Mkurugenzi  Mkuu  wa  Taasisi  ya  Kuzuia  na  Kupambana  na  Rushwa  (TAKUKURU) anawatangazia Watanzania wenye sifa kuomba kuajiriwa katika nafasi za kazi zifuatazo:

1.1    AFISA UCHUNGUZI (NAFASI 200)
1.2   Sifa za Kitaaluma:
Muombaji awe angalau na elimu ya shahada ya kwanza iliyotolewa na chuo kinachotam­bulika na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika fani zozote kati ya hizi: Mambo ya  Kale na Utalii, Sheria, Uhasibu,Teknolojia ya  Habari, Elekitroniki, Misi­tu, Kilimo, Ununuzi, Uchumi na Mipango, Usimamizi wa Rasilimali Watu, Takwimu, Utawala wa Umma/Serikali, Utunzaji wa Kumbukumbu, Usimamizi na Uthamini wa Ardhi, Mafuta  na Gesi,Ukadiriaji wa  Majenzi, Uhandisi wa  Umeme, Uhandisi kati­ka Kemia, Mifugo, Usanifu wa Majengo, Mambo ya anga, Uhandisi wa Mitambo, Uhandisi wa Ujenzi na Uhandisi wa Maji;

2.1    MCHUNGUZI MSAIDIZI (NAFASI 150)
2.2    Sifa za Kitaaluma:
Muombaji awe na cheti cha elimu ya kidato cha nne (CSE) au kidato cha sita (ACSE). astashahada au stashahada ya fani yoyote inayotolewa na Taasisi au chuo kinachotam­bulika na Serikali ya Tanzania, pamoja na fani kama vile ujenzi, ulinzi, udereva, upa­kaji rangi, ufundi magari, vifaa vya muziki, utunzaji wa kumbukumbu , TEHAMA, maendeleo ya jamii, uhazili, menejimenti ya hotel , n .k.

 Mwisho wa kutuma maombi ni - 8th November, 2021 

 👉Kujua zaidi pamoja na kutuma Maombi <<BOFYA HAPA>>

👉Kupata nafasi mbalimbali za kazi Serikalini na mashirika binafsi <<BOFYA HAPA>>
Share To:

Teddy Kilanga

Post A Comment: