Mkuu
wa Mkoa wa Tabora Balozi Dkt. Batilda Buriani(kulia) akiangalia leo
mmoja ya mahindi ambayo yamezalishwa na Watafiti kutoka Kituo cha
Utafiti wa Kilimo –Tumbi cha Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Tanzania(TARI)
kwa ajili ya mbegu bora. Kushoto ni Kaimu Mkurugenzi wa Kituo cha
Utafiti wa Kilimo –Tumbi Dkt . Emmanuel Mrema
Mkuu
wa Mkoa wa Tabora Balozi Dkt. Batilda Buriani(kushoto) akiangalia leo
kili mbili za mbegu bora ya mahindi yaliyozalishwa na Watafiti kutoka
Kituo cha Utafiti wa Kilimo –Tumbi cha Taasisi ya Utafiti wa Kilimo
Tanzania(TARI) kwa ajili ya mbegu bora. Kulia ni Kaimu Mkurugenzi wa
Kituo cha Utafiti wa Kilimo –Tumbi Dkt . Emmanuel Mrema
Kaimu
Mkurugenzi wa Kituo cha Utafiti wa Kilimo –Tumbi Dkt . Emmanuel
Mrema(kushoto) akimwonyesha leo Mkuu wa Mkoa wa Tabora Balozi Dkt.
Batilda Buriani(kulia) miche ya michikichi ambayo imezalishwa na
Watafiti kutoka Kituo cha Utafiti wa Kilimo –Tumbi cha Taasisi ya
Utafiti wa Kilimo Tanzania(TARI) kwa ajili ya mbegu bora.
Mkuu wa Mkoa wa Tabora Balozi Dkt. Batilda Buriani amewaagiza Wakuu
wa Wilaya kuhakikisha kuwa wanawakamata watu watakaobainika kuchoma
moto na kusababisha uharibifu katika mistu ya kupanda na ile ya asili
katika maeneo mbalimbali.
Hali imekuwa ikisababisha hasara kubwa kwenye mistu na mimea ya Taasisi na watu binafsi.
Balozi
Dkt. Batilda alitoa agizo hilo leo wakati akipokuwa na ziara ya kikazi
katika Kituo cha Utafiti wa Kilimo –Tumbi cha Taasisi ya Utafiti wa
Kilimo Tanzania(TARI) iliyokuwa na lengo la kuwahamasisha kuzalisha kwa
wingi mbegu bora za Alizeti.
Amesema tabia ya uchomaji moto ovyo
katika maeneo yote ya Mkoa wa Tabora kwa kisingizio cha kuandaa mashamba
na wengine kutaka majani mapya yaote kwa ajili ya mifugo haikubaliki.
Balozi
Dkt. Batilda amewataka Wakuu wa Wilaya zote na Watendaji kuhakikisha
wanawakamata na kuchukuliwa hatua kali ili iwe fundisho kwa wenzake
wenye tabia chafu ya kuchoma moto ya kuteketeza mistu na miti
inayoendelea kupandwa.
Amesema ni vema Sheria Ndogo zilizopo zitumikea kuwaadhibu wale wote watakaokamatwa kwa makosa ya kuchoma mistu moto.
Mkuu
huyo wa Mkoa wa Tabora alilazimika kutoa agizo hilo haraka mara baada
ya watu wasiofahamika kuchoma moto miti iliyokuwa imepanda katika
barabara inayoelekea Chuo cha Musoma Utalii, eneo la Cheyo na eneo
Malolo mjini Tabora.
Alisema kuwa haiwezekana mtu anachoma halafu
viongozi wa mitaa au vitongoji wanasema hawawajui na kuongeza kuwa huo
ni uzembe wa hali ya juu.
Bw. Mwanri alisema kuwa yeye atapambana
na Mkuu wa Wilaya ambaye uharibifu utakea katika eneo lake na kushindwa
kuwasimamia wa chini ili kukomesha tabia hiyo.
“Haiwezekani moto
unachomwa katika maeneo yenu , mnashindwa kutambua mtu aliyeendesha
hujuma hiyo…lazima panapotokea moto wahusika wasakwe na kuadhibu kwa
mujibu wa Sheria” amesisitiza Mkuu huyo wa Mkoa.
Amesema kuwa
inasikitisha kuona wananchi na wadau mbalimbali wamejitokeza kupanda
miti kwa wingi kisha wanatokea wachache wanachoma moto kwa kisingizio
cha kusafisha mazingira au kutaka majani mapya kwa ajili ya mifugo.
Balozi
Dkt. Batilda amesema wananchi lazima watambue miti ya asili na ile ya
kupandwa ni kwa ajili ya faida ya wote na kuwaomba kusaidia kuwafichua
watu wote wanaochoma miti kwa visingizio ambavyo sio vya msingi.
Kaimu
Mkurugenzi wa Kituo cha Utafiti wa Kilimo –Tumbi Dkt . Emmanuel Mrema
amesema uchomaji wa moto ovyo katika eneo la Kituo umekuwa
ukiwasababishia hasara kubwa katika mimea mbalimbali wanaendeshea
utafiti.
Amesema katika siku za hivi karibu wamepata hasara ya
kupoteza miche ya miti ya miembe ipatayo elfu 6 kutokana na watu
wasiojulikana kuchoma moto.
Dtk. Mrema amemuomba Mkuu huyo wa Mkoa kusaidia katika utatuzi wa tatizo hilo amabalo limekuwa sugu Mkoani humo.
Post A Comment: