Na Oscar Assenga, TANGA

MAMLAKA ya Usimamizi wa Bandari nchini (TPA) umesema kwamba maboresho makubwa yaliyofanywa katika Bandari ya Tanga umepelekea wastani wa kuhudumia meli moja kwa siku tatu kutoka siku saba za awali kutokana na kuongezeka kwa ufanisi mkubwa.

Hayo yalisemwa na Mwakilishi wa Meneja wa Bandari ya Tanga Peter Milanzi wakati wa upokeaji aina mpya ya mzigo wa Lami kupitia Kampuni ya Wakala wa Usafirishaji ya Amura unaosafirishwa kwenda nchi jirani ya Malawi ambao wameamua kutumia Bandari hiyo kutokana na ufanisi wake

Alisema kwamba kutokana na ufanisi huo umepelekea kuvutia wateja wengi kuitumia Bandari hiyo kupitisha shehena mbalimbali za mizigo ikiwemo magari na mizigo mbalimbali ambazo zinakwenda nchi mbalimbali.

“Bandari ya Tanga tumeendelea kufanya vizuri kutokana na maboresho yaliyofanywa na Serikali kupitia Rais Dkt Samia Suluhu na hivyo kuvutia wateja wengi na leo tunapokea aina mpya ya mzigo wa Lami kwa wenzao wa Kampuni ya Amoue wameamua kuitumia Bandari ya Tanga kutokana na ufanisi ambao wanao kwa majaribio wameamua kupitisha makontena sita na kila moja lina mapipa 110 inaenda nchi ya Malawi”Alisema

Alisema kwamba hiyo ni ishara kubwa ya kuaminiwa na wafanyabiashara na watu mbalimbali hivyo wanawaambia wateja waendele kuitumia Bandari hiyo kutokana na wao wanaendelea kuwahudumia kwa ufanisi na kutoa huduma bora kama wenzao Amoura.

“Bandari ya Tanga ni salama na itaendelea kuwa samana na kutoa huduma ya ushushaji wa mizigo na kwa wale waliokwama kwenye Bandari nyengine njooni Tanga mtahudumiwa kwa ufanisi mkubwa na kwa muda mfupi”Alisema Milanzi.

Hata hivyo alisema kwamba kuanzia mwezi Julai mwaka huu wa Fedha 2025/2026 walipangiwa kuhudumia Tani milioni 1.6 ,sasa wastani wa kuhudumia tani laki 137,000 lakini tokea mwezi Julai mwaka huu wamekuwa wakivuka malengo walianza na tani laki 152,000 na baadae wakapanda tani 157,000 na mwezi Septemba –Octoba wamefikisha tani 200,000 kila mwezi.

Alieleza kwamba wanaona malengo ambao wamewekewa watayafikia hayo yote yamekua kutokana na ufanisi wao kwenye kazi na hivyo wateja wameongezeka hatua inayoonyesha watavuta malengo waliopangiwa kutokana na m.

Awali akizungumza mara baada ya mara baada ya kushushwa kwa Shehena hiyo ya Lami –Mwakilishi wa Kampuni ya  Amura ya Dar ,Zakaria Mohamed Nanimuka alisema kwamba kutokana na ufanisi wa Bandari ya Tanga wanategemea kuingiza kontena nyengine 20 zitazohudumiwa kwenye Bandari hiyo.

“Sisi kama Kampuni Amura tumefurahishwa na ufanisi wa Bandari ya Tanga na hakuna malalamiko wala changamoto zozote zile tunashukuru Serikali kwa kuwekeza hapa na sasa sisi wasafirishaji tutaendelea kuitumia katika kuingiza shehena mbalimbali”Alisema

Zakari alisema kwamba wamekuja Tanga kupokea shehena ya mzigo wa Lami kutoka Iran na kushukia Bandari ya Tanga kontena sita zenye tani 125 na kilo 430 ambapo kontena moja lina kuwa na pipa 110 kwa kontena

Alisema kwamba wanashukuru kwa namna walivyohudumiwa wamefanya kazi vizuri na wala hakukuwa na changamoto za aina yoyote ile mzigo wao umeweza kushughulikiwa wamepita scana kwa wakati hivyo wanamshukuru Rais Dkt Samia Suluhu kwa maboresho makubwa yaliyosaidia kuongeza ufanisi.





Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, leo amefanya mazungumzo na Kaimu Balozi wa Marekani nchini Tanzania, Andrew Lentz, katika Ikulu ya Chamwino, kujadili maeneo muhimu ya ushirikiano na kuimarisha dhamira ya pamoja ya kujenga ushirikiano wa kisasa na wenye manufaa kwa pande zote mbili.


Balozi Lentz—aliyefuatana na Mshauri wa Masuala ya Kisiasa na Uchumi—amesisitiza dhamira ya Washington kuhuisha mahusiano na kuongeza kina la ushirikiano wa kiuchumi, kisiasa na kiusalama kati ya mataifa haya mawili.


“Marekani imejitolea kujenga ushirikiano usiotegemea misaada, bali unaojengwa juu ya ustawi wa pamoja,” alisema Balozi Lentz.

Mazungumzo yamejikita katika hatua za majadiliano ya miradi mikubwa inayoongozwa na kampuni za Marekani. Pande zote mbili zimekubaliana kuwa majadiliano ya miradi miwili ya kimkakati—Mradi wa LNG na Mradi wa Tembo Nickel—yamefikia hatua za mwisho kabla ya kutiwa saini rasmi. Uwekezaji wa tatu, Mradi wa Mahenge Graphite, unaendelea kufanyiwa uchambuzi wa kiufundi.


Rais Samia ameukaribisha upya msimamo wa Marekani na kuhakikishia ujumbe huo kuwa Tanzania itaendelea kusimamia hatua zote zilizobaki ili kukamilisha taratibu na kufungua njia ya utekelezaji wa miradi hiyo.

“Kama taifa lisilofungamana na upande wowote, Tanzania iko wazi, tayari na imejitoa kufanya kazi na washirika wote wanaoheshimu uhuru wetu na kushiriki katika dira yetu ya maendeleo,” alisema Rais.

“Miradi hii ni ya umuhimu mkubwa kwa taifa, na tumejidhatiti kuikamilisha ili iweze kufungua ajira, uwekezaji, na ustawi endelevu kwa wananchi wetu.”

Rais pia alibainisha kuwa zaidi ya kampuni 400 za Marekani kwa sasa zinafanya shughuli zao nchini Tanzania—kiashiria cha uthabiti wa nchi, mazingira mazuri ya uwekezaji na historia ya muda mrefu ya ushirikiano wa kiuchumi kati ya mataifa haya mawili.

Mbali na uwekezaji, mazungumzo yamegusa maeneo mapana ya ushirikiano ikiwemo utulivu wa kisiasa, usalama wa kikanda, mageuzi ya kiuchumi, ukuaji wa sekta binafsi, ushirikiano katika afya na programu za kubadilishana uzoefu kati ya wananchi wa nchi hizi mbili.




Balozi Lentz amempongeza Rais Samia kwa maono na mipango madhubuti ya muda mrefu kupitia Vision 2050, na kusisitiza kuwa Serikali ya Marekani iko tayari kuunga mkono utekelezaji wake pamoja na kuimarisha falsafa ya 4R ya Rais—maridhiano, ustahimilivu, mageuzi na kujenga upya imani katika utawala.

Pande zote zimekubaliana kuwa mawasiliano ya karibu, ushirikiano wa mara kwa mara, na hatua za haraka katika kukamilisha makubaliano yaliyosalia ni muhimu katika kufungua uwezo kamili wa uhusiano kati ya Tanzania na Marekani.

Kikao hiki kinawakilisha hatua muhimu katika kufafanua upya na kuhuisha mahusiano kati ya Tanzania na Marekani. Dhamira ya pamoja iliyothibitishwa na serikali zote mbili inaashiria mwanzo wa ushirikiano wa kisasa, wazi, unaoongozwa na sekta binafsi—ukijengwa juu ya ustawi wa pamoja, kuheshimiana na ushirikiano wa muda mrefu wa kimkakati.

Miradi Mikuu ya Kimkakati




1. Mradi wa LNG — Thamani Inayokadiriwa: Dola Bilioni 42




Mradi mkubwa wa kugundua na kuchakata gesi asilia unaohusisha kampuni kubwa za kimataifa za nishati. Mradi huu unalenga kufungua hazina kubwa ya gesi iliyopo baharini, kuongeza mapato ya taifa, kuunda maelfu ya ajira na kuiweka Tanzania katika ramani ya dunia kama mchezaji muhimu wa LNG.




2. Mradi wa Tembo Nickel — Thamani: Dola Milioni 942




Uwekezaji mkubwa wa madini muhimu eneo la Ngara unaolenga nikeli—kiungo muhimu katika utengenezaji wa betri za magari yanayotumia umeme. Mradi huu utaimarisha minyororo ya kimataifa ya nishati safi, kuchochea viwanda na kuongeza pato la mauzo ya nje.




3. Mradi wa Mahenge Graphite — Thamani: Dola Milioni 300




Chanzo kikubwa duniani cha madini ya graphite yenye ubora wa juu, yenye umuhimu katika uzalishaji wa betri na teknolojia za nishati jadidifu. Mradi huu utaimarisha nafasi ya Tanzania kama mtoa huduma mkuu wa malighafi muhimu za viwanda vya kisasa vya betri.
The Open University of Tanzania (OUT), through its UNESCO Chair on Teacher Education and Curriculum, has completed a dissemination and certificate award workshop for 24 STEM teachers from Iringa District Council who were trained under the CL4STEM digital skills programme.

 


Naibu Waziri wa Nishati Mhe. Salome Makamba amefanya ziara katika  Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) pamoja na Mamlaka ya Udhibiti wa Mkondo wa Juu wa Petroli (PURA) kwa lengo la kuzungumza na Watendaji taasisi hizo mara baada ya kuteuliwa na Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan kushika nyadhifa hiyo  ambapo amewataka watendaji kuhakikisha  Watanzania wananufaika moja kwa moja na uwepo wa rasilimali za mafuta na gesi.

Katika mazungumzo hayo yaliyofanyika jijini Dar es Salaam, Mhe. Salome ameweka mkazo kuhusu upatikanaji wa ajira kwa Watanzania, huduma za kijamii na upatikanaji wa nishati kwa gharama nafuu. 

Mhe. Salome pia ameielekeza Menejimenti ya TPDC kuongeza kasi ya usambazaji wa gesi asilia majumbani ili Watanzania waendelee kunufaika zaidi na rasilimali hiyo muhimu.

Vilevile  ameipongeza TPDC kwa jitihada wanazoendelea kufanya katika utafutaji na uendelezaji wa rasilimali za mafuta na gesi asilia nchini kwani uboreshaji huo umeanza kuleta matokeo chanya katika upatikanaji wa nishati hiyo katika maeneo mbalimbali nchini huku akiwataka kuhakikisha jitihada hizo zinawanufaisha wananchi wengi zaidi.

Katika hatua nyingine, Mhe. Salome amewapongeza PURA kwa kazi nzuri wanazozifanya katika kuhakikisha sekta ya mafuta inakua nchini huku akiwahimiza kuhakikisha mazingira ya uwekezaji yanakuwa rafiki kwa wawekezaji wapya ili kuongeza ajira na kuhakikisha wananchi wanapata manufaa ya moja kwa moja kutokana na rasilimali na uwekezaji uliopo nchini.  

Aidha, amesisitiza kuwa miradi ya utafiti na uendelezaji wa gesi asilia, ikiwemo mradi wa LNG, ipewe kipaumbele ili kuongeza tija katika uwekezaji na kuhakikisha nchi inanufaika kikamilifu na rasilimali zake huku akisisitiza kuwa taasisi zote zilizo chini ya Wizara lazima ziweke mbele maslahi ya wananchi wakati wa kusimamia miradi ya kimkakati ya nishati lakini pia kufuatilia utekelezaji wa maagizo ya Serikali kuhusu usimamizi, matumizi na faida za rasilimali za gesi asilia.

Kwa upande wake, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati, Dkt. James Mataragio amewasisitiza TPDC kuongeza kasi ya uzalishaji na upatikanaji wa  gesi ili nishati hiyo iwe ya kutosha na inawafikia wananchi huku akiisisitiza PURA kuhakikisha wanawapa wawekezaji kipaumbele katika kuwekeza katika fursa za mafuta na gesi kwa lengo la kuhakikisha Serikali inapata mapato na wananchi wananufaika na miradi hiyo.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa TPDC Mussa Makame amesema shirika linaendelea kuimarisha miundombinu ya kuhifadhi na kusafirisha nishati ya mafuta na gesi, huku likiandaa vizuri upande wa maboresho ya masoko ili kuongeza ufanisi na upatikanaji wa bidhaa hizo nchini na kueleza kuwa kampuni ipo kwenye hatua za kufanya upanuzi wa miradi ya gesi, ikiwemo utekelezaji wa miradi midogo ya LNG itakayowezesha kusafirisha gesi hiyo katika mikoa mbalimbali kwa gharama nafuu na kwa wakati.

Naye Mkurugenzi Mkuu wa PURA, Eng. Charles Sangweni amesema PURA itaendelea kutekeleza majukumu yake kwa ufanisi huku ikichangia kufanikisha malengo ya sekta kwa mujibu wa Dira ya Taifa 2050.

















Kampuni ya Noble Helium kutoka Australia imetangaza mpango wa kuajiri zaidi ya vijana 50 kupitia utafiti mpya wa Helium unaotarajiwa kuanza mwezi Desemba hadi Februari katika kijiji cha Kinambo, Wilayani Sumbawanga mkoani Rukwa.

Akizungumza kupitia mahojiano maalum hivi karibuni Mwakilishi wa Kampuni hiyo, Pius Simeon Mwita, alisema Noble Helium imefanikisha tafiti mbalimbali za awali na kubaini viashiria muhimu vya uwepo wa gesi ya Helium, huku ikichangia ajira na maendeleo kwa jamii zinazozunguka maeneo ya uchimbaji.

Mwita alisema katika tafiti zilizopita kampuni ilitoa ajira zisizo rasmi zipatazo 450, na pia ilishirikisha wananchi kwenye utoaji wa huduma kama ulinzi, usambazaji wa bidhaa, vilainishi kwa shughuli za uchorongaji, zabuni ndogo, ununuzi wa chakula pamoja na uboreshaji wa miundombinu ya barabara.

Aidha, alisema Noble Helium imekamilisha tathmini na ulipaji wa fidia kwa wananchi waliopo katika maeneo ya leseni ya utafiti wa Helium, ikiwa ni sehemu ya kuhakikisha shughuli za kampuni zinaendeshwa kwa kuzingatia maslahi ya jamii na sheria za nchi.

Kwa mujibu wa Mwita, utafiti mpya utakaofanyika Kinambo utaongeza nafasi nyingine zaidi 50 kwa vijana, na hivyo kuchochea maendeleo ya kiuchumi katika eneo hilo. 

“Tunawaomba vijana wajitokeze kwa wingi pindi fursa hizi zitakapotangazwa. Lengo letu ni kuhakikisha jamii inanufaika moja kwa moja na uwekezaji huu,” alisema.

Utafiti huo unatarajiwa kuongeza kasi ya maandalizi ya uwekezaji mkubwa wa Helium nchini, gesi ambayo imekuwa na mahitaji makubwa duniani kwa matumizi ya teknolojia za tiba, anga na vifaa vya sayansi.

 



Na Oscar Assenga, MUHEZA

VIKUNDI 29 vya Wanawake,Vijana na Watu Wenye ulemavu wamekabidhiwa Milioni 250 zinazotokana na mikopo asilimia 10 kutoka katika Halmashauri ya wilaya ya Muheza ikiwa ni kuwawezesha kujikwamua kiuchumi wao na jamii zao.

Makabidhiano ya Hundi ya Fedha hizo ilitolewa na Mkuu wa Mkoa wa Tanga Dkt,Balozi Batilda Burian na kushuhudiwa na viongozi mbalimbali wa wilaya ya Muheza akiwemo Mkuu wa wilaya,Mkurugenzi wa Halmashauri,Mwenyekiti wa Halamshauri na Madiwani wa Halmshauri hiyo.

Akizungumza baada ya kukabidhi mikopo hiyo ,Mkuu huyo wa Mkoa aliwaasa wanufaika wa mikopo ya asilimia 10 ya Halmashauri kuitumia kwa uangalifu ili kuweza kujikwamua kiuchumi pamoja na kuhakikisha wengine nao wananufaika na fursa hizo.

Alisema kwamba dhamira ya Rais Dkt Samia Suluhu ni kuona mikopo hiyo inawafikia wahitaji bila kuwepo kwa vikwazo vya aina yoyote kupitia mfumo wa mtandao bila kuhitaji kumjua mtu .

Aidha alitoa wito kwa vijana kujitokeza kwa wingi kuchangamkia fursa za uwepo wa mikopo hiyo ili waweze kujikwamua kiuchumi.

“Tumekubaliana kuandaa kongamano la vijana litakalowakutanisha maafisa maendeleo ya jamii na wadau wa mikopo kwa lengo la kuwaelimisha juu ya mchakato mzima wa kuipata na jinsi ya kuunda vikundi imara”Alisema

Mkuu huyo wa mkoa alisema lengo ni kuhakikisha kila kijana anakuwa na uelewa hatua za kuomba mikopo na kutumia fursa zilizopo.

Awali akizungumza Mkuu wa wilaya ya Muheza Ayoub Sebabili alisema kwamba mikopo iliyozinduliwa ya asilimia 10 ,wanawake asilimia 4,vijana 4 na walemavu 2 huku akimpongeza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Muheza Dkt Jumaa Mhina na menejimentii ya halmshauri kwa kuratibu vizuri mikopo na kuwafikia walengwa.

Aliwaomba wanufaika wa mikopo hiyo watoa ushirikiano kwenye marejesho ili kuweza kutoa nafasi watu wengine kupata mikopo kwa lengo la kukuza kipato na kujikwamua kiuchumi.





“Tunaopokea mikopo hii tutoe ushirikiano wakati wa marejesho kwa sababu utapelekea mfuko wa mikopo uweze kuwa endelevu na kuwafikia watu wengine na hivyo kuondoa umaskini kwa mtu mmoja mmoja na wengine kunufika nayo”Alisisitiza



Naye kwa upande wake Mkurugenzi wa Halmshauri ya Muheza Dkt Jumaa Mhina alimpongeza Mkuu huyo wa wilaya akieleza kwamba ndio muhimili wa halmashauri kuhakikisha asilimia 10 inatoka na kufikia vikundi hivyo.


Dkt Jumaa alisema kwamba wameweka mkazo kwa vikundi vyote lakini hususani kwa vijana ambao siku za nyuma walikwa wanawatafuta kwa tochi hivyo sasa watawafuata vijana walipo ili kuwaibua waweze kuunda vikundi na hivyo kunufaika na mikopo asilimia 10 ikiwa ni sehemu ya kutengeneza ajira .



Mkuu wa Mkoa wa Njombe, Mhe. Anthony Mtaka,akizungumza katika Ibada ya Jumamosi katika Kanisa la Waadventista Wasabato (SDA) Njombe Mjini.

Na Mwandishi Wetu, Njombe

Mkuu wa Mkoa wa Njombe, Mhe. Anthony Mtaka, amewataka vijana wa kizazi kipya (Gen-Z) na wananchi kwa ujumla kuimarisha mshikamano na kuilinda amani ya Tanzania, akisisitiza kuwa ndiyo nguzo muhimu ya maendeleo ya taifa.

Akizungumza katika Ibada ya Jumamosi katika Kanisa la Waadventista Wasabato (SDA) Njombe Mjini, RC Mtaka amesema vijana wana nafasi kubwa katika kuhakikisha nchi inaendelea kuwa kisiwa cha amani.

“Vijana wetu wa Gen-Z wana wajibu wa kulinda amani ya Tanzania; ninyi ndiyo kizazi kinachobeba matumaini na sura ya taifa letu,"amesema.

Aidha, ameongeza kuwa amani ni matokeo ya haki na uwajibikaji wa kila mwananchi.

“Amani ni tunda la haki na wajibu, ni msingi thabiti wa maendeleo yetu kama jamii na kama taifa. Tuna wajibu wa kuilinda amani ya nchi yetu kwa wivu mkubwa… ni jukumu letu vijana wa leo kuitunza amani yetu kwa faida ya vizazi vilivyopo na vijavyo,"amesema.

Akizungumzia hali ya usalama mkoani Njombe, Mtaka amewahakikishia wananchi kuwa mazingira bado ni salama na hakuna viashiria vya kuvuruga utulivu.

“Mkoa wetu bado upo salama, hauna matishio ya kihalifu. Tunaendelea kujenga mazingira thabiti ya ulinzi wa watu na mali ili kutoa fursa kwa wananchi kuendelea na shughuli zao za uzalishaji. Usalama huu utaongeza imani kwa wawekezaji kuendelea kuchagua Njombe kama sehemu sahihi ya kuweka mitaji,” amesema.

Hata hivyo, amewataka wananchi kuendelea kushirikiana na vyombo vya dola kwa kutoa taarifa za mapema pale wanapohisi au kuona dalili za kuvunjika kwa amani.

“Wananchi wenzangu, mkiona au kuhisi dalili yoyote hata ndogo inayoashiria uvunjifu wa amani au kuhatarisha usalama wa eneo lenu au maisha ya mtu, basi mtoe taarifa mapema. Ulinzi shirikishi huanza na wanajamii mmoja mmoja,” amesisitiza.

Amehimiza umoja, uzalendo na uadilifu wa wananchi wote ili kuendelea kujenga Njombe yenye fursa, utulivu na maendeleo endelevu.

Makundi mbalimbali ya Vijana wanajishughulisha na shughuli mbalimbali za kajamii ikiwemo bodaboda wametakiwa kuacha kujihusisha na matukio yenye kuharibu amani ya nchi na badala yake wawe mstari wa mbele katika kuilinda na kuitunza amani iliyopo.

Hayo yamesemwa na mbunge wa jimbo la korogwe vijijini Mheshimiwa Timotheo Mnzava katika ziara yake ya kukutana na makundi mbalimbali ikiwemo vijana wanaojishughulisha na shughuli mbalimbali za kiuchumi ikiwemo madereva bodaboda.

Akizungumza na vijana wa jimbo hilo amesisitiza kuwa ni vyema kuilinda amani iliyopo kwa nguvu zote huku akisistiza vijana hao kutojihusisha katika maandamano yanayotajwa kufanyika desemba 9 ambayo si halali kisheria kwani wapo baadhi ya vijana walioweza kupata athari mbalimbali ikiwemo ulemavu katika maandamano ya oktoba 29.

Kwa upande wao baadhi ya vijana hao wameahidi kutojihusisha na matukio ya ukatili badala yake watakuwa mabalozi wazuri wa amani.

MKUU wa Wilaya ya Bagamoyo, Shaibu Ndemanga, amewapongeza Wakala wa Maendeleo ya Uongozi wa Elimu (ADEM) kwa kuratibu na kushiriki kikamilifu mbio za marathon zilizolenga kuhamasisha juhudi za kuboresha miundombinu ya elimu katika chuo hicho.
   

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Adolf Mkenda, amesema kuwa Serikali inawetegemea wanasayansi na wahandisi ili kufanikisha dhamira ya Tanzania ya kujenga uchumi wa viwanda, amesisitiza kuwa kundi hilo lina mchango katika kuendeleza ubunifu, kuongeza tija na kuleta maendeleo endelevu nchini.

Prof. Mkenda amesema hayo Disemba 5, 2025 jijini Dar es Salaam katika Mahafali ya 19 ya Taasisi ya Teknolojia ya Dar es Salaam (DIT), akisema katika kutimiza azma hiyo Serikali imeendelea kuongeza fursa za mafunzo na Elimu ya Ufundi na Mafunzo ya Ufundi Stadi ili kusimamia ubora wa elimu sambamba na utekelezaji wa Sera ya Elimu na Mafunzo ya mwaka 2014, Toleo la 2023.

"Mhe Dkt. Samia Suluhu Hassan amedhamiria kuleta mageuzi ya elimu, kwa kuwawezesha watanzania hususan vijana kupata maarifa, stadi na ujuzi ili kuchangia maendeleo ya kijamii na kiuchumi" Amesema Waziri Mkenda.

Amebainisha kuwa, Serikali kupitia mkopo nafuu wa Benki ya Dunia imewekeza jumla ya Dola za Marekani milioni tisini (90) ambapo kupitia fedha hizo Taasisi ya DIT, imeanzisha Kituo cha Umahiri cha Kikanda cha Mafunzo ya TEHAMA (RAFIC) katika Kampasi ya Dar es Salaam na Kituo cha Umahiri cha Uchakataji bidhaa za ngozi (CELPAT) kampasi ya Mwanza.

Ameipongeza DIT kwa kuendelea kutoa mafunzo bora, sambamba na kutambua, kujenga, kukuza na kuendeleza bunifu. Amesema kuwa Serikali inajivunia juhudi hizo na ameisisitiza kuendelea kusimamia majukumu yake kikamilifu.

Mkuu wa Taasisi ya DIT, Profesa Preksedis Ndomba, amesema kuwa Taasisi hiyo imejikita katika dhana ya ufundishaji inayotilia mkazo mafunzo kwa vitendo pamoja na ziara za mafunzo viwandani, ambayo imewasaidia wanafunzi kuwa wabunifu na kufikia viwango vya kuanzisha makampuni.

Naye, Mwenyekiti wa Baraza la Taasisi hiyo, Dtk. Richard Masika ameishukuru Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutenga zaidi ya Sh. Bilioni mbili katika mwaka wa fedha 2025/26, ili kuanzisha Kituo cha Ujasiriamali, Ubunifu na Uhawilishaji wa Teknolojia kupitia Mradi wa TELM II.

Kumbuka, Mradi huo wa miaka miaka mitano (2025/2030) unatekelezwa kwa bajeti ya Euro milioni 19.79 (sawa na Sh. Bilioni 54). Fedha hizo ni mkopo nafuu kutoka Serikali ya Italia kwa Serikali ya Tanzania kupitia makubaliano rasmi.

Taasisi zingine zinazonufaika na Mradi wa TELMS II, ni Chuo Kikuu cha Sayansi na Teknolojia Mbeya (MUST), Chuo cha Ufundi Arusha (ATC) na Taasisi ya Sayansi na Teknolojia ya Karume (KIST).

Katika duru ya kwanza ya mahafali hayo, Waziri Mkenda amewatunuku vyeti jumla ya wahitimu 1,341 katika ngazi za Astashahada, Stashahada, Shahada na Shahada ya Uzamivu katika nyanja za Sayansi na Teknolojia. Kati ya hao, wanaume ni 1,003 na wanawake 338.