Na Ahmed Mahmoud,
WATU 1800 wanapata chanjo ya Uviko-19 Mkoani Tanga, kwa siku
tofauti na awali ambapo idadi ilikuwa 500 kwa siku. Mganga mkuu wa mkoa wa
Tanga, Dkt ,Jonathan Badem ameyasema hayo Jijini Tanga kwenye kikao cha kamati
ya Uhamasishaji wa Chanjo ya kitaifa ofisini mwake walipofika kujitambulisha
wakati akielezea sekta ya afya. Dkt Badem alisema hivi sasa kuna mwamko tofauti
na awali walikuwa wanachanjwa watu 66 kwa siku ila hivi sasa wanachanjwa watu
500 kwa siku. “Ongezeko hilo la watu kuchanjwa limekuja baada ya kuingia chanjo
mpya ya Sinopharm, ambapo watu wengi wameichangamkia,” alisema Dkt . Alisema
walipokea dozi mpya 36,766 na hadi hivi sasa wamechanja watu 36,112 kwenye
Wilaya sita za mkoa wa Tanga. Alisema mipango ya idara ya afya ni kuongeza kasi
ya kuchanja hadi kufikia watu 3,000 hadi 4000 kwa siku. “Hali ikiendelea kuwa
hivi itatuchukua muda wa miezi sita kufikia asilimia 60 ya malengo
tuliyojiwekea,” amesema Dk Kayera. Alisema ushirikiano wa viongozi wa mkoa huo
wa kisiasa, kidini na kimila ndiyo imekuwa chachu ya watu kuzidi kujitokeza
kuchanja. “Nawasihi wananchi waendelee kujitokeza kwa wingi kupata chanjo ya
Uviko-19 kwenye mahospitali, vituo vya afya na zahanati. Kwa Upande wake Mratibu
wa Timu ya Taifa ya Uhamasishaji Regina alisema kuwa zoezi hilo linaendelea
vizuri licha ya changamoto kadhaa walizokutana nazo katika vituo vya Afya katika
maeneo kadhaa ya wilaya walipopita. Aliwataka wahudumu wa Afya kuendelea
kuhamasisha chanjo ya Uviko 19 sanjari na Afua zingine za mapambano dhidi ya
Korona ili kuendana na dhana nzima ya awamu ya pili ya uhamasishaji kwa
kuwatumia wahudumu wa Afya Ngazi ya jamii. “Niwasihii sana watendaji wa Afya
mliopewa dhamana hii ya upimaji wa chanjo ya Uviko 19 zoezi hili liendane na
Afua zongine ikiwemo uvaaji wa Barakoa utumiaji wa maji tiririka bila kusahau
kuwatumia wahudumu wa Afya ngazi ya jamii kwani wanawajua wananchi na
imethibitika kuwa ndio chachu ya kuongeza idadi ya wapimaji sanajri na viongozi
wa serikali dini na mila”
Home
Unlabelled
WATU 1800 TANGA WANAPATA CHANZO YA UVIKO-19 KWA SIKU
Post A Comment: