Spika wa Bunge Job Ndugai akizungumza na wananchi, viongozi wa Wilaya ya Kongwa, na wafanyakazi wa Kampuni ya  Bia ya Serengeti (SBL)  katika Shule ya Sekondari ya Laikala wakati wa shughuli ya upandaji wa miti iliyoandaliwa na SBL jana.  Kulia ni Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya  Bia ya Serengeti (SBL), Mark Ocitti,

Mkurugenzi Mkuu wa SBL, Mark Ocitti, akizungumza  kabla ya kuanza shughuli hiyo ya upandaji wa miti.
Spika wa Bunge Job Ndugai, akishiriki kupanda miti katika Shule ya Sekondari ya Laikala.
Spika wa Bunge Job Ndugai (kushoto) na Mkurugenzi Mkuu wa SBL,  Mark Ocitti wakiwa wameshika miti ikiwa ni ishara ya kuhamasisha wadau wengine kushiriki shughuli ya upandaji miti.

Mkurugenzi Mkuu wa SBL Mark Ocitti, akishiriki kupanda miti katika Shule ya Sekondari ya Ndurugumi iliyopo wilayani humo.

Wafanyakazi wa SBL wakiwa katika picha ya pamoja baada ya kukamilika kwa shughuli hiyo ya upandaji wa miti.

 Spika wa Bunge Job Ndugai (kulia) akizungumza na viongozi wa Kampuni ya  Bia ya Serengeti (SBL) baada ya kukamilika kwa shughuli hiyo ya upandaji miti.


Na Mwandishi Wetu, Dodoma


KAMPUNI ya Bia ya Serengeti (SBL),  imeungana na viongozi pamoja na wananchi wa wilaya ya Kongwa mkoani Dodoma katika shughuli ya upandaji miti ikiwa ni sehemu ya mpango wa kampuni hiyo wa kutunza mazingira.

Mgeni rasmi aliku wa Spika wa Bunge Job Ndugai, viongozi wa wilayaya Kongwa, na wabunge ni badhi ya wageni walioshiriki katika zoezi hilo la upandaji miti lililoandaliwa na SBL.

Akiongea wakati wa zoezi hilo, Mkurugenzi Mkuu wa SBL, Mark Ocitti,  alisema upandaji miti katika wilaya ya Kongwa ni sehemu ya mkakati endelevu wa kampuni hiyo unaolenga kupanda maelfu ya miti sehemu mbalimbali hapa nchini. 

Mkurugenzi huyo alisema mwaka 2019 kampuni ya SBL ilipanda miti katika wilaya za Same Pamoja na Moshi ilikuongeza uoto katika maeneo ya jirani na mlima Kilimanjaro.

“SBL inachukulia miti kama sehemu muhimu sana yamazingira. Miti inasaidia kuhifadhi vyanzo vya maji, ni makazi kwa wanyama na wadudu mbalimbali, ina vutahewa chafu ya kaboni na kuzalisha hewa safi na pia miti ni chanzo cha dawa. 

Biashara yetu na jamii kwa ujumla ni sehemu ya mazingira na hii itunafanya kuwa jukumu letu sote kuyalinda na kuyatunza mazingira,” alisema Ocitti. 

Upandaji miti wa SBL unakuja katika kipindi ambacho dunia inahangaika kupunguza uzalishaji ya hewa ukaa ilikupunguza athari za mabadiliko ya tabia nchi pamoja na kuyalinda mazingira kwa manufaa ya vizazi vya sasa na vijavyo.

Kwa upande wake Mhe Job Ndugai aliishukuru kampuniya SBL kwa kuunga mkono jitihada za upandaji miti na kuongeza kuwa miti inanafasi ya kipikee kwa maisha ya watu na kusistiza kuwabila miti hakuna maisha.

Mhe Job Ndugai alisema ukataji miti holela ni moja kati ya sababu za mabadiliko ya tabiaya nchi ambayo yamesababisha changamoto nyingi zinazomkabili binadamu ikiwa ni pamoja na athari kwenye uzalishaji wa chakula, upatikanaji wa maji, afya ya viumbe mbalimbali ikiwa ni pamoja na binadamu.

Ni matumaini yangu kuwa zoezi hili la upandaji miti litawavuta wakazi wengi wa Kongwa na maeneo mengine nchini kupanda miti kila wanapopata fursa. Pia napenda kuzikumbusha taasisi na makampuni mbalimbali kufikiria juu ya dunia yetu na kuchukua hatua za kuilinda na kuitunza,” aliongeza Mhe Spika.

Katibu Mkuu Mtendaji wa Taasisi ya Habari Development Association (THDA),  Benard James alisema shughuli hiyo  imeandaliwa na taasisi hiyo na kuwa wamepanda miti 3000 wakiongozwa na Spika wa Bunge Job Ndugai kwa ufadhili wa SBL lengo likiwa ni kuikijanisha Dodoma na kuhamasisha jamii  kupanda miti na kuikuza kwa kuzingatia Dodoma ndio makao makuu ya nchi na ni eneo kame baada ya misitu mingi kuvamiwa na kukatwa kwa ajili ya mkaa, mbao na kuni.

James aliongeza kuwa miti hiyo imepandwa katika shule tatu wilayani humo ambazo amezitaja kuwa ni Shule ya Sekondari ya Ndurugumi, Laikala na Mwang'weta. 

Share To:

Post A Comment: