Naibu
Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Bw. Msafiri Mbibo
akiongea na Watumishi wa TRA pamoja na watumishi wengine wa baadhi ya
taasisi za Serikali zinazofanya kazi pamoja katika Kituo cha Huduma kwa
Pamoja Mpakani (OSBP) cha Mutukula mkoani Kagera ambapo ni mpakani mwa
Tanzania na Uganda, kuhusu namna ya kushirikiana kwa pamoja na kuwa na
nidhamu katika kazi zao wanapokua mpakani hapo.
Naibu
Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Bw. Msafiri Mbibo
(wa pili kulia) akiongea na kutoa maagizo mbalimbali kwa viongozi wa TRA
katika ofisi ya TRA iliyopo eneo la Kyaka mkoani Kagera wakati
alipofanya ziara yake ya kikazi mkoani hapo kwa ajili ya kusikiliza
changamoto mbalimbali katika mpaka wa Tanzania na Uganda.
Naibu
Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Bw. Msafiri Mbibo
akimsikiliza Katibu Tawala wa Mkoa wa Kagera, Profesa Faustin Kamuzora
(kushoto) wakati alipomtembelea ofisini kwake kwa lengo la kufanya nae
mazungumzo juu ya masuala mbalimbali ya kodi ikiwemo namna bora ya
kuboresha makusanyo ya mapato ya Serikali.
PICHA ZOTE NA TRA
………………………………………………………………
Na. Mwandishi wetu
Mamlaka
ya Mapato Tanzania (TRA), imewataka Maafisa Forodha wa TRA pamoja na
maafisa wa taasisi nyingine za Serikali kuhakikisha kuwa wanahamasisha
matumizi sahihi ya kisheria katika Vituo vya Huduma kwa Pamoja Mpakani
ili watu mbalimbali wanaopita kupitia katika mipaka hiyo waweze
kuhamasika kutumia njia sahihi badala ya njia zisizo rasmi.
Hayo
yamesemwa hivi karibuni na Naibu Kamishna wa TRA, Bw. Msafiri Mbibo
wakati alipofanya ziara yake ya kikazi katika mpaka wa Mutukula
unaounganisha nchi ya Tanzania na Uganda uliopo mkoani Kagera.
Bwana
Mbibo amesema kwamba, lengo la kutaka kuwepo kwa matumizi sahihi ya
sheria hizo katika maeneo ya mipakani ni kuzuia watumiaji kutumia njia
zisizo rasmi ambazo zinaweza kuathiri takwimu za kiuchumi, kuhatarisha
usalama wa nchi na pia uingizaji bidhaa mbazo hazina viwango ambazo
zitaumiza walaji wa ndani na zinaweza kuharibu mahusiano baina ya
Tanzania na nchi za jirani.
“Kuziingiza bidhaa ambazo hazina
viwango nchini kwetu na kupeleka bidhaa ambazo hazina viwango kwa nchi
ambazo ni majirani zetu kutaharibu mahusiano yetu ya kibiashara pindi
wakigundua tunaingiza nchini mwao bidhaa za namna hiyo, hivyo lazima
tusimamie vizuri sheria ili mambo haya yasitokee”, alisema Mbibo.
Ameongeza
kuwa, mpaka wa Mutukula kwa sasa ufanisi wake unaoongezeka mwaka hadi
mwaka ambapo kwa mwaka wa fedha uliopita wa 2020/2021 ulipangiwa lengo
la kukusanya shilingi bilioni 21 na umefanikiwa kukusanya jumla ya
shilingi bilioni 24 ambapo hiyo ni sawa ufanisi wa utendaji wa asilimia
114 ikilinganishwa na mwaka wa fedha wa 2019/2021 malengo yalikua ni
kukusanya shilingi bilioni 18 na zikakusanywa shilingi bilioni 20 na
zaidi.
“Mpaka huu ni wakutegemewa na unafanya vizuri zaidi, na
endapo tutazidi kuongeza huduma au vitendea kazi katika mpaka huu basi
ufanisi huu wa sasa utazidi kuongezeka na tutaweza kuwahudumia wananchi
wa nchi jirani na Watanzania pia”
Aidha, amefafanua kuhusu magari
yaliyopo mpakani hapo kwa kusema kwamba, baadhi ya magari ambayo
hayajakamilisha baadhi ya taratibu ndogo ndogo wahusika huwa wanaitwa
ili waweze kukamilisha taratibu hizo ili waweze kulipa kodi zao na
kuyaondoa, lakini pia kwa wale ambao wameyatelekeza magari yao sheria
inaitaka TRA kutangaza kwa muda fulani ili wahusika wenyewe wajitokeze
na kukamilisha taratibu za kiforodha na endapo hawajafanya hivyo baada
ya siku kadhaa kupita sheria inaitaka pia TRA iyaingize magari hayo
katika mnada ambao mtu atayevutiwa nayo aweze kuyanunua ili kodi ya
Serikali iweze kukombolewa.
“Mnada wa kuuza magari
yaliyotelekezwa tunafanya kwa njia ya mtandao (Online), hivyo mtu yeyote
nchi nzima anaweza kushiriki katika mnada, lakini kuna baadhi ya magari
ya watu ambao ni wakorofi na wamekua wakichezea chesisi namba za magari
na kwa bahati nzuri sheria inamruhusu Kamishna Mkuu wa TRA kuyatoa kwa
namna anavyotaka yeye, basi sisi tunaweza kuyagawa kwa taasisi nyingine
za Serikali lakini hii huwa hatufanyi mara kwa mara”, alisema Mbibo.
Naibu
Kamishna Mkuu wa TRA yuko katika ziara ya kikazi katika mikoa ya Kanda
ya ziwa na lengo la ziara hiyo ni kuona namna ya utendaji kazi wa ofisi
za TRA mipakani ikiwemo kusikiliza changamoto mbalimbali katika ofisi
hizo ili ziweze kutafutiwa ufumbuzi wake na hatimaye makusanyo ya mapato
yazidi kuongezeka na kwenda kuleta maendeleo kwa Taifa.
Post A Comment: