Na OWM - TAMISEMI, Dar es Salaam

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa  (OWM-TAMISEMI), Mhe. Prof. Riziki Shemdoe amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutoa zaidi ya Shingi Bilioni 28 zilizorejesha tabasamu kwa wafanyabiashara wa Kariakoo ambazo zimetumika kujenga Soko Jipya la Kariakoo na kukarabati Soko la zamani la Kariakoo ambalo liliharibika kutokana na janga la moto  Oktoba 07, 2021.

Prof. Shemdoe ametoa shukrani hizo leo kwa Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan alipokuwa akitoa neno la utangulizi, wakati ya hafla ya ufunguzi wa Soko Kuu Jipya la Kariakoo iliyofanyika jijini Dar es Salaam. 

“Mhe. Rais natumia fursa hii kutoa shukrani za dhati kwa nia yako njema ya kurejesha tabasamu kwa wafanyabishara na wananchi, kwa kutoa fedha zaidi ya  Shilingi Bilioni 28 ili kujenga soko jipya na kukarabati lililoteketea kwa janga la moto la Oktoba 07, 2021”, ameeleza Prof. Shemdoe.

Prof. Shemdoe ameongeza kuwa, Soko la Kariakoo ni kitovu cha biashara ndani ya Jiji la Dar es Salaam na Taifa kwa ujumla, hivyo ofisi yake kwa kutambua hilo itahakikisha  soko hilo linatoa huduma bora na kwa ufanisi ili kuleta tija na kuakisi thamani ya fedha iliyowekezwa na Serikali.

Sanjali na hilo, Prof. Shemdoe amesema kuwa, Serikali inaendelea na utaratibu wa kuhakikisha barabara zote zinazozunguka Soko la Karikakoo na maeneo jirani zinafunguliwa ili ziweze kupitika wakati wote na kulifanya soko litoe huduma kwa wananchi masaa 24.

Aidha, Prof. Shemdoe ametumia fursa hiyo kumshukuru Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kumuamini na kumteu kuwa Waziri anayesimamia Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na kumuahidi Mhe. Rais kwamba atafanya kazi kwa bidii na uadilifu mkubwa.

 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akivuta kitambaa kuashiria uzinduzi wa Soko Kuu jipya la Kariakoo, Ilala Jijini Dar es Salaam tarehe 08 Februari, 2026.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa katika picha ya pamoja na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba, katika eneo la jiwe la ufunguzi wa Soko Kuu jipya la Kariakoo, Ilala Jijini Dar es Salaam tarehe 08 Februari, 2026.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akikata utepe kuashiria uzinduzi wa Soko Kuu jipya la Kariakoo, Ilala Jijini Dar es Salaam tarehe 08 Februari, 2026.
Wageni na viongozi mbalimbali wakiwa kwenye hafla ya ufunguzi wa Soko Kuu jipya la Kariakoo, Ilala Jijini Dar es Salaam tarehe 08 Februari, 2026.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mhe. Patrobas Katambi pamoja na Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wanawake na Makundi Maalum Dkt. Doroth Gwajima wakiwa katika uzinduzi huo.

 

Kassim Nyaki, Ndutu Ngorongoro.

Waswahili husema aungurumapo Simba mcheza nani?

Tarehe 7 Februari, 2026 Simba ameunguruma  ndani ya hifadhi ya Ngorongoro eneo la Ndutu kwa uzinduzi wa Chapa mpya ya Destination Ngorongoro.

Kamishna wa Uhifadhi mamlaka ya Hifadhi ya eneo la Ngorongoro (NCAA) Abdul-Razaq Badru ameongoza Menejimenti ya mamlaka hiyo na wadau mbalimbali wa sekta ya utalii kuzindua  Utambulisho Mpya wa Chapa ya “Destination Ngorongoro” inayoashiria mwanzo mpya wa maajabu ya Ngorongoro ambayo kwa miongo mingi imekuwa ikivutia dunia kwa uzuri wake wa kipekee.

Akizindua utambulisho huo katika eneo la Ndutu  Ngorongoro, Kamishna Badru ameeleza kuwa kabla Ngorongoro haijawa kivutio cha utalii kinachotambuliwa duniani, ilikuwa ni sauti yenye mwito wa uhai unaounganisha Wanyamapori, utamaduni, ardhi, historia ya mwanadamu, malikale, mazingira na maumbo mbalimbali yanayoiakisi dunia ilipojikunja na kuunda Kasoko ya Ngorongoro.

“Katika dunia ambayo ushindani wa vivutio vya utalii ni mkubwa unaozidi kuwa na Faru, tembo  na visukuku pekee, Ngorongoro imeamua kujipambanua zaidi kwa mwito wenye dhamana na wajibu ndio maana tunawatambulisha rasmi muonekano mpya wa chapa ya Destination Ngorongoro kwa kufanya maboresho ya namna Ngorongoro inavyojitambulisha kwa dunia na kwa wageni kwa umahiri na muonekano ulioboreshwa” amefafamua kamishna Badru.

Moja ya maajabu ya kipekee ya asili duniani ni tukio la kuzaliana kwa nyumbu  eneo la Ndutu ambapo kila baada ya saa moja takribani ndama 80,000 huzaliwa. 

Katika Bonde la Olduvai na Laetoli, historia na nyayo za kwanza za binadamu zilipatikana zikitukumbusha kuwa Ngorongoro si hadithi ya wanyamapori pekee, bali ni Chimbuko la binadamu, hii ni ishara kuwa Ngorongoro ni maajabu yanayopaswa kusimuliwa hatua kwa hatua na  Ngorongoro sio tu unatazamwa bali inabaki na kuishi mioyoni mwa watu.

Kamishna Badru amebainisha kuwa maboresho ya chapa ya Ngorongoro hayapo kwenye muonekano pekee bali pia yanasimuliwa kwa hadithi za Ngorongoro ili wageni wa mataifa mbalimbali wanapogika  Ngorongoro kuielewa kwa undani zaidi. 

Simulizi za maajabu ya Ngorongoro zinaenda sambamba na  kuimarisha nyenzo kidijitali kwa uwazi zaidi na  upeo wa kimataifa ambapo Ngorongoro inazungumza kupitia hadithi moja iliyounganisha  mazingira hai historia ya binadamu, utamaduni, na asili na kuzungumza kwa sauti moja, mtindo mmoja, na utambulisho mmoja.

Badru anabainisha kuwa mwaka 2026 utakuwa Mwaka wa Maajabu,

chini ya kauli mbiu isemayo “Wonders Are Calling” ambayo itatekelezwa kwa awamu ikifichua maajabu ya Ngorongoro kwa kila msimu utaangazia ajabu tofauti.

Jee Maajabu hayo yatayofichuliwa kwa awamu yatakuwa ni yapii? Fuatana nasi katika taarifa zetu zijazo.

Enzi mpya ya Maajabu imeanza.

Mwito umetolewa.

Destination Ngorongoro, Experience the Wonders.




 

Na Kassim Nyaki, Ngorongoro.

Mabadiliko makubwa katika ushirikishwaji wadau wa sekta ya utalii yameibuliwa na uongozi Mamlaka ya Hifadhi ya  Ngorongoro ikianza mwanzo wa safari mpya ya simulizi kwa chapa ya Destination Ngorongoro kwa kuzungumza sauti moja, iliyo thabiti, yenye kujiamini na kukumbukwa.

Ngorongoro imeamua kuzindua shindano la upigaji  picha kwa waongoza watalii (Tour Guides)  lijulikanalo kama “The Birth of Wonders photo competition” katika eneo la Ndutu hususan msimu huu wa mazalia ya Nyumbu.

Akitangaza kampeni hiyo Kamishna Msaidizi Mwandamizi anayesimamia huduma za Utalii na Masoko Mariam Kobelo ameeleza kuwa shindano hilo linahusu eneo la Ndutu ambapo ndipo Safari Kuu ya Nyumbu huzaliwa na maisha kuanza ambapo eneo hilo hadithi ya Ngorongoro hujirudia upya kila mwaka.

“Waongoza Watalii ni mabalozi wetu muhimu katika kuisimulia Ngorongoro kwa dunia, katika msimu huu wa uzaaji wa nyumbu hapa Ndutu, tunawaalika kutumia lenzi zao kunasa pumzi za kwanza za uhai wa ndama, hatua za kwanza za ndama, mahusiano ya mama na mwana, 

Waongoza watalii watapaswa kupiga picha na kuzituma kupitia akaunti zao za instagram, _tag_ na kushiriki (collaborate) na akaunti rasmi ya  _instagram_ ya ngorongoro ijulikanayo kama (@visitngorongoro

Katika shindano hilo  la upigaji picha ( _The Birth of Wonders photo competition)_ Washindi watachaguliwa kwa kuzingatia ushiriki (engagement) wa watazamaji pamoja na kufuata masharti yote ya shindano ambapo mshindi wa kwanza atajinyakulia kitita kinono cha shilingi Milioni  3,000,000, mshindi wa pili shilingi milioni 2,000,000 na mshindi wa tatu atajishindia shilingi milioni 1,000,000 mtawalia.

Waongoza Watalii ambao ni washiriki wa kampeni hii wanakuwa wasimulizi wa sauti ya chapa ya _Destination Ngorongoro_ Kwani wao ndiyo mashuhuda wa kwanza wa simulizi ya uzao wa nyumbu.








 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akikata utepe kuashiria uzinduzi wa Soko Kuu jipya la Kariakoo, Ilala Jijini Dar es Salaam tarehe 08 Februari, 2026.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha ya pamoja na Waziri Mkuu Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba mara baada ya kufungua Soko Kuu jipya la Kariakoo, Ilala Jijini Dar es Salaam tarehe 08 Februari, 2026.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa mbele ya Soko Kuu jipya la Kariakoo mara baada ya ufunguzi uliofanyika Sokoni hapo, Ilala Jijini Dar es Salaam tarehe 08 Februari, 2026.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akivuta kitambaa kuashiria uzinduzi wa Soko Kuu jipya la Kariakoo, Ilala Jijini Dar es Salaam tarehe 08 Februari, 2026.

Wageni mbalimbali wakiwa kwenye hafla ya ufunguzi wa Soko Kuu jipya la Kariakoo, Ilala Jijini Dar es Salaam tarehe 08 Februari, 2026.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Waziri Mkuu Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba wakati wa hafla ya ufunguzi wa Soko Kuu jipya la Kariakoo, Ilala Jijini Dar es Salaam tarehe 08 Februari, 2026.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye hafla ya uzinduzi wa Soko Kuu jipya la Kariakoo, Ilala Jijini Dar es Salaam tarehe 08 Februari, 2026.

Matukio mbalimbali katika hafla ya ufunguzi wa Soko Kuu jipya la Kariakoo, Ilala Jijini Dar es Salaam tarehe 08 Februari, 2026.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akipokea zawadi ya picha mara baada ya kufungua Soko Kuu jipya la Kariakoo, Ilala Jijini Dar es Salaam tarehe 08 Februari, 2026.

Katibu Tawala wa Mkoa wa Mwanza, Bw. Balandya Elikana,akizungumza wakati akifungua mafunzo ya kuwajengea uwezo wafanyabiashara jijini Mwanza,ili  kuwaongezea uelewa kuhusu masuala ya ushindani wa soko pamoja na taratibu za kupata haki katika shughuli za kibiashara yaliyoandaliwa na Baraza la Ushindani wa Soko (FCT).

Na.Mwandishi Wetu-MWANZA

 BARAZA  la Ushindani wa Soko (FCT)  limetoa mafunzo ya kuwajengea uwezo wafanyabiashara jijini Mwanza, yakilenga kuwaongezea uelewa kuhusu masuala ya ushindani wa soko pamoja na taratibu za kupata haki katika shughuli za kibiashara.

Mafunzo hayo yaliwakutanisha wadau mbalimbali wa sekta ya biashara, ambapo waliipongeza Wizara ya Viwanda na Biashara chini ya Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kwa juhudi zake za kuweka mazingira bora ya biashara na uwekezaji kupitia uwepo wa chombo huru cha kusimamia na kudhibiti ushindani wa soko.

Akifungua semina hiyo, Katibu Tawala wa Mkoa wa Mwanza, Bw. Balandya Elikana, alisema kuwa mafunzo hayo ni muhimu kwa wadau wa sekta ya biashara kwani yanawawezesha kuelewa kwa kina majukumu ya Baraza la Ushindani pamoja na umuhimu wa mshikamano katika utekelezaji wa sheria za ushindani.

“Kupitia semina hii, wadau watapata uelewa mpana kuhusu Baraza la Ushindani na nafasi yake katika kulinda haki za mlaji pamoja na kuendeleza ushindani wa haki katika soko.”Alisema Bw.Elikana

Akizungumza katika mafunzo hayo, Msajili wa Baraza la Ushindani, Bw. Mbegu Kaskasi, alisema kuwa Baraza lipo kwa ajili ya kulinda masuala yote yanayohusu ushindani wa soko na kuchochea maendeleo ya kiuchumi nchini. Alieleza kuwa utekelezaji wa majukumu ya Baraza unalenga kuimarisha misingi ya utawala bora kwa kuhakikisha sheria za ushindani zinatekelezwa kikamilifu, kwa haki na kwa uwazi.

Aidha, aliongeza kuwa Baraza huhakikisha mamlaka za udhibiti zinazingatia taratibu na kanuni za ushindani wakati wa utekelezaji wa majukumu yao, sambamba na kutoa majibu sahihi na ya haraka katika migogoro ya kibiashara. Alibainisha kuwa hatua hiyo inalenga kumlinda mlaji dhidi ya vitendo vinavyodhoofisha ushindani, hivyo kuchangia katika ujenzi wa uchumi shindani, jumuishi na wenye tija kwa Watanzania.

Kwa upande wake, Meneja wa Mkoa wa Chemba ya Wafanyabiashara, Bw. Hassan Karambi, alisema kuwa amepata elimu yenye manufaa makubwa kupitia programu ya Baraza ya kuwajengea uwezo wadau.

Alieleza kuwa mafunzo hayo yamewasaidia wafanyabiashara kufahamu kuwa endapo hawataridhika na maamuzi ya mamlaka za udhibiti kama LATRA, TCRA, TCAA, EWURA, PURA pamoja na Tume ya Ushindani (FCC), wana haki ya kukata rufaa katika Baraza la Ushindani ili kupata haki yao.

Naye Meneja wa Mamlaka ya Mawasiliano Kanda ya Ziwa, Bi. Imelda Salumu, alifafanua utaratibu wa Baraza katika kupokea rufaa kutoka kwa wadau.

Alisema kuwa malalamiko huanza kwa mtoa huduma husika, na endapo hayatapatiwa ufumbuzi, hufikishwa katika mamlaka ya udhibiti kama hatua ya kwanza ya rufaa. Aliongeza kuwa iwapo mlalamikaji hataridhishwa na maamuzi ya mamlaka hiyo, utaratibu humruhusu kuwasilisha rufaa katika Baraza la Ushindani kwa hatua zaidi za kisheria.


Kijiji kilishuhudia tukio la kushtua. Daktari mmoja aliyekuwa akijitangaza kama mtaalamu wa upasuaji alinaswa akifanya kazi hatari mtaani. Watu walishangaa kuona kuwa huduma aliyoitoa ilikuwa hatari na haikufuata taratibu za afya.

Wagonjwa walikuwa wakijiingiza hatarini kila siku. Familia za wagonjwa walikuwa na hofu na wasiwasi. Hakukuwa na mamlaka ya kudhibiti kitendo hicho mara kwa mara, na tukio hili lilitokea bila kutarajiwa.

Baada ya tukio, watu walihisi wamesalia na mashaka na hofu kubwa. Familia na marafiki walijaribu kusaidia wagonjwa waliopata matatizo. Wengi walijua kuwa suluhisho la haraka lilihitajika.Soma Zaidi.
Mwanamke huyu alishangaza kijiji chote. Alidai kuwa nyumba ya jirani ni yake na akaanza kujaribu kuiuza. Wajirani walishangaa na kushangilia kwa hofu. Familia ya jirani ilihisi kutoamini kilichotokea.

Tukio hili lilipelekea kesi ya kisheria. Wajirani walijaribu kulinda haki yao. Kila hatua ilichukua muda na hofu ilikuwa kubwa. Mwanamke huyo alijikuta akishindwa kuelezea kitendo chake mbele ya mamlaka.

Baada ya tukio, watu walihisi wamesalia na mashaka. Wengi walihitaji mwongozo wa kisaikolojia na kiroho.Soma Zaidi.
Mume huyu alishangaza wakewe na familia yake. Alimfumania pastor kitandani kwake. Tukio hili liliibua hofu, hasira, na mshangao mkubwa. Familia ilijikuta ikitafuta njia ya kuelewa kilichotokea.

Pastor alidai kuwa alifanya yote kwa ajili ya kutoa pepo na kusaidia kuondoa dhambi. Wengine walishangaa na kushangilia. Watu walijikuta wakiwa kwenye mgongano wa hisia: kuamini au kushuku.

Hali iliendelea kuwa ngumu. Mume na wakewe walijikuta kwenye hofu ya kijamii na kiroho. Wote walihitaji mwongozo sahihi wa kuelewa na kushughulikia tukio hili lisiloeleweka.Soma Zaidi.