramani ni 126, Kozi za Usimamizi wa Ardhi, Uthamini na Usajili ni 483, Kozi za Usimamizi wa Mazingira ni 22 na Kozi za Mfumo wa Taarifa za Kijiografia ni 29. 


 

 

BARAZA la Ushindani (FCT) jana Desemba 18, 2025, limeendesha semina ya elimu kwa wadau mkoani Mbeya kwa lengo la kuongeza uelewa kuhusu majukumu na huduma zinazotolewa na Baraza hilo.

Semina hiyo ilifanyika katika Ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mbeya na kufunguliwa na Katibu Tawala Msaidizi – Viwanda, Biashara na Uwekezaji Mkoa wa Mbeya, Bi Anna Mwambene, ambaye aliwahimiza wadau kutumia ipasavyo mifumo ya kisheria iliyopo na kuwa mabalozi wa kuitangaza huduma za Baraza la Ushindani.

Bi Mwambene alisema uelewa wa sheria na taratibu za ushindani ni muhimu katika kukuza mazingira bora ya biashara na uwekezaji, akisisitiza umuhimu wa wadau kushiriki kikamilifu katika kulinda haki zao kwa kutumia mifumo rasmi iliyowekwa na Serikali.

Katika semina hiyo, Baraza la Ushindani liliwapatia washiriki elimu kuhusu matumizi ya mfumo wa kidijitali wa kuwasilisha rufaa zinazotokana na maamuzi ya Tume ya Ushindani (FCC) pamoja na mamlaka mbalimbali za udhibiti, zikiwemo LATRA, EWURA, TCRA, TCAA na PURA.

Akizungumza wakati wa mafunzo hayo, Afisa TEAMA wa Baraza la Ushindani, Bw Athuman Kanyegezi, alisema mfumo huo unamwezesha mtumiaji kuanzisha akaunti, kuwasilisha rufaa kwa njia ya mtandao, kupakia nyaraka husika, kulipa ada na kufuatilia hatua za mwenendo wa kesi bila kulazimika kufika ofisini.

Aliongeza kuwa matumizi ya mfumo wa kidijitali yanalenga kurahisisha upatikanaji wa haki, kuongeza uwazi na kupunguza gharama na muda kwa wadau wanaohitaji huduma za Baraza hilo.

Semina hiyo iliwahusisha wafanyabiashara, wajasiriamali na wawakilishi wa taasisi mbalimbali, ambapo washiriki walipata fursa ya kuuliza maswali na kupata ufafanuzi kuhusu taratibu za rufaa na utoaji wa haki kwa njia ya kidijitali.

Kuanza safari ya siasa bila pesa nyingi ni changamoto kubwa kwa mwanasiasa mpya. Nilichojifunza mapema ni kwamba umaarufu wa kweli hauanzi na fedha, unaanzia kwa watu.

Wananchi wanahitaji kuona, kusikia, na kuhisi kuwa uko nao, si juu yao. Hii ndiyo msingi wa kujijenga kisiasa bila bajeti kubwa. Hatua ya kwanza ni kuwa karibu na wananchi.

Kutembelea vijiwe, masoko, mikutano ya kijamii na hata mazishi kunajenga jina lako polepole. Kusikiliza matatizo yao bila kutoa ahadi zisizotekelezeka hujenga heshima na uaminifu.

Watu wanapokujua kama mtu wa kwao, huanza kukutangaza wenyewe. Hatua ya pili ni kutumia hadithi yako binafsi. Wananchi huamini simulizi za kweli kuliko hotuba ndefu.

Nilielewa kuwa kueleza nilipotoka, changamoto nilizopitia, na sababu ya kuingia siasani kulinifanya nieleweke zaidi. Hadithi ya kweli huunganisha hisia na kuvuta uungwaji mkono.Soma Zaidi.........
https://kiwangadoctor.com/kiswahili/jinsi-mwanasiasa-mpya-anaweza-kujijenga-na-kupata-umaarufu-bila-pesa-nyingi/
Kwa muda mrefu nilikuwa naishi nikiwa nimechoka kiakili kuliko kimwili. Mawazo hayakuacha kunizunguka, usingizi ulikuwa shida, na hata mambo madogo yalionifanya nihisi nimeelemewa.

Nilitabasamu mbele ya watu, ila ndani nilikuwa navunjika polepole. Nilidhani huu ndio mwisho wangu, kwamba msongo wa mawazo ulikuwa umenishinda kabisa. Nilijaribu kujituliza kwa kujishughulisha, kuzungumza na marafiki, hata kujilazimisha kuwa na nguvu.

Hakuna kilichodumu. Kila nikikaa peke yangu, mawazo yalirudi kwa nguvu zaidi. Hofu isiyoelezeka, huzuni ya ghafla, na kukosa matumaini vilikuwa sehemu ya siku zangu za kawaida.Soma Zaidi...........
https://kiwangadoctor.com/kiswahili/nilidhani-msongo-wa-mawazo-umenishinda-nilijifunza-kuponya-akili-yangu/
Nilianza kunywa pombe kama burudani ya kawaida. Ilikuwa njia ya kupunguza msongo wa mawazo baada ya kazi na kusherehekea wikendi na marafiki. Kadri muda ulivyopita, pombe ikawa sehemu ya maisha yangu ya kila siku.

Nilichelewa kazini mara kwa mara, nilianza kukosa umakini, na hatimaye nikapoteza ajira niliyokuwa nimeitumikia kwa miaka.
Marafiki waliondoka mmoja baada ya mwingine. Familia ilianza kuniona kama mzigo.

Heshima yangu iliporomoka taratibu. Kila nilipojaribu kuacha, nilishindwa. Nilijilaumu, nilijificha, na nilianza kuamini kuwa nilikuwa nimeharibiwa kabisa. Soma Zaidi..............
https://kiwangadoctor.com/kiswahili/pombe-ilinifanya-nipoteze-kazi-marafiki-na-heshima-safari-ya-kuacha-ilikuwa-ngumu-inawezekana/

 


Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Mhandisi Maryprisca Mahundi, ameagiza  Chuo  cha Maendeleo ya jamii Uyole   kupitia  dhana  ya  ushirikishwaji  jamii kupinga  vitendo  vya  ukatili  wa kijinsia  na  kutaka  kazi    hiyo kuwa  endelevu ndani  na  nje ya chuo 

Mahundi  amezungumza  hayo  wakati  wa mahafali  ya kumi  na  sita  ya  chuo  cha  maendeleo  ya  jamii  CDTI uyole  yaliofanyika  viwanja  vya michezo  chuo cha maendeleo  ya jamii  Uyole  na kusema  licha  ya  siku  kumi na  sita  za kupinga ukatili  kufanyika  lazima   zoezi hilo  likawe  endelevu

Ameitaka    jamii  inayozunguka  Chuo na kila  mwanafunzi   ni  vema kila  mmoja  akawa mjumbe kupeleka  elimu  ya kupinga ukatili  hasa  wanaporudi  nyumbani  au  katika  sehemu za kazi.

Mahundi  amesema  ni  mategemeo  ya  Wizara na  Serikali  kwa  ujumla kuwa  watumishi  na wanafunzi  wa  Chuo  hicho  wataendelea  kutimiza  wajibu  kwa  kufanya  kazi  kwa  bidii na kuendelea  kuzingatia  sheria,taratibu,kanuni   na  miongozo mbalimbali  ya Kitaifa na   kama  wakifanya  hivyo  wataendelea  kutoa  wahitimu mahili na wenye maadili  mema  wanaoweza  kushindana  katika soko  la  ajira .   

Amesema  mustakabali  wa  Taifa  lolote  duniani  unategemea  sana mchango wa Taasisi  za mafunzo  katika  kuandaa wataalamu mahili na  wenye  weredi  ambao  ndio  chachu  ya kuleta mageuzi  ya kifkra na maendeleo  jumuishi  na  endelevu  katika  jamii  yoyote

Naibu  Waziri  Mahundi  ameongeza  kuwa  Wizara  inatambua  mchango  mkubwa uliotolewa  na Chuo  cha maendeleo  ya  jamii Uyole  katika  kuanda  wataalamu wa maendeleo  ya jamii ambao  wanatoa  mchango  mkubwa  katika  maendeleo  ya taifa  na  kuwapongeza wakufunzi  kwa  kufanya  kazi hiyo kwa uweledi.

Mhandisi  Mahundi  amesema  katika  kutekeleza  dhana  ya  uanagenzi ,ubunifu  na  kusema  kama   zitatekelezwa vyema zitawawezesha  wahitimu  kuajiliwa  kwa  urais  zaidi,kijiajili  na kuajili  wengine  huku  jamii  inayozunguka  Chuo hicho  ikinufaika  na mafunzo  hayo.

Kwa  upande  wake  Mkurugenzi    anayesimamia  vyuo vya Maendeleo  ya  jamii  nchi  kutoka  Wizara  ya Maendeleo  ya  jamii.jinsia   na makundi maalumu Neema Ndoboka amesema  vyuo  vya maendeleo  ya jamii nchini  vimekuwa  na mchango mkubwa  na  kwenda  maeneo mbalimbali  hapa nchini  katika  kwenda kuleta maendeleo   hasa  vijijini na mashirika mengine

Awali  akisoma  taarifa  ya  chuo   hicho  makamu  mkuu wa  chuo  anaeshughulikia  taaluma    Spay Mwangomile amesema kwa  ujumla  nidhamu ya  wanafunzi  imekuwa  ya  kuridhisha uku  wakifundishwa  maadili  mema,uadilifu   na  uwajibikaji  popote  watakapokuwa  wakiwa  kama  mabalozi  wa  chuo  hicho na kuwataka  wanafunzi  waliohitimu chuo hicho   kuwa  wabunifu

Jumla ya  wahitimu     530  wanawake  272 na  258 wanaume  wamehitimu  katika  mahafali  ya  Chuo  hicho  katika  ngazi  ya  aatashahada na  shahada.










 


Naibu Waziri wa Fedha, Mhe. Mshamu Ali Munde amesema Mradi wa Elimu ya Juu kwa Mageuzi ya Kiuchumi (HEET) ni sehemu muhimu ya mageuzi ya elimu ya juu nchini. 

Mhe. Munde ameyasema hayo Disemba 19, 2025 katika Mahafali ya 27 ya Chuo cha Uhasibu Arusha, yaliyofanyika katika Kampasi ya Arusha.

Mhe. Munde amesema kupitia Mradi wa HEET, IAA imeboresha miundombinu ya kufundishia na kujifunzia , imejenga na kukarabati wa majengo ya kisasa katika Kampasi za Arusha, Babati na Songea na hivyo  kuongeza uwezo  wa chuo kupokea wanafunzi wengi zaidi.

Mhe. Munde ameongeza kuwa IAA imenunua vifaa vya TEHAMA vya kisasa na kutengeneza madarasa janja (smart glasses) na kutoa mafunzo kwa  Wahadhiri ili waweze kufundisha kwa mbinu zinazokidhi viwango vya kimataifa.

Mwenyekiti wa Baraza la Uongozi wa Chuo IAA, Dkt. Mwamini Tulli chuo kinaendelea kuboresha na kupanua miundombinu ya kufundishia na kujifunzia ikiwemo madarasa, ofisi za wahadhiri, maktaba na miundombinu ya TEHAMA katika kampasi zake zote za Arusha, Babati, Dar es Salaam, Dodoma na Songea. Vile vile, chuo kinaendelea kujipanga kuwekeza nguvu na rasilimali katika ujenzi wa kampasi mpya ya Bukombe.

Naye Mkuu wa Chuo IAA, Prof. Eliamani Sedoyeka amesema, " IAA inawaandaa wahitimu wake kukidhi mahitaji ya soko la ajira kwa kuajiriwa na kujiajiri wenyewe. IAA tumewajengea uwezo wanafunzi kuanzisha miradi yao, ambapo baadhi  wameanzisha biashara na kusajili makampuni ambayo yametoa nafasi kwa wanafunzi wetu kujiajiri na kuajiri vijana wenzao".