Julieth Ngarabali. Chalinze.
Mkoa wa Pwani una uhaba wa magari ya kubebea wagonjwa 18 changamoto ambayo inachangia adha ya usafi kwa wagonjwa hasa wale wa rufaa kutoka katika kituo kimoja kwenda kingine.
Mkuu wa mkoa wa Pwani Abubakar Kunenge amesema mkoa huo unahitaji kuwa na magari ya wagonjwa 38 lakini kwa Sasa yaliyopo ni 22 ambapo kati yake mawili ni mabovu .
Kunenge amesema hayo Desemba 17 alipokua akikabidhi gari moja la wagonjwa (ambulance) litakalotoa huduma katika kituo Cha Afya Kibindu ambacho kipi umbali wa kilomita 126 kutoka makao makuu ya Halmashauri ya Chalinze.
Gari hilo ni la aina ya Landcruiser na kwamba limenunuliwa kwa sh. Mil. 120 fedha za mapato ya ndani ya Halmashauri hiyo.
Mkuu huyo wa mkoa ameipongeza Chalinze kwa kununua gari Hilo kwa mapato yake ya ndani na kubainisha kuwa sababu kubwa ya Serikali kuzianzisha Halmashauri pamoja na kurudisha maamuzi kwa wananchi wenyewe kusogeza huduma kwa jamii ni pamoja na kusaidia Seriakki kutoka huduma.
"Zinatakiwa kila Halmashauri zijiendeshe wenyewe,Sasa kujiendesha ndio Kama haya mnayofanya na mmesema wenyewe kila mwaka mmepanga kupata gari moja na mkiwa na vipaumbele sahihi mnaweza"amesema Kunenge.
Kunenge amesema kwa kupitia mfano huo wa Chalinze ametoa agizo kwa katibu tawala mkoa, wakurugenzi Halmashauri zote Tisa ziweke utaratibu wa kupata magari hayo ya kuhudumia wagonjwa na kuweka miundombinu ya kupata nyumba za watumishi wa idara hiyo.
Aidha magari hayo yawe yanafanyiwa matengenezo Kama ambavyo utaalamu unataka kwa sababu yakiachwa baada ya muda yanachakaa na kuharibika.
"Na magari haya yanatumika unaona kwanza yanaenda kwa Kasi mwendo wake ni wa haraka na ni magari yanayotumika wakati wa dharura na kwa muundo wetu tuna vituo vya afya,zahanati, hospital za wilaya na mpaka za Rufaa za mkoa na Taifa na hii inatokana na aina ya changamoto atakayokutana nayo mwananchi kwa upande wa afya hivyo nii lazima tuwe na magari haya, hivyo nawapongeza Sana Chalinze"amesema
Awali akitoa taarifa ya manunuzi ya gari hilo kwa niaba ya Mkurugenzi mtendaji wa Chalinze Ramdhani Possi,Mganga Mkuu wa Halmashauri hiyo Dr. Allen Mlekwa ameeleza kuwa kwa kipindi cha robo ya Julai hadi Septemba mwaka huu Takwimu za wagonjwa aa rufaa ilikua watu 90.
Dr. Mlekwa amesema huduma ya magari ya wagonjwa ni muhimu kwa sababu ya uwepo wa wagonjwa wa rufaa wanaotokana na matatizo mbalimbali ya uzazi ,ajali za barabarani, mahitaji ya damu na matatizo memgine na kwamba gari hilo litahudumia pia kata zingine za Mbwewe na Kimange
Diwani wa kata ya Kibindu Ramadhan Mkufya amesema gari hilo itakwenda kupunguza adha na hata vifo vya watoto wadogo na wajawazito kwa sababu Sasa uhakika wa kupata usafiri wa rufaa kwa wakati tofauti na awali walikua wakitumia usafiri wa machela, baiskeli na pikipiki .
Mwakilishi wa wananchi wa Kata ya Kibindu Amina Almasi ameishukuru Halmashauri hiyo kuwapa usafiri wa uhaka kwa sababu imewaondolea adha ya kusafiri umbali mrefu zaidi ya kilomita 40 kwenda kufata huduma kituo jirani.
Post A Comment: