Mbunge wa Jimbo la Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo, akizungumza na Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Kisarawe alipokutana nao kwa ajili ya kuzungumzia maendeleo ya kisarawe pamoja na kuwashukuru kwa kuchaguliwa katika uchaguzi uliomalizika.

Na Alex Sonna, Kisarawe

Mbunge wa Jimbo la Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo, amewaambia Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Kisarawe kuwa kipindi cha miaka mitano ijayo kitakuwa cha mchakamchaka wa maendeleo, akisisitiza kuwa wana jukumu kubwa la kuwatumikia wananchi kwa ufanisi na mshikamano.

Akizungumza katika kikao cha kuwashukuru na kuomba ushirikiano wa madiwani hao, Dkt. Jafo amesema amejipanga kuhakikisha anatafuta rasilimali fedha zitakazosaidia utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo katika kata zote za wilaya hiyo.

Amesema matarajio ya wananchi ni makubwa, hivyo madiwani wanapaswa kutambua uzito wa dhamana waliyopewa na wananchi.

“Chaguzi zote zimekwisha. Tulianza na kura za maoni, tukapita kwenye uchaguzi mkuu na uchaguzi wa Mwenyekiti wa Halmashauri. Kila uchaguzi huwa na makundi, lakini sasa ni wakati wa kuungana na kushirikiana kwa ajenda moja ya maendeleo,” amesema Dkt. Jafo.

Mbunge huyo ameahidi kutoa ushirikiano wa kutosha kwa Baraza la Madiwani ili liweze kutekeleza majukumu yake kwa ufanisi, akibainisha kuwa tayari ameshawasilisha maombi mbalimbali serikalini yanayohusu ujenzi wa shule mpya na kuboresha miundombinu ya shule zilizopo.

“Nitahangaika kwa kila hali kuhakikisha tunasonga mbele kama halmashauri. Maombi ya ujenzi wa shule mpya na miundombinu ya elimu yameshapokelewa na serikali,” amesema.

Ameongeza kuwa katika kipindi cha sasa atakuwa karibu zaidi na wananchi kwa kufanya ziara nyingi vijijini, kutoa taarifa na kusikiliza changamoto zao, huku akisisitiza umuhimu wa mshikamano.

“Tusikubali kugawanywa, kwa sababu tukiruhusu hilo tutaleta udhaifu. Tufanye kazi kama timu, tushirikiane na tupendane, wote tuwe kitu kimoja,” amesema.

Kwa upande wa sekta ya afya, Dkt. Jafo amesema amejipanga kuweka historia mpya kwa kuhakikisha kila kijiji katika Wilaya ya Kisarawe kinakuwa na zahanati, ili kuboresha upatikanaji wa huduma za afya kwa wananchi.

Aidha, amewataka madiwani kusimamia kwa karibu matumizi ya mapato ya ndani ili yatumike kwa usahihi na kuleta matokeo yanayo onekana.

“Haiwezekani mwaka ukapita bila kuwa na kitu kinacho onekana kimefanyika. Lazima fedha tunazo kusanya ziwe na matunda kwa wananchi,” amesema.

“Nikuhakikishie Mwenyekiti, miradi ya maendeleo tutahangaika nayo kwa ujumla wake. Tunaahidi mengi vijijini, hivyo ushirikiano na kupendana ni jambo la msingi ili tufanikiwe,” amesema.

Amewahimiza madiwani hao kwenda kuwashukuru wananchi waliowaamini na kuwachagua, akisisitiza kuwa mafanikio ya safari ya miaka mitano ijayo yatategemea namna watakavyoanza na kuendeleza kazi ya kuwatumikia wananchi kwa bidii na uadilifu.

   

Mbunge wa Jimbo la Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo,akizungumza na watumishi  wa Halmashauri ya Wilaya ya Kisarawe wakati wa ziara yake ya kuwashukuru kwa kazi wanayoifanya katika wilaya hiyo.

Na.Alex Sonna-KISARAWE

Mbunge wa Jimbo la Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo, amewahimiza watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kisarawe kufanya kazi kwa weledi, bidii na kwa kushirikiana kwa karibu na Baraza la Madiwani ili kuchochea maendeleo ya wilaya hiyo na kuboresha utoaji wa huduma za msingi kwa wananchi.

Rai hiyo ameitoa alipokuwa akizungumza na watumishi wa halmashauri hiyo, ambapo amesema lengo la kikao hicho lilikuwa ni kuwashukuru kwa kazi wanazozifanya na kuwaomba waendelee kutoa ushirikiano katika kuwatumikia wananchi wa Kisarawe.

“Ni muhimu kupendana na kushirikiana kama watumishi wa Serikali. Fanyeni kazi bila kuchoka, kwa kuwa mnalipwa mshahara wakati wapo wananchi wengi bado hawana ajira. Fanyeni kazi kama ibada; mkifanya hivyo kwa moyo wote mtapata mafanikio makubwa,” amesema Dkt. Jafo.

Ameongeza kuwa watumishi wanapaswa kujiepusha na utendaji wa mazoea na badala yake wafanye kazi kwa ubunifu na uwajibikaji, huku wakiacha alama chanya katika maeneo wanayoyahudumia.

Aidha, amesisitiza umuhimu wa kutafuta rasilimali fedha na kuhakikisha matumizi sahihi ya fedha za miradi ili miradi hiyo iwe na tija na kuleta manufaa kwa wananchi.

Kwa upande wake, Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kisarawe, Nyahori Mahumbwe, ameahidi kumpa ushirikiano Mbunge huyo katika kuwatumikia wananchi na kutekeleza ahadi zilizotolewa wakati wa kampeni za uchaguzi.

“Tupo tayari kufanya kazi mchana na usiku kuwatumikia wananchi na kutekeleza ahadi mlizozitoa wakati wa uchaguzi. Watekelezaji wa mkataba ule ni sisi watumishi wa Serikali, hivyo tutahakikisha tunashirikiana kikamilifu kutekeleza Ilani ya Uchaguzi,” amesema Mahumbwe.

Naye, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Kisarawe, Aidan Kitare, amesema madiwani wapo tayari kufanya kazi kwa weledi na mshikamano katika kipindi cha miaka mitano ijayo.

Mbunge wa Jimbo la Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo,akizungumza na watumishi  wa Halmashauri ya Wilaya ya Kisarawe wakati wa ziara yake ya kuwashukuru kwa kazi wanayoifanya katika wilaya hiyo.

Mbunge wa Jimbo la Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo,akizungumza na watumishi  wa Halmashauri ya Wilaya ya Kisarawe wakati wa ziara yake ya kuwashukuru kwa kazi wanayoifanya katika wilaya hiyo.

Mbunge wa Jimbo la Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo,akizungumza na watumishi  wa Halmashauri ya Wilaya ya Kisarawe wakati wa ziara yake ya kuwashukuru kwa kazi wanayoifanya katika wilaya hiyo.

Mbunge wa Jimbo la Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo,akizungumza na watumishi  wa Halmashauri ya Wilaya ya Kisarawe wakati wa ziara yake ya kuwashukuru kwa kazi wanayoifanya katika wilaya hiyo.

Mbunge wa Jimbo la Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo,akizungumza na watumishi  wa Halmashauri ya Wilaya ya Kisarawe wakati wa ziara yake ya kuwashukuru kwa kazi wanayoifanya katika wilaya hiyo.

Sehemu ya watumishi wakimsikiliza Mbunge wa Jimbo la Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo,wakati akizungumza na watumishi  wa Halmashauri ya Wilaya ya Kisarawe wakati wa ziara yake ya kuwashukuru kwa kazi wanayoifanya katika wilaya hiyo.

Mbunge wa Jimbo la Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo akimsikiliza Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kisarawe, Nyahori Mahumbwe,wakati ,akizungumza na watumishi  wa Halmashauri hiyo  wakati wa ziara yake ya kuwashukuru kwa kazi wanayoifanya katika wilaya hiyo.

Mbunge wa Jimbo la Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo akimsikiliza KMwenyekiti wa Halmashauri ya Kisarawe, Aidan Kitare,wakati ,akizungumza na watumishi  wa Halmashauri hiyo  wakati wa ziara yake ya kuwashukuru kwa kazi wanayoifanya katika wilaya hiyo.

Mbunge wa Jimbo la Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo akimsikiliza Afisa Utumishi wa halmashauri ya wilaya ya Kisarawe Bi.Sabra Mwankenja,wakati ,akizungumza na watumishi  wa Halmashauri hiyo  wakati wa ziara yake ya kuwashukuru kwa kazi wanayoifanya katika wilaya hiyo.

Sehemu ya watumishi wakimsikiliza Mbunge wa Jimbo la Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo (hayupo pichani) ,wakati akizungumza na watumishi  wa Halmashauri ya Wilaya ya Kisarawe wakati wa ziara yake ya kuwashukuru kwa kazi wanayoifanya katika wilaya hiyo.

Mbunge wa Jimbo la Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo ,akiwa katika picha ya pamoja ,mara baada ya kuzungumza na watumishi  wa Halmashauri hiyo  wakati wa ziara yake ya kuwashukuru kwa kazi wanayoifanya katika wilaya hiyo.

Mbunge wa Jimbo la Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo,akizungumza katika kikao cha Kamati ya Siasa ya Wilaya ya Kisarawe kwa ajili ya kuwashukuru wajumbe mara baada ya kumalizika kwa uchaguzi Mkuu  kilichofanyika leo Disemba 12,2025 wilayani Kisarawe Mkoani Pwani.

Na.Alex Sonna-KISARAWE

Mbunge wa Jimbo la Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo, ameanza utekelezaji wa ahadi alizozitoa wakati wa uchaguzi mkuu 2025 kupitia Ilani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), huku akitaja barabara, maji, afya na elimu kuwa miongoni mwa vipaumbele vyake vikuu katika kipindi cha miaka mitano ijayo.

Akizungumza katika kikao cha Kamati ya Siasa ya Wilaya ya Kisarawe, Dkt. Jafo amesema tayari amewasiliana na Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) kuhusu barabara ya Kisarawe, hatua inayolenga kuhakikisha mkandarasi anaanza utekelezaji wa mradi huo kwa wakati.

Katika sekta ya maji, amesema amefanya kikao na ujumbe kutoka Korea kuhusu utekelezaji wa mradi wa maji utakaohusisha ujenzi wa vituo 105 vya kuchotea maji katika vijiji 17. Ameongeza kuwa ameomba kuzingatiwa kwa uwekaji wa matenki makubwa na kuangalia uwezekano wa kuvifikia vijiji vya Gwata na Dololo.

“Eneo hili linahitaji matenki makubwa kutokana na kuongezeka kwa idadi ya watu kufuatia uwepo wa Bandari ya Kwara. Mradi huu ni mkubwa, una thamani ya takribani sh. bilioni 27, si jambo dogo,” amesema Dkt. Jafo.

Kwa upande wa elimu, amesema ataendelea kutafuta pesa Serikali kuu pamoja na wadau wengine wa elimu ili kuboresha miundombinu pamoja na  ujenzi wa shule za sekondari pamoja na kuipandisha hadhi Shule ya Sekondari Jafo kuwa na kidato cha tano na sita na kuitenga kwa wavulana.

“Pia nimeomba kuongezwa kwa bweni Shule ya Sekondari Kisarawe, ujenzi wa sekondari mpya Mafizi, Maluwi, Kwala, Sungwi, Mwanzo Mgumu, Kiluvya B, Sanze na Bwama,” amesema.

Ameongeza kuwa amewasilisha pia maombi ya ujenzi wa shule mpya katika maeneo ya Kibesa, Mjimpya, Darfur na Vihingo, pamoja na kuongeza madarasa katika shule za Malumbo, Mfulu na Kibwemwenda. 

Dkt. Jafo amesema pia anaendelea kuifuatilia TARURA ili kuhakikisha barabara zinakuwa katika hali nzuri, na baadhi ya barabara korofi kujengwa kwa zege ili ziweze kupitika wakati wote wa mvua.

“Naiomba CCM tushirikiane ili katika miaka hii mitano tuweze kutimiza matarajio ya wananchi. Nitaanza ziara za kushukuru awamu kwa awamu na kuwashukuru wajumbe wa mkutano mkuu,” amesema.

Awali, amempongeza Aidan Kitare kwa kuchaguliwa kuwa Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Kisarawe na kuahidi kuwa Ofisi ya Mbunge itatoa ushirikiano wa kutosha katika utekelezaji wa majukumu ya chama

Pia amewashukuru wana-CCM kwa kumuamini na kumpa nafasi ya kuendelea kuongoza kwa kipindi kingine cha miaka mitano, akieleza kuwa wilaya hiyo imeendelea kuwa tulivu kisiasa.

Aidha, amemshukuru Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuridhia kutolewa kwa fedha za serikali zilizochochea maendeleo ya Wilaya ya Kisarawe.

“Tumsaidie Rais wetu kwa kutimiza wajibu wetu. Kwa upande wangu, nitaongoza kuhakikisha malengo ya Rais kwa Kisarawe yanatimia,” amesema.

Kwa upande wake Mwewnyekiti wa Chama cha Mapinduzi Wilaya ya Kisarawe ndg.Khalfan Sika,amempongeza Mhe.Jafo kwa kazi kubwa aliyoifanya katika Jimbo la Kisarawe kwa kuleta maendeleo hivyo watampa ushirikiano wa kutosha ili aendelee kumsaidia Mhe.Rais Samia kutekeleza miradi ya wanakisarawe.

Mbunge wa Jimbo la Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo,akizungumza katika kikao cha Kamati ya Siasa ya Wilaya ya Kisarawe kwa ajili ya kuwashukuru wajumbe mara baada ya kumalizika kwa uchaguzi Mkuu  kilichofanyika leo Disemba 12,2025 wilayani Kisarawe Mkoani Pwani.

Mbunge wa Jimbo la Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo,akizungumza katika kikao cha Kamati ya Siasa ya Wilaya ya Kisarawe kwa ajili ya kuwashukuru wajumbe mara baada ya kumalizika kwa uchaguzi Mkuu  kilichofanyika leo Disemba 12,2025 wilayani Kisarawe Mkoani Pwani.

Mbunge wa Jimbo la Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo,akizungumza katika kikao cha Kamati ya Siasa ya Wilaya ya Kisarawe kwa ajili ya kuwashukuru wajumbe mara baada ya kumalizika kwa uchaguzi Mkuu  kilichofanyika leo Disemba 12,2025 wilayani Kisarawe Mkoani Pwani.

Mbunge wa Jimbo la Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo,akimsikiliza Mwewnyekiti wa Chama cha Mapinduzi Wilaya ya Kisarawe ndg.Khalfan Sika,wakati wa kikao cha Kamati ya Siasa ya Wilaya ya Kisarawe kwa ajili ya kuwashukuru wajumbe hao kilichofanyika leo Disemba 12,2025 wilayani Kisarawe Mkoani Pwani.

 

Mbunge wa Jimbo la Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo,akimsikiliza Katibu  wa Chama cha Mapinduzi Wilaya ya Kisarawe Bi.Josephine Mwanga ,wakati wa kikao cha Kamati ya Siasa ya Wilaya ya Kisarawe kwa ajili ya kuwashukuru wajumbe hao kilichofanyika leo Disemba 12,2025 wilayani Kisarawe Mkoani Pwani.

Mbunge wa Jimbo la Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo,akimsikiliza Mwenyekiti wa Halmashauri ya Kisarawe, Aidan Kitare,katika kikao cha Kamati ya Siasa ya Wilaya ya Kisarawe wakati wa ziara ya kutoa shukrani kwa  wajumbe hao kilichofanyika leo Disemba 12,2025 wilayani Kisarawe Mkoani Pwani.

 

 

Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Mhe. Wanu Hafidh Ameir, amemtaka Mkandarasi wa COMFIX & ENGINEERING kuongeza kasi ya ujenzi wa miundombinu ya Mradi wa Kujenga Ujuzi na Ushirikiano Afika Mashariki (EASTRIP ) katika Taasisi ya Teknolojia Dar es Salaam (DIT) Kampasi ya Mwanza, ili ikamilike kwa wakati kulingana na maktaba.

Naibu Waziri huyo, ametoa maagizo hayo jijini Mwanza wakati akikagua maendeleo ya utekelezaji wa mradi huo. Pia amewataka wazabuni wote kuhakikisha vifaa na mitambo vinawasili na kufungwa kwa wakati ili kuwezesha utoaji wa mafunzo kwa wakati.

Mhe. Wanu Ameir amesema ucheleweshaji wa ujenzi unaweza kuathiri malengo ya Serikali ya kuhakikisha vijana wanapata ujuzi na umahiri unaohitajika katika soko la ajira la ndani na kimataifa, kama alivyoelekeza Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Mhe. Ameir amewahakikishia wananchi na uongozi wa DIT kuwa Serikali itaendelea kuimarisha uwezo wa kampasi hiyo, ikiwemo kuongeza udahili wa wanafunzi kutoka 358 wa sasa hadi 2,000

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Daniel Mushi, amesema kuwa katika Kampasi ya DIT Mwanza kinajengwa Kituo cha Kikanda cha Umahiri cha uchakataji na utengenezaji wa bidhaa za Ngozi ambacho kinatekelezwa kupitia Mradi wa EASTRIP. Amesema kuwa ujenzi huo unahusisha majengo matano ambayo ni jengo la kufundishia, jengo la taaluma, hosteli mbili na karakana ya kisasa kwa ajili ya mafunzo ya utengenezaji wa bidhaa za ngozi.

Prof. Mushi ameongeza kuwa ujenzi wa majengo hayo unatekelezwa na Serikali kwa kushirikiana na Benki ya Dunia ambayo imetoa mkopo wa riba nafuu kufanikisha mradi huo. Ambapo gharama za utekelezaji wa mradi DIT Mwanza ni shilingi bilioni 37.

Mkurugenzi wa Taasisi ya Teknolojia ya Dar Es Salaam (DIT) Kampasi ya MWANZA Dkt. John Msumba amesema kuwa Kampasi hiyo imefufua Sekta ambayo ilikuwa imekufa nchini kutokana na kukosekana Kwa wataalamu na kwamba Viwanda Kwa sasa vinapata wataalamu tofauti na awali ambapo walikuwa wakilazimika kuwatoa nje ya nchi.