Aliyekuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Hayati John Joseph Magufuli (kulia,) akiwa na mama yake mzazi Suzana Magufuli  ambaye ni mgonjwa hadi sasa  na Serikali imehaidi kusimamia matibabu yake hadi atakaporejea katika hali yake ya kawaida.

Na Leandra Gabriel, Dar es Salaam

WAZIRI Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Kassim Majaliwa amesema mama mzazi wa Hayati Rais Dkt.John Joseph Magufuli bado ni mgonjwa na yupo kitandani kwa miaka miwili sasa na Serikali itahakikisha madaktari wanamtibu hadi atakaporejea katika hali yake ya kawaida.

Akizungumza leo Wilayani Chato mkoani Geita wakati wa Ibada ya mazishi ya aliyekuwa Rais wa awamu ya tano Hayati JPM, Majaliwa amesema hadi sasa mama mzazi wa Hayati Rais Magufuli yupo kitandani akiendelea na matibabu.

"Nimeongea na Mh. Rais kuhusiana na jambo hili  na tutahakikisha madaktari wanamtibu bibi yetu hadi pale atakaporejea katika hali yake ya kawaida." Amesema Majaliwa.

Waziri Majaliwa msiba huo umewagusa watanzania wengi na kama Taifa hawana budi kumshukuru Mungu na kumuenzi Hayati JPM kwa vitendo.

Pia amewashukuru wasanii, waandishi wa habari na watanzania kwa ushirikiano wanaoonesha katika kipindi chote cha maombolezo.

Share To:

Post A Comment: