Na Munir Shemweta, WANMM MOROGORO

Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Dkt Leonard Akwilapo amewaasa wahitimu wa Chuo cha Ardhi Morogoro (ARIMO) kujiepusha na matendo maovu na elimu na maarifa waliyopata yawe tunu na faida kwa Taifa.

Mhe. Dkt Akwilapo ametoa wito huo tarehe 12 Desemba 2025 wakati wa mahafali ya 44 ya Chuo cha Ardhi Morogoro (ARIMO) yaliyofanyika mkoani Morogoro ambapo jumla ya wahitimu 450 wa fani za Jiomatikia (Upimaji Ardhi), Upangaji Miji na Vijiji na Mifumo ya Taarifa za Kijiografia (GIS) walitunukiwa Astashada na Stashahada katika fani hizo.

Mhe. Dkt Akwilapo amewataka wahitimu hao kukumbuka kuwa utii, nidhamu na tabia njema ni silaha itakayowafanya wapendwe mahali popote.

‘’Tukiwa hapa Morogoro tunakumbuka maneno yaliyoimbwa na mwanamuziki wa hapa hayati Mbaraka Mwinshehe na bendi yake ya Okestra Volcano; alisema “Heshima Kijana tanguliza kwanza mbele, ujeuri mbaya; uzuri si hoja tabia njema ni silaha utapendwa popote” mwisho wa kunukuu, alisema Mhe. Dkt Akwilapo.

Amewataka vijana kutodanganyika na maneno ya eti kuna watu wanaitwa Gen Z ambapo alieleza kuwa, hizo ni propaganda za kujenga hofu na kufifisha juhudi za nchi maskini kujitafutia maendeleo.

“Msidanganywe kuwa eti nyie ni kizazi cha vijana wasio na nidhamu, wapenda fujo, wasiosikiliza wazee wao, viongozi wao, chenye kujiamulia mambo yao bila kufuata sheria, taratibu, miongozo na tamaduni zetu; na mambo mengine ya hovyo’’ amesisitiza Mhe. Dkt Akwilapo.

Kwa mujibu wa Waziri huyo wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi, inasikitisha na kushangaza kuona vijana wa Kitanzania wanasikiliza maelekezo ya watu ambao hawaishi Tanzania na wala hawajawahi kuwaona na kupuuza  maelekezo ya Viongozi wao na hata wazazi wao ambao wamewalea mpaka hapo walipoifikia.

Amesema, kuhitimu masomo kunatakiwa kuendane na uzalendo waliojengewa wa kuipenda Tanzania na kusisitiza kuwa waithamini nchi yao.

Mhe. Dkt Akwilapo amewataka kutumia utaalamu walioupata kwa weledi, uadilifu na kufuata sheria, kanuni, taratibu na miongozo na kuepuka vitendo vinavyoenda kuhatarisha amani.

Vile vile amewataka kuendelea kujifunza kwani elimu ni bahari, haina mwisho na kuwataka wanaobaki chuoni kuongeza bidii katika masomo, nidhamu na kutunza amani na umoja kwani kesho yao inajengwa na maamuzi ya leo.

Kwa upande wake Mkuu wa wilaya ya Morogoro, Bw. Musa Ramadhani Kilakala akimuwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Bw. Adam Malima amesema, migogoro ya ardhi imepungua mkoani humo hasa pale wizara ya ardhi ilipoanzisha Kliniki za Ardhi ambazo amezieleza zimesaidia kwa kiasi kikubwa kuwafikia wananchi katika maeneo yao.

Akitoa taarifa kwa Mgeni Rasmi, Mkuu wa Chuo cha Ardhi Morogoro (ARIMO) Charles Saguda amesema chuo hicho kina Mpango Kabambe wa Miaka 20 (2023-2043) unaolenga kuboresha mazingira ya kujifunza na kujifunzia na utendaji wa chuo katika kuwaandaa wataalamu wa sekta ya ardhi.

“Mpango kabambe huu unalenga kuongeza udahili wa wana chuo kutoka 660 hadi 5000, kuongeza watumishi kutoka 58 hadi 310 kuongeza program za mafunzo ya wanafunzi kutoka 2 hadi 7 pamoja na kujenga kampasi mpya katika eneo Mlima Kola mkoani Morogoro’’. Amesema Bw. Saguda




Na Munir Shemweta, WANMM MOROGORO

 

Mkuu wa mkoa wa Morogoro Bw. Adam Malima ameipongeza Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa kuweka kumbukumbu za ardhi vizuri jambo alilolieleza kuwa linasaidia katika utatuzi wa migogoro ya ardhi.

 

‘’Mhe Waziri kwa kweli nitoe pongezi kwa wizara yako kwa kuwa na kumbukumbu nzuri za wamiliki wa ardhi jambo hili limetusaidia kama mkoa wa morogoro kutatua migogoro ya ardhi pale inapojitokeza’’ amesema Bw. Malima

 

Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi moja ya vipaumbele vyake ni katika mwaka wa fedha 2025/2026 ni kuongeza kasi ya upangaji, upimaji, umilikishaji na usajili wa ardhi mijini, vijijini na katika maeneo ya kimkakati.

 

Bw. Malima amesema hayo tarehe 12 Desemba 2025 ofisini kwake alipokutana na Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Dkt Leonard Akwilapo aliyekuwa mkoani humo kwa ajili ya kuhudhuria mahafali ya 44 ya Chuo cha Ardhi Morogoro (ARIMO).

 

Amesema, migogoro ya ardhi katika mkoa wake wa Morogoro imepungua kwa kiasi kikubwa kutokana na juhudi kubwa za wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi kupitia ofisi ya Kamishna wa Ardhi Msaidizi mkoa ambapo imefanya kazi kubwa ya kufikia wananchi kupitia Kliniki ya Ardhi.

 

Kwa upande wake Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Dkt Leonard Akwilapo alimueleza mkuu wa mkoa wa Morogoro kuwa, wizara yake kwa sasa inafanya juhudi kubwa kuhakikisha migogoro ya ardhi iliyopo inatatuliwa na hakuna migogoro mipya inayozalishwa kwenye maeneo mbalimbali nchini.

 

‘’Nikuhakikishe RC sisi ndani ya wizara tumejiwekea mikakati ya kuhakikisha migogoro iliyopo tunaimaliza lakini pia hakuna migogoro mipya inayozalishwa’’ amesema Mhe. Dkt Akwilapo.

 

Aidha, Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi amezihimiza taasisi za umma kuhakikisha zinalinda maeneo yao ili kuepuka uvamizi alioueleza kuwa ndiyo unaochangia kwa kikubwa migogoro ya ardhi katika maeneo ya umma.

 


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Ridhiwani Kikwete amesema Wizara hiyo imefanya maboresho mbalimbali ya mifumo yake ikiwemo mfumo wa e- mrejesho, ili kutoa fursa zaidi kwa wananchi wa pembezoni kutoa maoni, malalamiko na pongezi kuhusu huduma zinazotolewa na serikali na Taasisi zake.

Mhe. Ridhiwani amebainisha hayo wakati akizungumza na waandishi wa habari Jijini Dar Es Salaam, akisema mfumo huo unapatikana kwenye simu za mkononi kupitia nambari *152*00#, ukiwa na module ya sema na Kiongozi, sehemu inayomruhusu mwananchi kutoa maoni kwa Waziri, Mkuu wa Mkoa ama Kiongozi mwingine, akisema mfumo huo utakusanya maoni na kisha kuchakatwa na kufanyiwa kazi.

"Mfumo huu wa e- mrejesho ni kiunganishi cha moja kwa moja cha mwananchi na Kiongozi na hii itatusaidia pale tunapojadili namna ya kuboresha mifumo ya utumishi wa umma na ni mfumo wa kweli huu, hata kama kuna Kiongozi hatojibu sisi tutasimamia kuhakikisha majibu yanapatikana." Amesema Mhe. Ridhiwani.

Aidha Mhe. Ridhiwani amehimiza wananchi kuutumia mfumo huo katika kutoa maoni yao, akisisitiza kuwa maboresho hayo yanaenda sambamba na utengenezaji wa Aplikesheni itakayowezesha wananchi kutoa mrejesho wa haraka na wa uwazi ili kuimarisha uwajibikaji wa watumishi wa serikali.

 


✅️ _Akemea Jasi Kuuzwa na Kununuliwa Chini ya Bei Elekezi_

✅️ _Aingilia Kati Kero kwa Wachimbaji Wadogo, Wadau Kukutana Dodoma Kutafuta Suluhu ya Kudumu_

✅️ _Awahimiza Vijana Kuchangamkia Fursa Zilizopo Sekta ya Madini_ 

✅️ _Mining For A Brighter Tomorrow-MBT Kimbilio Jipya kwa Vijana na Wanawake_

Naibu Waziri wa Madini, Mhe. Dkt. Steven Kiruswa amesema kuwa Serikali kupitia Wizara ya Madini inatarajia kukutana jijini Dodoma katika siku za karibuni na wadau wa madini ya jasi (gypsum) wakiwemo wachimbaji wadogo, wasafirishaji, wamiliki wa viwanda vya saruji, Uongozi wa Wilaya na Halmashauri ya Wilaya ya Same ili kujadili na kutatua changamoto zinazoathiri shughuli za uchimbaji na biashara ya madini hayo ambazo zimechangia kusuasua kwa maendeleo ya wananchi wanaotegemea sekta hiyo.

Alitoa kauli hiyo jana, Desemba 12, 2025, wakati wa ziara yake ya kukagua shughuli za uchimbaji katika Kata za Makanye na Ruvu Jeungeni, wilayani Same, mkoani Kilimanjaro, ambako pia alizungumza na wachimbaji wadogo wa madini ya jasi.

Dkt. Kiruswa alisisitiza marufuku ya kununua madini ya jasi chini ya bei elekezi iliyotolewa na Tume ya Madini, akiwataka wote kuheshimu miongozo hiyo ili kulinda maslahi ya wachimbaji.

Kwa upande wa mazingira, alitoa wito kwa wachimbaji kuhakikisha utunzaji wa mazingira, kufukia mashimo mara baada ya shughuli za uchimbaji kukamilika, pamoja na kupongeza juhudi za uanzishwaji wa Mfuko Maalum wa kusaidia kurejesha mazingira mara baada ya kutamatika kwa shughuli za uchimbaji, ambao umeelezwa kuwa chachu ya kuimarisha uwajibikaji na uendelevu wa shughuli za madini wilayani humo.

Katika hatua nyingine, Dkt. Kiruswa aliendelea kusisitiza umuhimu wa mafunzo ya MBT kwa vijana na wanawake, utoaji wa leseni, pamoja na upatikanaji wa vifaa vya kisasa ili kuongeza ufanisi na usalama katika uchimbaji mdogo wa madini ya jasi na kuwahimiza vijana kuchangamkia fursa zilizopo katika mnyororo mzima wa Sekta ya Madini. 

Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Same, Kasilda Mgeni alieleza kuwa uchimbaji wa jasi ni uti wa mgongo wa maendeleo ya wananchi na Halmashauri ya Wilaya ya Same, na kwamba kuibuka kwa mgogoro huo baina ya wachimbaji wadogo na wamiliki wa viwanda vya saruji unakwamisga maendeleo katika wilaya hiyo na kwamba Serikali imejipanga kuhakikisha sekta hiyo inakuwa na tija kwa wadau wote.

Naye, Afisa Madini Mkazi wa Mkoa wa Kilimanjaro Mhandisi Abel Madaha alisema kuwa Tume ya Madini kwa kushirikiana na taasisi nyingine za Serikali pamoja na wadau wa madini wamekuwa wakikaa mara kwa mara kwa manufaa ya wachimbaji na watumiaji wa madini husika ikiwemo kutafuta ufumbuzi wa changamoto zinazowakumbuka wachimbaji kuanzia migodini hadi kwa watumiaji wa mwisho.











Shirika la Masoko ya Kariakoo limeanza rasmi maandalizi ya Mpango Mkakati mpya wa miaka mitano 2026-2031, hatua inayolenga kulifanya soko hilo la kimataifa kutoa huduma bora, kwa wakati na kuzingatia mabadiliko ya teknolojia yanayojitokeza duniani.

Meneja Mkuu wa Shirika la Masoko ya Kariakoo, CPA. Ashiraf Abdulkarim,akizungumza wakati wa ufunguzi wa mafunzo ya uchambuzi na uandaaji wa mpango Mkakati mpya wa miaka mitano 2026-2031 wa Shirika la Masoko ya Kariakoo.

....

Shirika la Masoko ya Kariakoo limeanza rasmi maandalizi ya Mpango Mkakati mpya wa miaka mitano 2026-2031, hatua inayolenga kulifanya soko hilo la kimataifa kutoa huduma bora, kwa wakati na kuzingatia mabadiliko ya teknolojia yanayojitokeza duniani.

Mpango huo unakuja baada ya baada ya mpango wa 2021-2025 kumaliza muda wake wa utekelezaji kwa mafanikio makubwa.

Akizungumza wakati wa ufunguzi mafunzo ya uchambuzi na uandaaji wa mpango huo, Meneja Mkuu wa Shirika la Masoko ya Kariakoo, CPA. Ashiraf Abdulkarim , amesema maandalizi ya mpango huo umeshirikisha wadau ikiwemo Ofisi Waziri Mkuu TAMISEMI, Wafanyabiashara wa Kariakoo, Wapangaji na wadau wengine ili kuwa na mpango mkakati bora, uliochukua mawazo ya wengi na unaojibu matamanio ya kila mmoja na hivyo kuwa rahisi katika utekelezaji wake.

CPA Abdulkarim ameongeza kuwa katika kuandaa mpango huo, Shirika litazingatia nyaraka mbalimbali ikiwemo Dira ya Maendeleo ya Taifa 2025-2050, hotuba ya Rais wakati akifungua Bunge la 13, Mpango wa Nne wa Maendeleo wa Taifa, Ilani ya Uchaguzi ya mwaka 2025-2030 pamoja na Sheria na miongozo mbalimbali iliyoanzisha Shirika la Kariakoo.

“Mafunzo haya yatafanyika kwa siku tano na yatakuwa endelevu. Lengo ni kuwa na mpango mkakati bora, unaotekelezeka na unaoweza kupimika kila mwaka kwa kipindi cha miaka mitano ambao utalifanya soko la kariakoo kuwa kinara na linalotoa huduma anuai na sio mazao pekee" amebainisha CPA Abdulkarim.

Amesema mpango huo ukikamilika utalibadilisha soko la Kariakoo kuwa kituo cha kisasa cha biashara, chenye mifumo ya kisasa ya uendeshaji na utoaji huduma.

CPA. Abdulkarim amesema kuwa Kariakoo mpya itakuwa na miundombinu ya kisasa kuanzia maeneo ya maegesho ya magari, mifumo ya kuzima moto, maeneo ya dharura, hewa ya kutosha na mifumo ya kiteknolojia ya uendeshaji. Tunataka kuwahudumia Watanzania katika mazingira bora na ya kisasa.

Kwa upande wake, Meneja wa Mipango na Biashara wa Shirika la Kariakoo, Bi. Mwinga Luhoyo amesema maandalizi ya mpango huo yanahusisha tathmini ya mpango uliopita wa 2021–2025 ili kubaini mafanikio, changamoto na maeneo yanayohitaji maboresho.

Meneja huyo ameongeza kuwa lengo ni kuhakikisha mpango huo unaendana na mikakati ya kitaifa na huku ukilenga kuongeza tija, kuimarisha biashara, na kukuza mchango wa Kariakoo katika uchumi wa taifa.

‎Mkuu wa wilaya ya Karatu Mhe. Dkt. Lameck  Ng'ang'a Karanga amewapongeza Kampuni ya Serengeti Breweries Limited (SBL) na shirika lisilo la serikali AFRICAI kwa kuendelea kutekeleza ujenzi wa miradi Miwili (2) ya maji mmoja ukiwa  kata Mbulumbulu na mwingine Kata ya Baray. 

‎Mhe. Dkt Lameck ametoa pongezi hizo leo Desemba 12, 2025 ofisni kwake wakati akipokea taarifa ya maendeleo ya miradi ya maji  inayotekelezwa na wadau hao katika vijiji vya Kambi ya simba, Dumbechand, Mbuga Nyekundu pamoja na Geobaj 

‎Aidha serikali imewahakikishia wadau hao  kuwapa ushirikiano  kwa kutumia Mamlaka zake ikiwemo RUWASA ili huduma ya maji iwafikie wananchi popote walipo na kwa nyakati zote. 

‎Miradi hiyo ilianza Oktoba 2025 na inatarajiwa kumalizika mwishoni kwa mwezi Januari 2026 huku zaidi ya wananchi 2, l000 wanakadiriwa kunufaika    na miradi hiyo ambayo itamaliza tatizo la maji katika vijiji hivyo.

 


Na Munir Shemweta, WANMM MOROGORO

Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Dkt Leonard Akwilapo amewaasa wahitimu wa Chuo cha Ardhi Morogoro (ARIMO) kujiepusha na matendo maovu na elimu na maarifa waliyopata yawe tunu na faida kwa Taifa.

Mhe. Dkt Akwilapo ametoa wito huo tarehe 12 Desemba 2025 wakati wa mahafali ya 44 ya Chuo cha Ardhi Morogoro (ARIMO) yaliyofanyika mkoani Morogoro ambapo jumla ya wahitimu 450 wa fani za Jiomatikia (Upimaji Ardhi), Upangaji Miji na Vijiji na Mifumo ya Taarifa za Kijiografia (GIS) walitunukiwa Astashada na Stashahada katika fani hizo.

Mhe. Dkt Akwilapo amewataka wahitimu hao kukumbuka kuwa utii, nidhamu na tabia njema ni silaha itakayowafanya wapendwe mahali popote.

‘’Tukiwa hapa Morogoro tunakumbuka maneno yaliyoimbwa na mwanamuziki wa hapa hayati Mbaraka Mwinshehe na bendi yake ya Okestra Volcano; alisema “Heshima Kijana tanguliza kwanza mbele, ujeuri mbaya; uzuri si hoja tabia njema ni silaha utapendwa popote” mwisho wa kunukuu, alisema Mhe. Dkt Akwilapo.

Amewataka vijana kutodanganyika na maneno ya eti kuna watu wanaitwa Gen Z ambapo alieleza kuwa, hizo ni propaganda za kujenga hofu na kufifisha juhudi za nchi maskini kujitafutia maendeleo.

“Msidanganywe kuwa eti nyie ni kizazi cha vijana wasio na nidhamu, wapenda fujo, wasiosikiliza wazee wao, viongozi wao, chenye kujiamulia mambo yao bila kufuata sheria, taratibu, miongozo na tamaduni zetu; na mambo mengine ya hovyo’’ amesisitiza Mhe. Dkt Akwilapo.

Kwa mujibu wa Waziri huyo wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi, inasikitisha na kushangaza kuona vijana wa Kitanzania wanasikiliza maelekezo ya watu ambao hawaishi Tanzania na wala hawajawahi kuwaona na kupuuza  maelekezo ya Viongozi wao na hata wazazi wao ambao wamewalea mpaka hapo walipoifikia.

Amesema, kuhitimu masomo kunatakiwa kuendane na uzalendo waliojengewa wa kuipenda Tanzania na kusisitiza kuwa waithamini nchi yao.

Mhe. Dkt Akwilapo amewataka kutumia utaalamu walioupata kwa weledi, uadilifu na kufuata sheria, kanuni, taratibu na miongozo na kuepuka vitendo vinavyoenda kuhatarisha amani.

Vile vile amewataka kuendelea kujifunza kwani elimu ni bahari, haina mwisho na kuwataka wanaobaki chuoni kuongeza bidii katika masomo, nidhamu na kutunza amani na umoja kwani kesho yao inajengwa na maamuzi ya leo.

Kwa upande wake Mkuu wa wilaya ya Morogoro, Bw. Musa Ramadhani Kilakala akimuwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Bw. Adam Malima amesema, migogoro ya ardhi imepungua mkoani humo hasa pale wizara ya ardhi ilipoanzisha Kliniki za Ardhi ambazo amezieleza zimesaidia kwa kiasi kikubwa kuwafikia wananchi katika maeneo yao.

Akitoa taarifa kwa Mgeni Rasmi, Mkuu wa Chuo cha Ardhi Morogoro (ARIMO) Charles Saguda amesema chuo hicho kina Mpango Kabambe wa Miaka 20 (2023-2043) unaolenga kuboresha mazingira ya kujifunza na kujifunzia na utendaji wa chuo katika kuwaandaa wataalamu wa sekta ya ardhi.

“Mpango kabambe huu unalenga kuongeza udahili wa wana chuo kutoka 660 hadi 5000, kuongeza watumishi kutoka 58 hadi 310 kuongeza program za mafunzo ya wanafunzi kutoka 2 hadi 7 pamoja na kujenga kampasi mpya katika eneo Mlima Kola mkoani Morogoro’’. Amesema Bw. Saguda

Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Judith Kapinga,akizungumza wakati akizindua Bodi mpya ya Wakurugenzi wa WRRB) hafla iliyofanyika leo Disemba 12,2025 jijini Dodoma.

.......

Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Judith Kapinga (Mb), amesema Bodi ya Usimamizi wa Mfumo wa Stakabadhi za Ghala (WRRB) imeleta mageuzi makubwa katika Biashara ya mazao nchini katika kipindi cha miaka mitano (2019–2025), hatua iliyoongeza tija kwa wakulima na mapato ya Serikali.

Mhe. Kapinga ameyasema hayo Disemba 12, 2025 jijini Dodoma wakati akizindua Bodi mpya ya Wakurugenzi wa WRRB alipobainisha kuwa mageuzi hayo yameongeza ufanisi, uwazi na matumizi ya TEHAMA katika minyororo ya biashara ya mazao nchini.

Aidha, kiasi cha mazao yanayopitia mfumo huo kimeongezeka kwa zaidi ya asilimia 120, kutoka chini ya tani 600,000 hadi zaidi ya tani 1.3 milioni kwa mwaka, huku bei za mazao zikiongezeka kwa wastani wa asilimia 15 hadi 35, na hivyo kuongeza kipato cha maelfu ya wakulima.

Pia amesema kuwa idadi ya maghala yaliyosajiliwa imeongezeka kutoka chini ya 300 hadi zaidi ya 500, huku mapato ya Serikali yakipanda kwa zaidi ya asilimia 140 kutokana na ushuru, kodi na tozo mbalimbali.

Waziri Kapinga ameielekeza Bodi mpya kuhakikisha mafanikio yaliyopatikana yanaimarishwa na kupanuliwa zaidi katika kipindi kijacho cha miaka mitano huku akiitaka bodi hiyo Mpya kuongeza ufanisi, uwajibikaji na ushindani katika biashara ya mazao nchini.

Kwa upande wake Katibu Mkuu Wizara ya Viwanda na Biashara, Dkt. Hashil Abdallah, amesema kuwa wizara hiyo itaendelea kushirikiana kwa karibu na Wizara ya Kilimo ili kuboresha huduma za masoko na kuongeza tija kwa wakulima nchini pamoja na kuimarisha uwezo wa wakulima, kukuza ajira na kuunganisha kilimo na viwanda ili kuchochea maendeleo endelevu ya taifa.

Awali, Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Usimamizi wa Mfumo wa Stakabadhi za Ghala (WRRB), Asangye Bangu, amebainisha kuwa matumizi ya stakabadhi yameendelea kuongezeka mwaka hadi mwaka, ambapo idadi ya stakabadhi imepanda kutoka 33,100 hadi 53,107 kwa mwaka 2024/2025, hatua inayoonyesha kuongezeka kwa uelewa na mwitikio wa wakulima na wafanyabiashara.

Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Judith Kapinga,akisalimiana na Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Usimamizi wa Mfumo wa Stakabadhi za Ghala (WRRB), Asangye Bangu,wakati alipowasili kwa ajili ya kuzindua Bodi mpya ya Wakurugenzi wa WRRB) hafla iliyofanyika leo Disemba 12,2025 jijini Dodoma.

Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Judith Kapinga,akizungumza wakati akizindua Bodi mpya ya Wakurugenzi wa WRRB) hafla iliyofanyika leo Disemba 12,2025 jijini Dodoma.

Naibu Waziri Wa Kilimo Mh.David Silinde ,akizungumza wakati wa uzinduzi wa  Bodi mpya ya Wakurugenzi wa WRRB) hafla iliyofanyika leo Disemba 12,2025 jijini Dodoma.

Katibu Mkuu Wizara ya Viwanda na Biashara, Dkt. Hashil Abdallah,akizungumza wakati wa uzinduzi wa  Bodi mpya ya Wakurugenzi wa WRRB) hafla iliyofanyika leo Disemba 12,2025 jijini Dodoma.

Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Judith Kapinga,akiteta jambo na Katibu Mkuu Wizara ya Viwanda na Biashara, Dkt. Hashil Abdallah, wakati wa uzinduzi wa uzinduzi wa Bodi mpya ya Wakurugenzi wa WRRB) hafla iliyofanyika leo Disemba 12,2025 jijini Dodoma.

Sehemu ya washiriki wakisikiliza hotuba ya Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Judith Kapinga (hayupo pichani)  wakati akizindua Bodi mpya ya Wakurugenzi wa WRRB) hafla iliyofanyika leo Disemba 12,2025 jijini Dodoma.

Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Judith Kapinga,akiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kuzindua  Bodi mpya ya Wakurugenzi wa WRRB) hafla iliyofanyika leo Disemba 12,2025 jijini Dodoma.

Waziri wa Madini Mhe. Anthony Mavunde amemtaka mkandarasi wa ujenzi wa kituo cha Jemolojia Tanzania (TGC) kukamilisha ujenzi wa majengo ya kituo cha mafunzo ya  Uongezaji thamani madini ya vito kwa kuongeza nguvukazi na kufanya kazi kwa masaa 24 ili kukamilisha ujenzi wa jengo kwa muda mfupi.

Waziri Mavunde ameyasema hayo leo Desemba 12, 2025 mkoani Arusha  wakati wa ziara yake ya  kukagua mradi wa kituo hicho  ulioanza ujenzi rasmi ambapo katika maelekezo yake amemtaka mkandarasi kuzingatia ujenzi bora wenye kukidhi vigezo vilivyoainishwa kwenye mkataba.

Waziri Mavunde amefafanua kuwa, Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais.Dkt. Samia Suluhu Hassan  inatekeleza mikakati yake kwenye mnyororo mzima wa uongezaji thamani madini ya vito kama Sera ya Madini ya Mwaka 2009 inavyoelekeza.

Sambamba na hapo, Waziri Mavunde amesisitiza kuwa,  kuanza kwa ujenzi huu ni sehemu ya utekelezaji wa maagizo aliyoyatoa Mhe. Rais. Dkt. Samia Suluhu Hassan wakati akihutubia Bunge la 13 jijini Dodoma.

Waziri Mavunde amebainisha kuwa,  kukamilika kwa  kituo hicho , kutaleta faida mbalimbali ikiwa pamoja na kuongezeka kwa idadi ya wanafunzi watakao jiunga kwenye kituo, kuongezeka kwa wataalamu wa uongezaji thamani madini ya vito, kufungua fursa za ajira kwa vijana na wafanyabiashara wa madini , pamoja na kutosafirishwa kwa madini ghafi nje ya nchi hivyo kutachagiza  ongezeko la  mapato kwa taifa.

Pamoja na mambo mengine, Waziri Mavunde ametoa siku 7 kwa Katibu Mkuu Wizara ya Madini kukutana na wakandarasi ,TGC na Taasisi za serikali kwa ajili ya upatikanaji vibali muhimu vya kuendeleza ujenzi.

Kwa upande wake , Mkuu wa Wilaya Arusha Mhe. Joseph Mkude ameahidi kuendelea kufuatilia maendeleo ya ujenzi ili kuhakikisha ujenzi unakamilika kama Serikali inavyotaka.

Mkude ameongeza kuwa, kukamilka kwa kituo hicho itakuwa moja ya sehemu ya uwekezaji mkubwa wa serikali  husasan kwenye Sekta ya Madini mkoani Arusha.

Awali, akitoa taarifa ya maendeleo ya ujenzi, Mkuu wa kituo cha TGC Mhandisi. Ally Maganga ameeleza kuwa, ujenzi wa majengo pacha hayo ya ghorofa 8 utagharimu Tsh Bilioni 33 na kukamilika kwake kutaongeza fursa ya vijana wengi kupata ajira kupitia ujuzi wa uongezaji thamani madini ya vito.

Naye, Meneja Mradi Mhandisi Robert Lubuva ameahidi kuhakikisha kama wakandarasi wataongeza nguvu ya rasilimali watu na vifaa ili mradi uweze kukamilika na kuwahudumia watanzania kwa wakati.







๐Ÿ“Œ Utaimarisha upatikanaji wa umeme Mbagala na Gongo la Mboto

๐Ÿ“Œ Majaribio yameanza ; Shukurani kwa Rais Samia kwa uwekezaji mkubwa


Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba, amesema kuwa mradi wa upanuzi wa Kituo cha Kupokea na Kupoza Umeme cha Kinyerezi 1 Extension umekamilika rasmi, ikiwa ni pamoja na kufungwa kwa Transfoma yenye uwezo wa MVA 175.

Amesema hatua hii ni muhimu kwa kuboresha upatikanaji wa umeme wa uhakika kwa Jiji la Dar es Salaam, hususan maeneo ya Mbagala na Gongo la Mboto, ambayo yamekuwa yakikumbwa na changamoto za kukatika kwa umeme kutokana na ongezeko la watu na shughuli za kiuchumi.

Mhe. Salome amesema hayo Desemba 11, 2025, wakati wa ziara yake katika vituo vya uzalishaji umeme vya Kinyerezi I, Kinyerezi II, Ubungo I, Ubungo II na Ubungo III akiongeza kuwa mradi tayari umeanza majaribio (testing).

“Tunamshukuru sana Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa uwekezaji mkubwa. Transfoma zimefungwa, majaribio yanaendelea, na wananchi wa Gongo la Mboto na Mbagala sasa watapata umeme wa uhakika,” Mhe. Salome.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO, Bw. Lazaro Twange, amesema Shirika linaendelea kuboresha miundombinu yake ili kukidhi mahitaji yanayoongezeka.

Amebainisha kuwa katika eneo la Kinyerezi kumefungwa Transfoma kubwa ya MVA 175, huku maeneo ya Gongo la Mboto na Mbagala yakiwekewa Transfoma ya MVA 120 ili kukidhi ongezeko la mahitaji ya umeme.

Amesisitiza kuwa idadi ya watu imekuwa ikiongezeka Jiji la  Dar es Salaam, hivyo miundombinu ya umeme lazima iboreshwe mara kwa mara ili kuendana na uhitaji uliopo. 

"Lengo la Kinyerezi 1 Extension lilikuwa kuongeza uwezo wa kusambaza umeme unaozalishwa kuwafikia wateja wetu kwa kiwango kinachostahili," amesema Bw. Twange.