WAZIRI wa Maji Jumaa Aweso akisistiza jambo wakati wa ziara hiyo kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Mwanza John Mongela
WAZIRI wa Maji Jumaa Aweso akisistiza jambo wakati wa ziara yake
WAZIRI wa Maji Jumaa Aweso katikati akiwa na Mkuu wa Mkoa wa Mwanzo John Mongela kushoto wakati wa ziara yake mkoani humo 
WAZIRI wa Maji Jumaa Aweso akishuka kwenye tenki mara baada ya kulikagua





NA MWANDISHI WETU, MWANZA.

WAZIRI wa Maji Jumaa Aweso amewataka mameneja wa Mamlaka za Maji nchini kuwaeleza Mameneja Masoko wenu wasiwape wasoma mita malengo ya makubwa ya makusanyo yasiyo halisia ambayo hayatekelezeki na yanawaumiza wananchi na kusababisha malalamiko.

Badala yake aliwata mameneja hao wasimamie kikamilifu zoezi la usomaji wa mita za maji ziwe halisia ili kuepuka kuwabambikia wananchi bili za maji.

Aweso alisema hayo leo wakati wa ziara yake mkoani Mwanza ambapo alisema ni haki ya mwananchi kupatiwa huduma ya maji naye weajibu wake kulipa bili za maji lakini zisiwe bambikizi kwao.

Aliyasema hayo wakati akiwa kwenye mradi wa Maji wa Buswelo ambapo aliwaelekeza Mameneja Masoko hao kuhakikisha wanasimamia kikamilifu suala za usomaji wa mita za maji ili kuepusha malalamiko.

“Baadhi ya maeneo wananchi hulkalamikia bili za pemaji naomnba wakurugenzi waelekezei mameneja masoko wenu wasiwape malengo makubwa ya makusanyo wasoma mita yasiyohalisia maana leo unampa malengo makubwa ya makusanyo hafikii atakachokifanya atambamikizia bili mwananchi ili akuridhishe hivyo wekeni makarido halisia”Alisema .

Hata hivyo aliwataka wahakikisha wanaweka makadirio halisia juu ya kukusanya mapato ili wananchi waweze kulipa bili stahiki ambazo sio kichefuchefu.

Katika hatua nyengine amewataka Wakala wa Maji Vijijini Ruwasa na Mamlaka ya Maji ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Mwanza kuhakikisha tenki lililopo eneo la Igogwe na kahama tokea 2017 ambalo hakuna usambaji wowote wa huduma maji wajipange miradi hiyo waende kuikamilisha na wananchi wapate huduma za maji.
Share To:

TANGA RAHA BLOG

Post A Comment: