Picha ya pamoja baina ya Mhe. Innocent Bashungwa na Sanjay Dutt Viongozi mbalimbali kwenye Sekta Sanaa na wasanii (waliosimama nyuma)


Innocent Bashungwa(kushoto) akimkabidhi zawadi ya Kamusi ya Kiswahili Sanjay Dutt

Mhe. Innocent Bashungwa akizungumza na Waandishi wa Habari

Wasanii mbalimbali waliohudhuria Mkutano wa Sanjay Dutt

*********************************

Na John Mapepele, WUSM

Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo. Mhe Innocent Bashungwa amesema mwigizaji maarufu duniani kutoka nchini India Sanjay Dutt amekubali kuwasaidia Wasanii wa Tanzania katika maeneo ya kuandaa filamu, vifaa na utaalam ili kutangaza utalii wa Tanzania duniani.

Akizungumza kwenye Mkutano wa kumtambulisha Dutt kwa Waandishi wa Habari na wadau mbalimbali wa Sanaa na Filamu nchini leo Novemba 11, 2021 jijini Dar es Salaam. Mhe, Bashungwa amefafanua kuwa Msanii Dutt amekubali kuleta wataalam ambao watashirikikiana na Bodi ya Filamu, Taasisi ya Chuo cha Sanaa Bagamoyo na Kampuni ya Africable katika kuwasaidia wasanii wa Tanzania katika maeneo mbalimbali.

“Ujio wake ni fursa kwa nchi yetu na kunatusaidia kuendeleza safari ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan ya kuitangaza Tanzania kupitia filamu, safari ambayo Mhe. Rais aliianza kupitia maandalizi ya filamu ya Royal Tour” Ameongeza Mhe. Bashungwa

Amesema ujio huu unaashiria kuwa tasnia ya filamu nchini Tanzania, inapitia mabadiliko chanya na makubwa, kiasi kwamba waigizaji wakubwa wa filamu kama Dutt, wanasikia furaha na kutenga muda kutembelea Tanzania na kuwa uwepo wake hapa utakuwa ni fursa kubwa kwa tasnia ya filamu na wadau wote wa filamu nchini.

Aidha, Mhe. Bashungwa ametumia muda huo kumwomba Msanii Sanjay Dutt kutoa vifaa vya kuandaa filamu za kisasa kwa wasanii wasio na uwezo wa kuwa na vifaa hivyo na kwamba vitakuwa vikitunzwa na kusimamiwa na Bodi ya Filamu nchini na Msanii huyo amekubaliana na ombi hilo.

Pia, Mhe. Bashungwa amefafanua kuwa Sanjay Dutt amesema anakusudia kuandaa filamu kubwa ambayo itaisambaza duniani kwa ajili ya kuitangaza Tanzania.

Akizungumza kwenye mkutano huo Msanii Sanjay Dutt amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Mhe, Samia Suluhu Hassan na Waziri Mkuu kwa ukaribisho ambapo ameahidi kuisaidia Tanzania kuwa katika sura ya dunia kwenye tasnia ya filamu.

Pia ametoa wito kwa Serikali kuwa “film academy” ambayo itasaidia kuandaa fani mbalimbali kama uigizaji na muziki ambapo amekubali kuwaleta wataalam kutoka India kuja kufundisha.
Share To:

emmanuel mbatilo

Post A Comment: