Nilipoanzisha biashara yangu, nilikuwa na ndoto kubwa za kujenga kampuni ambayo ingenipa uhuru wa kifedha na kusaidia familia yangu. Kwa miaka ya mwanzo, mambo yalikuwa yanaenda vizuri. Wateja walikuwa wengi, mauzo yalikuwa yanaongezeka, na nilikuwa na matumaini makubwa kuhusu siku zijazo.

Lakini hali ilibadilika ghafla.

Mauzo yalianza kushuka mwezi baada ya mwezi. Wateja ambao walikuwa waaminifu kwa biashara yangu walianza kupungua, na baadhi yao walihamia kwa washindani wangu. Nilijaribu kupunguza bei za bidhaa na kuanzisha ofa mbalimbali, lakini matokeo hayakuwa yale niliyotarajia.

Hasara zilianza kuongezeka. Kila mwisho wa mwezi nilikuwa nikiangalia hesabu za biashara na kuona fedha zikizidi kupungua. Baadhi ya wafanyakazi walihofia kuhusu mustakabali wa biashara hiyo, na hata mimi mwenyewe nilianza kujiuliza kama ningelazimika kuifunga.
Usiku mwingi nilikosa usingizi.

Nilikuwa nikifikiria jinsi ya kulipa madeni, kuhifadhi biashara, na kuhakikisha familia yangu haipati matatizo kutokana na hali hiyo. Kadri muda ulivyopita, presha iliongezeka zaidi. SOMA ZAIDI.

Baada ya kuhitimu masomo yangu, nilikuwa na matumaini makubwa ya kupata kazi nzuri na kuanza kujitegemea.

Nilituma maombi kwa kampuni nyingi, mashirika mbalimbali, na hata biashara ndogo ndogo zilizokuwa zinatafuta wafanyakazi. Kila nilipoitwa kwenye usaili, nilijiambia kwamba safari hii ndiyo nafasi yangu ya mwisho ya kubadilisha maisha.

Lakini majibu yalikuwa yale yale. Mara kwa mara nilipokea ujumbe wa kukataliwa. Wakati mwingine nilifika hatua za mwisho za usaili na kuambiwa nisubiri majibu, lakini siku zote nafasi hiyo ilipewa mtu mwingine. Miaka mitatu ilipita katika hali hiyo.

Akiba yangu ilianza kuisha na nilianza kutegemea msaada wa familia katika baadhi ya mahitaji yangu. Kilichoniumiza zaidi ni kuona watu niliomaliza nao shule wakipiga hatua kubwa maishani huku mimi nikibaki sehemu ileile. Nilianza kukata tamaa.

Kulikuwa na siku ambazo sikutaka hata kufungua barua pepe kwa sababu nilikuwa nimechoka kuona majibu ya kukataliwa. Hata hivyo, ndani yangu bado kulikuwa na tumaini dogo kwamba siku moja mambo yangebadilika. SOMA ZAIDI.
Mimi nilikuwa naishi na maumivu ya tumbo kwa muda mrefu sana. Kila siku nilikuwa naanza siku nikiwa sijisikii vizuri, na wakati mwingine maumivu yalikuwa yanazidi baada ya kula. Ilifika wakati nilianza kuogopa hata kula chakula kwa sababu sikujua kama nitapata maumivu tena.

Hali hii ilinifanya nipungue nguvu na hata uzito wangu ukaanza kushuka.
Nilitembelea vituo vya afya mara kadhaa, nikapewa dawa tofauti, lakini nafuu ilikuwa ya muda mfupi tu. Baada ya muda maumivu yalirudi tena kama kawaida.

Hali hii ilinichosha sana. Nilianza kukata tamaa na kuona kama nitakuwa na tatizo hili maisha yangu yote. Siku moja nilimweleza rafiki yangu wa karibu hali yangu. SOMA ZAIDI.

Bodi ya Usimamizi wa Stakabadhi za Ghala (WRRB) imetunukiwa tuzo ya kutambua mchango wake katika kufanikisha utafiti kuhusu maboresho ya kisasa ya mnyororo wa thamani wa kilimo uliofanywa na Taasisi ya Kimataifa ya Utafiti wa Maendeleo ya Canada (IDRC-CRDI) kwa kushirikiana na Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM).

Tuzo hiyo imekabidhiwa leo kwa Mkurugenzi Mtendaji wa WRRB, Bw. Asangye Bangu, na Meneja wa Kitengo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) wa Bodi hiyo, Bw. Elfaraja Kintingu.

Akizungumza baada ya kupokea tuzo hiyo, Bw. Bangu amesema heshima hiyo ni uthibitisho wa nafasi muhimu ya WRRB katika kuimarisha sekta ya kilimo kupitia Mfumo wa Stakabadhi za Ghala, ambao umeendelea kuongeza ufanisi wa biashara ya mazao, uwazi wa masoko na ushindani wa bei katika masoko ya ndani na nje ya nchi.

Amesema WRRB itaendelea kushirikiana na taasisi za utafiti na wadau mbalimbali katika kuendeleza ubunifu na maboresho yanayochochea maendeleo ya mnyororo wa thamani wa kilimo kwa manufaa ya wakulima na uchumi wa Taifa.

Awali, akielezea kuhusu tuzo hiyo, Bw. Kintingu amesema imetolewa kwa kutambua ushirikiano na mchango wa WRRB katika kufanikisha utafiti huo, ambapo watafiti walitembelea ghala mbalimbali nchini ili kujionea utekelezaji wa Mfumo wa Stakabadhi za Ghala na mchango wake katika kuimarisha biashara ya mazao, kuongeza uwazi wa masoko na kuboresha mnyororo wa thamani wa kilimo.

✅ Wajadili Fursa za Ajira kwa Madereva wa Kitanzania

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Deus Sangu amekutana na kufanya mazungumzo na Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Usafirishaji ya MOWASALAT, Ahmad Hassan Al Obaidly, alipofanya ziara katika kampuni hiyo tarehe 8 Julai, 2026, jijini Doha, nchini Qatar.

Aidha, mazungumzo yao yalilenga majadiliano kuhusu kuendelea kuimarisha ushirikiano kati ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Kampuni ya MOWASALAT katika sekta ya usafirishaji na masuala ya ajira, hususan kuongeza fursa za ajira kwa Madereva wa Kitanzania nchini Qatar.

Katika ziara hiyo, Waziri Sangu aliambatana na Balozi wa Tanzania nchini Qatar, Mhe. Habibu Awesi Mohamed, Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Ajira na Mahusiano, Zuhura Yunus, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Vijana, Ajira na Uwezeshaji Zanzibar, Khalid Masoud Waziri, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Kazi na Uwekezaji, Rashid Ali Salim, pamoja na Kaimu Mkurugenzi wa Kitengo cha Huduma za Ajira, Jane Sorogo.

-Geneva, Julai 2026

Tanzania imelitaka Shirika la Miliki Ubunifu Duniani (WIPO) kujenga mfumo wa kimataifa wa miliki bunifu unaowezesha nchi zinazoendelea kunufaika na maendeleo ya akili mnemba (Artificial Intelligence–AI), huku ikisisitiza umuhimu wa kuhamasisha matumizi ya teknolojia na kujengea watu uwezo.
- Wajadili Fursa za Ajira kwa Madereva wa Kitanzania

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Deus Sangu amekutana na kufanya mazungumzo na Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Usafirishaji ya MOWASALAT, Ahmad Hassan Al Obaidly, alipofanya ziara katika kampuni hiyo tarehe 8 Julai, 2026, jijini Doha, nchini Qatar.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Deus Sangu akizungumza na Wafanyakazi Madereva wa Kitanzania wanaofanya kazi katika kampuni ya MOWASALAT iliyopo nchini Qatar alipofanya ziara katika kampuni hiyo, tarehe 8 Julai, 2026.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Deus Sangu akizungumza na Wafanyakazi Madereva wa Kitanzania wanaofanya kazi katika kampuni ya MOWASALAT iliyopo nchini Qatar alipofanya ziara katika kampuni hiyo.

Na: OWM (KAM) – Doha, Qatar

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Deus Sangu, amewahimiza Watanzania wanaofanya kazi nchini Qatar kuzingatia nidhamu, uwajibikaji na uadilifu wanapotekeleza majukumu yao ili kuendelea kujenga taswira nzuri ya Taifa la Tanzania na kufungua fursa zaidi za ajira na maendeleo kwa Watanzania wengine.

Mhe. Sangu ametoa wito huo  jijini Doha, Qatar, alipokutana na kuzungumza na Wafanyakazi Madereva wa Kitanzania wanaofanya kazi katika kampuni ya MOWASALAT iliyopo nchini humo, ambapo alisisitiza umuhimu wa kufuata sheria, kuheshimu mikataba ya ajira na kutekeleza majukumu kwa weledi.

Amesema kuwa mafanikio yanayoendelea kupatikana kwa Watanzania katika nchi mbalimbali yanatokana na juhudi, kujituma na kuonesha uwezo katika maeneo yao ya kazi.

“Uwepo wa Watanzania wanaofanya kazi katika mataifa ya nje kwa bidii ni sifa kubwa kwa taifa, kwani inasaidia kujenga imani na mahusiano mazuri kati ya Tanzania na mataifa mengine, hivyo kutoa fursa zaidi kwa vijana wengine kupata nafasi za ajira na kujifunza,” amesema Waziri Sangu Ameongeza kuwa Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan itaendelea kuweka mazingira wezeshi ya kuongeza fursa za ajira na kuimarisha ushirikiano wa kimataifa katika masuala ya ajira na kukuza maendeleo ya rasilimali watu.

Vile vile, Waziri Sangu amewataka Watanzania hao kuendelea kushirikiana na viongozi wa Serikali hususan Ofisi za Ubalozi, ili kupata mwongozo na msaada pale inapohitajika kuhusiana na masuala ya kisheria, kanuni na taratibu za nchi wanayoishi.

Kadhalika, Mhe. Sangu amewahamasisha madereva hao kuendelea kuwa mabalozi wazuri wa kulitangaza taifa la Tanzania kupitia juhudu zao katika kazi. Pia, amewahamasisha kujiunga katika Mfuko wa Taifa wa Hifadhi Jamii (NSSF) kupitia Hifadhi Scheme ili kujijengea usalama wa kipato na ustawi wa maisha yao baada ya kustaafu au wanapokumbwa na changamoto mbalimbali za maisha, kwa kuwa hatua hiyo ni uwekezaji muhimu kwa manufaa yao binafsi na familia zao.

Naye, Balozi wa Tanzania nchini Qatar, Mhe. Habibu Awesi Mohamed amewahakikishia wafanyakazi hao kupatiwa ushirikiano wakati wowote watakapokuwa wanahitaji kupata huduma, ushauri na msaada mbalimbali wanapokuwa katika nchi hiyo.

Kwa upande wa Madereva hao wakizungumza kwa nyakati tofauti, wameshukuru Serikali kwa kuwaunganisha na fursa za ajira nje ya nchi.

“Tunaishukuru sana Serikali kwa kutufungulia milango ya ajira nje ya nchi. Tunaomba juhudi hizi ziendelezwe ili vijana wengi zaidi waliopo Tanzania wapate fursa kama tulizopata sisi kwa kuwa zitaboresha maisha yao pamoja na kuwawezesha kuchangia maendeleo ya Taifa,” amesema Zulekifli Ali Massawe

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Deus Sangu akizungumza na Wafanyakazi Madereva wa Kitanzania wanaofanya kazi katika kampuni ya MOWASALAT iliyopo nchini Qatar alipofanya ziara katika kampuni hiyo.

Sehemu ya Viongozi kutoka Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Kampuni ya MOWASALAT pamoja na Wafanyakazi Madereva wa Kitanzania wanaofanya kazi katika kampuni ya MOWASALAT iliyopo nchini Qatar wakifuatilia hotuba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Deus Sangu (hayupo pichani) alipofanya ziara katika kampuni hiyo.

Balozi wa Tanzania nchini Qatar, Mhe. Habibu Awesi Mohamed akieleza jambo Wafanyakazi Madereva wa Kitanzania wanaofanya kazi katika kampuni ya MOWASALAT iliyopo nchini Qatar wakati wa ziara ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Deus Sangu katika kampuni hiyo.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Deus Sangu akisikiliza maoni ya Wafanyakazi Madereva wa Kitanzania wanaofanya kazi katika kampuni ya MOWASALAT iliyopo nchini Qatar alipofanya ziara katika kampuni hiyo.

Mkurugenzi wa Uendeshaji kutoka Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF), Bw. Omary Mziya pamoja na Meneja Mahusiano na Elimu kwa Umma NSSF, Bi. Lulu Mengele wakitoa elimu kwa Wafanyakazi Madereva wa Kitanzania wanaofanya kazi katika kampuni ya MOWASALAT iliyopo nchini Qatar wakati wa ziara ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Deus Sangu alipotembelea kampuni hiyo.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Deus Sangu akiwa katika picha ya pamoja na Wafanyakazi Madereva wa Kitanzania wanaofanya kazi katika kampuni ya MOWASALAT iliyopo nchini Qatar alipofanya ziara katika kampuni hiyo.

Kaimu Mkurugenzi wa Kitengo cha Huduma za Ajira, Bi. Jane Sorogo akieleza jambo Wafanyakazi Madereva wa Kitanzania wanaofanya kazi katika kampuni ya MOWASALAT iliyopo nchini Qatar wakati wa ziara ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Deus Sangu katika kampuni hiyo.

Na Mwandishi Wetu

WANAFUNZI wanaosoma mkondo wa elimu ya amali katika Shule ya Sekondari Dar es Salaam wameeleza kuwa ufadhili wa vifaa vya ushonaji uliotolewa na Mamlaka ya Elimu Tanzania (TEA) umeleta mapinduzi makubwa katika utoaji wa mafunzo ya vitendo, hatua inayowajengea uwezo wa kujiajiri na kuanzisha biashara mara baada ya kuhitimu masomo yao.

Kiwanga Doctors wanaendelea kujijengea jina miongoni mwa watu wanaotafuta msaada wa kushughulikia changamoto zinazowakabili katika maisha ya kila siku. Kwa mujibu wa wateja mbalimbali waliowahi kutafuta huduma zao, wamekuwa wakipata ushauri na mwongozo unaowasaidia kurejesha matumaini katika nyanja tofauti za maisha.

Baadhi ya wateja wanasema walifika Kiwanga Doctors wakikabiliwa na migogoro ya ndoa iliyokuwa imechukua muda mrefu bila kupata suluhisho. Kwa mujibu wao, baada ya kufuata ushauri walioupokea, mahusiano yao yalianza kuimarika na familia zao kurejea katika hali ya maelewano.

Katika upande wa biashara, wapo wafanyabiashara wanaodai walikuwa wakipitia kipindi kigumu cha kushuka kwa mauzo na hasara za mara kwa mara. Wanasema walipopata ushauri kutoka Kiwanga Doctors walirejea kufanya biashara kwa ari mpya, jambo ambalo, kwa mujibu wao, liliwasaidia kuona mabadiliko chanya katika shughuli zao za kila siku.SOMA ZAIDI.
MKwa watu wengi, changamoto za mahusiano zinaweza kuleta maumivu makubwa, hasa pale penzi linapovunjika au mwenza anapoondoka bila matarajio ya kurejea. Hata hivyo, baadhi ya wateja wanasema walipata mwongozo uliowapa matumaini mapya wakati walipokuwa wamekata tamaa.

Kwa mujibu wa ushuhuda wao, baadhi yao walikuwa wameachwa na wenza wao, ndoa zilikuwa ukingoni kuvunjika, huku wengine wakidai walikuwa wamepoteza mawasiliano kabisa na watu waliowapenda. Wanasema baada ya kufuata ushauri walioupokea, mahusiano yao yalianza kuboreka hatua kwa hatua, mawasiliano yakarejea na katika baadhi ya matukio walifanikiwa kupatana tena na wapenzi wao.

Wengine pia wanasema walikuwa wakikabiliwa na migogoro ya mara kwa mara ndani ya ndoa, ukosefu wa maelewano na kutokuaminiana. Kwa mujibu wao, walipata mwongozo uliowasaidia kujenga upya mahusiano yao na kurejesha ut. SOMA ZAIDI.
Kupata ajira ni changamoto inayowakabili watu wengi, hasa baada ya kutuma maombi mengi bila kuitwa kwenye usaili. Hata hivyo, baadhi ya wateja wanasema walipata matumaini mapya baada ya kutafuta ushauri walipokuwa wamekata tamaa.

Kwa mujibu wa ushuhuda wao, baadhi yao walikuwa wamekaa kwa muda mrefu bila kazi licha ya kuwa na elimu na uzoefu unaohitajika. Wanasema walipopata mwongozo na kufuata ushauri walioupokea, walianza kuona mabadiliko, ikiwa ni pamoja na kuitwa kwenye usaili na baadaye kupata nafasi za ajira walizokuwa wakizitafuta.

Wengine wanadai walikuwa wakikosa mafanikio ya mara kwa mara katika maombi ya kazi, huku wengine wakisema walikuwa wakikwama katika hatua za mwisho za usaili. Kwa mujibu wao, walirejea na ushuhuda wakisema walipata fursa zilizowabadilisha maisha yao.

Baadhi ya wateja pia wanasema walipata maendeleo katika biashara, ongezeko la wateja na kuimarika kwa shughuli zao za kiuchumi baada ya kupata ushauri. Wengine wanadai walifanikiwa kurejesha kujiamini na mtazamo chanya uliowasaidia kufuatilia malengo yao kwa bidii zaidi. SOMA ZAIDI.

Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Judith Kapinga (Mb), amewataka Watanzania kuendelea kutembelea Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba), akisema maonesho ya mwaka huu 2026 yameonesha mafanikio makubwa ya maendeleo ya viwanda, ubunifu wa teknolojia na ubora wa bidhaa zinazozalishwa nchini.

Akizungumza Julai 08, 2026 baada ya kutembelea mabanda mbalimbali ya maonesho hayo, Kapinga amesema mwitikio wa wananchi ni mkubwa kiasi kwamba Serikali inatafakari kuongeza siku moja ya maonesho ili kutoa nafasi kwa wananchi wengi zaidi kushiriki na wafanyabiashara kuendelea kufanya biashara.

Amesema ukubwa wa maonesho hayo unamlazimu kuyatembelea mara kwa mara kwa kuwa haiwezekani kuona mabanda yote kwa siku moja, huku akieleza kuridhishwa na namna waoneshaji walivyojiandaa na ubora wa bidhaa zinazooneshwa.

Waziri Kapinga amesema maonesho ya mwaka 2026 yamebeba teknolojia mbalimbali za kisasa, ikiwemo magari yanayotumia umeme, magari ya mseto (hybrid), magari yanayotumia gesi asilia (CNG) kwa asilimia 100 pamoja na mitambo ya kisasa inayotumia umeme, hatua inayoonesha ukuaji wa sekta ya viwanda na matumizi ya teknolojia rafiki kwa mazingira.

Aidha, amesema bidhaa za ndani zimeendelea kuongezeka ubora, hususan katika thamani na vifungashio, jambo linalodhihirisha mafanikio ya uwekezaji wa Serikali katika kuwawezesha wananchi kiuchumi na kukuza uzalishaji wa ndani.

"Wananchi waendelee kujitokeza kutembelea Sabasaba. Fursa zilizopo mwaka huu ni nyingi zaidi, hivyo ni wakati mzuri wa kujifunza, kufanya biashara na kuona maendeleo ya viwanda vya Tanzania," amesema Kapinga.

Ameongeza kuwa iwapo uamuzi wa kuongeza siku moja ya maonesho utapitishwa, utalenga kuwapa wananchi, hasa wanaokuwa kazini siku za kawaida, nafasi zaidi ya kutembelea maonesho hayo na kunufaika na fursa mbalimbali za biashara na uwekezaji.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Deus Sangu, akiwa kaitika mazungumzo na Waziri wa Kazi wa Qatar, Mhe. Dkt. Ali bin Samikh Al Marri, leo Julai 8, 2026, jijini Doha, nchini Qatar.
Na Said Mwishehe,Michuzi TV-Zanzibar

KIZIMKAZI Kumenoga! Hiyo ndio kauli mbiu iliyobeba Tamasha la Kizimkazi 20226 linatarajiwa kufanyika kuanzia Agosti 12 hadi Agosti 14 mwaka huu likiwa limesheheni fursa lukuki .
Waziri wa Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Juma Homera akisaini kitabu cha wageni alipotembelea banda la Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali wakati wa Maonesho ya Sabasaba yaliyofanyika Jijini Dar es Salaam.
Naibu Wakili Mkuu wa Serikali Bi. Alice Mtulo (aliyesimama katikati) akiwa pamoja na watumishi wa Ofisi ya Wakili Mkuu wakati wa Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba) yanayoendelea Jijini Dar es Salaam.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Deus Sangu, akiwa katika mazungumzo na Waziri wa Kazi wa Qatar, Mhe. Dkt. Ali bin Samikh Al Marri, leo Julai 8, 2026, jijini Doha, nchini Qatar.

Na.Mwandishi Wetu

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Deus Sangu, amekutana na kufanya mazungumzo na Waziri wa Kazi wa Qatar, Mhe. Dkt. Ali bin Samikh Al Marri, leo Julai 8, 2026, jijini Doha, nchini Qatar.

Mazungumzo ya Viongozi hao yamelenga kuimarisha ushirikiano kati ya Tanzania na Qatar katika sekta ya kazi na ajira, hususan eneo la kukuza maendeleo ya rasilimali watu, ulinzi na haki za wafanyakazi pamoja na kuongeza fursa za ajira kwa Watanzania.

Vilevile, wamejadili kuhusu Mkutano wa Uhamaji wa Wafanyakazi (Labour Mobility Dialogue) utakaowakutanisha nchi wanachama wa Baraza la Ushirikiano la Nchi za Ghuba (GCC), Jordan, Lebanon na nchi za Afrika zinazotuma wafanyakazi nje ya nchi chini ya mwamvuli wa Umoja wa Afrika (African Union). Mkutano huo unatarajiwa kufanyika Oktoba 2026 Tanzania, jijini Dar es Salaam, ukiwa na lengo la kuimarisha ushirikiano, kubadilishana uzoefu na kupanua fursa za ajira salama na zenye staha kwa wananchi wa nchi shiriki.

Katika kikao hicho, Waziri Sangu aliambatana na Balozi wa Tanzania nchini Qatar, Mhe. Habibu Awesi Mohamed, Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Ajira na Mahusiano, Zuhura Yunus, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Vijana, Ajira na Uwezeshaji Zanzibar, Khalid Masoud Waziri, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Kazi na Uwekezaji, Rashid Ali Salim, pamoja na Kaimu Mkurugenzi wa Kitengo cha Huduma za Ajira kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Ajira na Mahusiano, Jane Songoro.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Deus Sangu, akiwa katika mazungumzo na Waziri wa Kazi wa Qatar, Mhe. Dkt. Ali bin Samikh Al Marri, leo Julai 8, 2026, jijini Doha, nchini Qatar.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Deus Sangu, akimkabidhi tuzo Waziri wa Kazi wa Qatar, Mhe. Dkt. Ali bin Samikh Al Marri, tuzo ya kutambua ushirikiano katika ya Tanzaniana Qatar katika masuala ya Ajira, leo Julai 8, 2026, katika Ofisi za Wizara hiyo ya Kazi Jijini Doha, nchini Qatar.