Halmashauri ya Wilaya Uvinza
Na Angela Msimbira UVINZA - KIGOMA
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Ummy Mwalimu aipongeza Halmashauri ya Wilaya ya Uvinza kwa kutekeleza agizo la Serikali ya kutenga asilimia kumi ya Fedha za Maendeleo kwa ajili ya Mikopo ya Wanawake, Vijana na watu wenye ulemavu
Akikabidhi mfano wa hundi kwa Wanawake, Vijana na Watu wenye Ulemavu Waziri Ummy ameziagiza Halmashauri zote nchini kuacha kutoa mikopo midogo midogo kwa kuwa vikundi vingine vina uwezo wa kufanya biashara kubwa na kufanya marejesho kwa wakati na waweze kujikwamua kiuchumi.
Waziri Ummy amesema amevitaka vikundi vyote vya ujasiriamali vinavyopatiwa mikopo kurejesha kwa kuwa mikopo hiyo si hisani bali ni fedha ambazo zinahitajika wananchi wengine kupatiwa mikopo.
Halmashauri ya Wilaya ya Uvinza katika Mwaka wa Fedha wa 2013/2014 hadi 2020/2021 vikundi 64 vya wanawake vimenufaika na mikopo zaidi ya milioni 313, vikundi 39 vya vijana vimenufaika na mikopo ya zaidi ya shilingi 219 na vikundi 8 vya watu wenye ulemavu vimenufaika na mikopo yenye zaidi ya shilingi milioni 51 hivyo kufanya jumla ya mikopo iliyotolewa ni zaidi ya shilingi milioni 583.
Aidha, Jumla ya Mikopo yote iliyotolewa na Halmashauri ya Wilaya ya Uvinza kwa mwaka wa Fedha 2020/2021 ni shilingi milioni 194 ambazo zinajumuisha asilimia 10 ya mapato ya ndani ambayo ni shilingi milioni 124 na fedha za marejesho milioni 70
Post A Comment: