Mkuu wa Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA) Jaji Mstaafu  Joseph SindeWarioba akiangalia baadhi ya bidhaa wakati wa ziara yake ya siku moja ya kutembelea chuo hicho jana.
Ziara ya kutembelea miradi mbalimbali ikifanyika.
Hapa akipata maelezo wakati wa ziara hiyo.
Ziara ikiendelea,
Ziara ikiendelea,


Na Mwandishi Wetu, SUA Morogoro


MKUU wa Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA) Jaji Mstaafu  Joseph SindeWarioba amefurahishwa na mafunzo yanayotolewa SUA kwa kushirikiana na PASS (Private Agricultural Support Sector) yanayosaidia vijana kujiajiri na jamii kwa ujumla.

Jaji Warioba ametoa pongezi hizo jana katika ziara yake ya siku mbili Chuoni hapo, akiwa ameambatana na Mwenyekiti wa baraza la Chuo Jaji Othman Chande na makamu mwenyekiti wake Doroth Mwanyika.

“Hawa vijana akitoka hapa watasaidia kuwa walimu kwa j amii inayowazunguka na tayari wanakitu cha kufanya ukweli nimefurahi sana kuona vijana kutoka Mikoa mbalimbali kama Tabora, Mwanza, Kigoma, Rukwa wakipata mafunzo haya” alisema Warioba.

“Mafunzo hayo yatasaidia Taifa letu kwa kiasi kikubwa hususani miaka ijayo katika kukidhi mahitaji ya chakula nakuepukana na balaa la njaa kutokana na ongezeko la watu kwani wakati nchi inapata uhuru tulikuwa Watanzania milioni 9 lakini sasa wamefika milioni 60 hivyo tutarajie ongezeko kubwa la watu na uhitaji mkubwa wa Chakula”. 

Pia amewataka SUA kuongeza elimu kwa upana ili kuwafikia vijana wengi zaidi kwa ni mafunzo hayo tayari yameshaleta mafanikio kwa jamii kupitia vijana waliopita ambao wamepata mafunzo hayo.

Kwaupande wa Makamu Mkuuwa Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA) Prof. Raphael Chibunda alimshukuru Mkuu wa chuo hicho kwa kazi kubwa aliyoifanya katika kipindi cha miaka minne na mafanikio yaliyopatikana.

Profesa Chibunda alisema kuwa wamefanya maboresho makubwa chuoni hapo kwa kuboresha mazingira ya kufundishia na kujifunzia kwa wanafunzi hususani mashamba ya kujifunzia kwa vitendo ili kujifunza kwa vitendo ikiwemo ujenzi wa maabara na ununuzi wa vifaa vya kisasa vya maabara pamoja na ujenzi wa maabara ikiwemo maabara mtambuka ambayo inweza kuchukua wanafunzi 3200 kwa wakati mmoja.

Makamu mkuu wa chuo pia alisema kuwa chuo kimetenga fedha zaidi ya milioni 450 kwa ajili ya kujenga vitalu 100 katika kipindi cha miaka mitatu, ambapo kwa mwaka huu wataanza na vitalu 30 natayari wamepeleka maombi mahususi kwa Tume yaTaifa ya Sayansi naTeknolojia(COSTECH) kwa lengo la kushirikiana kuendeleza wabunifu kwa kujenga vitalu vingi zaidi.

Aidha, ameongeza kuwa tayari milioni 200 imetumika kwa ajili ya upanuzi wa sehemu ya upasuaji na manunuzi ya vifaa vipya kama mashine ya X- Ray Digital, Ultra Sound ya kisasa yenye kuwezesha kuona kama mnyama amepata tatizo kubwa zaidi kwa ndani lakini pia chuo kipo mbioni kununua gari litakalotumika kama kliniki inayotembea ili kuwafikia wafugaji wanaoshindwa kufika kwenye hospital hiyo yaTaifa ya rufaa ya wanyama ili kupatiwa matibabu.

“Nitoe wito kwa wafugaji wa Wanyama katika nchi hii pale wanapoona wamekosa msaada sehemu nyingine basi waitazame Hospitali yetu ya Rufaa ya Taifa ya wanyama kama sehemu ya kupata msaada” alisema Profesa. Chibunda.

Katika ziara hiyo Warioba alitembelea miradi mbalimbali ikiwemo yaTiba ya wanyama na sayansi za afya, miradi ya kilimo kwenye Shamba la mafunzo, maabara mtambuka, Kituoatamizi cha Vijana kilichopo chini ya Shule kuu ya uchumi kilimo na taaluma za biashara, kitengo cha mifugo Magadu, kitengo cha Samaki Magadu na maabara ya sayansi na teknolojia ya chakula.


Share To:

dotto mwaibale

Post A Comment: