Maafisa
wa Banki ya CRDB na Mfuko wa bima ya Afya NHIF wakiwa katika picha ya
pamoja (kushoto) ni Meneja wa kanda ya Kati Banki ya CRDB Chabu
Mishwaro,(wapili kutoka kushoto) Kaimu Meneja mkuu wa Banki ya CRDB,
Wilson Mnzava (watatu kutoka kushoto) ni Mkurugenzi wa huduma za
uanachama (NHIF ) Hipoliti Lello(wa mwisho kulia) ni Neema Matiga Afisa
masoko huduma kwa wateja NHIF.
Zoezi
la utiaji saini ya makubalino ya Bima ya Afya kwa wakulima likiendelea
baina ya Banki ya CRDB,NHIF, PAMOJA na AMCOS za wakulima wa miwa
Wilayani Kilombero (kushoto) ni Kaimu Meneja mkuu wa Banki ya CRDB,
Wilson Mnzava (kulia) kaimu Mkurugenzi wa huduma za uanachama (NHIF)
Hipoliti Lello
Kushoto
ni Kaimu Meneja mkuu wa Banki ya CRDB, Wilson Mnzava akiwa katika picha
ya pamoja na katibu wa chama cha ushirika cha Katurukila baada ya
utiaji saini hati ya makubaliano ya Bima ya afya kwa wakulima wa miwa
Wilayani Kilombero baina ya Banki ya CRDB,NHIF, na AMCOS.
Kaimu
Meneja mkuu wa Banki ya CRDB, Wilson Mnzava akizungumza na viongozi wa
vyama vya ushirika (AMCOS) Wilaya ya Kilombero katika hafla ya utiaji
saini ya makubaliano ya Bima ya afya kwa wakulima baina ya Banki ya
CRDB,NHIF, na AMCOS za wakulima wa miwa.
Katika kuhakikisha wakulima wanakuwa na uhakika wa matibabu pindi
wanapopatwa na maradhi, banki ya CRDB kwa kushirikiana na Mfuko wa Taifa
Bima ya Afya (NHIF) wameanzisha utaratibu wa kuwawezesha wanachama wa
AMCOS na familia zao kupata matibabu hospitalini kwa kutumia Bima ya
afya kwa gharama nafuu mkoani hapa.
Akizungmza wakati wa utiaji
saini makubaliano baina ya Banki ya CRDB, Mfuko wa Taifa Bima ya Afya
(NHIF) na viongozi wa AMCOS za wakulima wa Miwa wa Wilaya ya Kilombero,
Kaimu Meneja mkuu wa Banki ya CRDB, Wilson Mnzava Amesema CRDB inatambua
changamoto za wakulima hususani katika Afya ndio maana imekuja na
mkopo wa Bima ya Afya kwa wanaushirika, ambapo mkopo huo utatolewa bila
ya Riba.
Mnzava amesema kuwa wanufaika wa Ushirika Afya ni
wanachama wa AMCOS zote Tanzania pamoja na Familia zao ambapo watalipa
shilingi 76,800 kwa mtu mzima na 50,400 kwa mtoto itakayowawezesha
kupata matibabu Tanzania nzima ndani ya miezi 12 (mwaka mmoja).
“CRDB
tunajua umuhimu wa miwa na sukari hapa nchini ndio maana tumewaleta
ushirika afya ili muwe na uhakika wa afya zenu pamoja na matibabu ili
muendelea kulima na kuongeza uzalishaji wa miwa”. Alisema Mnzava.
Kwa
upande wake Kaimu Mkurugenzi huduma za wanachma kutoka Mfuko wa Taifa
wa Bima ya Afya, Hipoliti Lello alisema kuwa upatikana wa Bima hiyo
utawasaidia kuondoa usumbufu na michango ya matibabu isiyokuwa rasmi
iliyokuwa ikijitokeza kwenye vyama vya ushirika hasa inapotokea mmoja wa
wanachama akipatwa na maradhi.
“Ushirika Afya itawapunguzia
michango midogo midogo mliokuwa mnachangishana kwenye vyama vyenu
ikitokea mwezenu anaumwa au anauguliwa”. Alisema Lello.
Aliongeza
kuwa kuna yale maswala ya njoo univunie mimi kwanza mtoto wangu anaumwa
yataisha kama wanachama watajiunga kwenye Ushirika Afya, huku
akiwahakikishia kuwa NHIF itakuwa mstari wa mbele katika kuhakikisha
wanapata huduma bora.
Hata hivyo Kaimu Meneja wa Banki ya CRDB,
Wilson Mnzava amesema kuwa Banki hiyo itaendelea kushrikina na wakulima,
ambapo kwa mwaka wa Fedha wa 2021 Banki imetoa mikopo kwenye sekta ya
kilimo ya shilingi Bilioni 735 sawa na asilimia 43 ya mikopo yote
iliyotolewa na CRDB nchini.
Ameongeza kuwa Kati ya mikopo hiyo
shilingi Bilioni 494 zimeelekezwa kwenye mazao makuu ya kimkakati na
kusaidia zaidi ya AMCOS 472 kupata mikopo kwa ajili ya kuongeza tija
katika uzalishaji kwenye kilimo.
Aidha mikopo hiyo imetolewa
kwenye ununuzi wa pembejeo, Ujenzi wa Maghala na viwanda vya kuchakata
mazao vitaavyo saidia kuongeza mnyororo wa thamani kwenye mazao
yanayozalishwa hapa nchini.
Sambamba na hayo ametoa wito kwa
wakulima wadogo kujiunga na Banki ya CRDB ili waweze kujikwamua kiuchumi
na kupata mazingira wezeshi katika uzalishaji wa mzao.
Keneth
Shemdoe ni mrajisi msaidizi wa vyama vya ushirika Mkoa wa Morogoro
amevitaka vyama hivyo kuacha tabia ya kuvuruga utaratibu wa uvunaji wa
miwa kwa sababu ya kukosa fedha za matibabu badala yake watumie bima za
Afya kwenye matibabu.
Nae Makamu Mwenyekiti wa Miwa AMCOS Masoud
Mkinga akizungumza kwa niaba ya viongozi wa wakulima wa miwa amesema
wao kama viongozi wapo tayari kutoa elimu kwa wakulima wengine juu ya
umuhimu wa Ushrika afya na kuwataka wachangamkie fursa hiyo adhimu kwao.
Hafla ya utiaji saini hati ya makubaliano ya bima ya Afya kwa
wakulima wa miwa baina ya Banki ya CRDB, NHIF, na AMCOS za wakulim wa
miwa wilayani kilombero imehudhuliwa na viongozi mbalimbali wa Serikali
na AMCOS.
Post A Comment: