Katibu wa Chama cha Wachumi Kilimo Tanzania (AGREST) Dkt. Betty Waized akitoa salamu za Chama hicho na malengo ya mkutano huo kabla ya kumkaribisha Mgeni rasmi kwaajili ya ufunguzi. 
Waziri Mkuu Mstaafu wa Tanzania Mizengo Pinda akitoa nasaha zake mbele ya Wataalamu hao wa Uchumi Kilimo wakati akifungua rasmi mkutano huo wa 12 wa Kisayansi wa  Chama hicho mjini Dodoma.
Profesa. Aida Isinika akimkabidhi Pinda zawadi maalumu iliyotolewa na chama hicho kama kumbukumbu.
Mkutano ukiendelea.
Mkutano ukiendelea.
Mkutano ukiendelea.
Wanachama wa AGREST na Mgeni rasmi Mizengo Pinda mara baada ya ufunguzi wa mkutano huo wa 12 wa kisayansi.

Washiriki wa mkutano wakifuatilia hotuba za ufunguzi.
Washiriki wa mkutano wakifuatilia hotuba za ufunguzi. 


Na Calvin Gwabara, Dodoma


Imeelezwa kuwa Tanzania haitaweza kuondoa umasikini wala kupiga kasi ya Kim aendelee kwa Wananchi wake endapo swala la Kilimo Bora na cha kisasa halitapewa kipaumbele na Serikali, Watafiti na wadau wengine wa kilimo.

Hayo yamesemwa na Waziri Mkuu Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Mizengo Pinda wakati akifungua Kongamano la Kisayansi la Chama cha Wachumi Kilimo Tanzania (AGREST) lenye Mada kuu isemayo “Kuondoa vizuizi katika biashara ili kushanirisha biashara ya mazao ya Kilimo na mifumo ya chakula baina ya nchi za Afrika”lililofanyika mkoani Dodoma.

Pinda alisema pamoja na mabadiliko yanayoendelea katika shughuli za kiuchumi za watanzania katika maeneo ya vijijini zaidi ya asilimia 60 ya wananchi wanategemea kilimo lakini ni ukweli kwamba  wanaotegemea kilimo bado ni masikini kwa kiasi kikubwa wanategemea mazao ya chakula kama chanzo muhimu cha kipato cha kaya.

“ Juhudi za nchi  yetu za kuendeleza viwanda kwa kiasi kikubwa zinategemea uzalishaji na biashara ya mazao ya kilimo na hasa mazao ya chakula hivyo mada kuu ya kongamano hili ni muhimu sana katika ustawi wa Wananchi wengi ambao wanategemea moja kwa moja Kilimo cha mazao hayo au wale wanaofanya shughuli katika mnyororo wa thamani wa mazao hayo”  alisisitiza Pinda.

Alisema kuwa taarifa zilizopo zinaonyesha kuwa biashara ya mazao ya kilimo baina ya nchi za Afrika kwa sasa ni chini ya asilimia 20 huku ikikadiriwa kuwa tunakosa mapato Dola bilioni 30 kwa Mwaka kwa kutoboresha mazingira ya Biashara yetu ya Kilimo baina yetu wakati maeneo mengine nje ya Vara la Afrika yakifanya vizuri.

Pinda aliongeza kuwa kwa muongo mmoja na nusu Tanzania imeweza kupanda kutoka nafasi ya 10 Mwaka 2007 hadi kufikia nafasi ya 7 kama muuzaji mkubwa wa mazao ya kilimo ndani ya Afrika na kwamba muelekeo huo ni mzuri ingawa kuna mengi ya kufanya hasa ukilinganisha na uwezo na rasilimali zilizopo nchini.

Hata hivyo waziri mkuu huyo mstaafu alibainisha kuwa tafiti zinaonyesha kuwa

vikwazo visivyo kodi vinakwamisha zaidi biashara kuliko vikwazo vya kikosi na kwamba taarifa zilizopo zinaonyesha kuwa vikwazo visivyo kodi ni tatizo kubwa San katika kufanya biashara baina ya nchi za Afrika kuliko nchi zilizo nje ya Afrika.

“ Ni imani yangu kuwa katika kongamano hili mtajadili namna bora ya kutoka katika mzunguko au mkwamo huu” alisema Pinda.

Hata hivyo  Pinda alisema kwakuwa kilimo bodo kinaajiri watu wengi kuimarika kwa bishara ya mazao ya Kilimo kutaimarisha ajira za watu wengi na kufanya Kilimo kiwe ni ajira yenye kuvutia hasa vijana kwani benki ya dunia inakadiria hadi kufikia mwaka 2022 kutakuwa na watu bilioni 1.6 wanaohitaji ajira na Afrika pekee ni vijana milioni 25 wanaohitaji ajira kila mwaka.


“ Mimi binafsi ni muumuni wa kuwa maendeleo ya jamii ya jamii yoyote yanategemea sana matumizi ya taarifa za kutafiti ambazo zitasaidia wafanya maamuzi kuchukua Mrengo sahihi hivyo naamini Kongamano hili la wana AGREST mtajadili namna bora ya kutoka katika mzunguko huu ili Tanzania na Afrika kwa ujumla ziweze kunufaika katika biashara ya mazao na bidhaa za chakula” alisema Pinda.

Aliongeza kuwa Serikali ya CCM inayoongozwa na Rais John Magufuli ina nia njema kabisa ya kuhakikisha kuwa Tanzania inashirikiana na wadau wote katika kuhakikisha Kilimo kinaendelea na kuondoa changamoto zinazojitokeza lakini lazima wajue kwamba Serikali pekee haiwezi kuziondoa bila wataalamu kushirikiana na Serikali.

“ Nikipongeze Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA) kupitia wataalamu wake wabobevu na mahiri Kwani tunashuhudia kazi zinazofanywa na nanyi na Taasisi zingine katika kukuza shughuli za utafiti na ubunifu hapa nchini” alipongeza Pinda.

Awali akizungumza kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi katibu wa chama hicho Dkt. Betty Waized  alisema kuwa lengo kuu la AGREST ni kusaidia kuchochea maendeleo na matumizi ya Elimu ya Uchumi Kilimo na biashara nchini Tanzania na mikutano hiyo ndio njia mojawapo ya kufikia lengo hilo ni kupitia mikutano hiyo ya kisayansi ambayo wanajadili na kubadilishana mambo muhimu ya uchumi kilimo na kusambaza kwa jamii kubwa zaidi.

Alisema mkutano huu wa 12 kisayansi wa AGREST ni fursa nzuri ya maandalizi ya mijadala  mkutano wa Mifumo ya chakula unaotarajiwa kufanyika mwaka 2021 ambao unalenga kuboresha mbinu za mifumo ya hakika hapa nchini.

“ Tanzania imeingia kwenye uchumi wa kati na  lengo ni ifikapo mwaka 2025 tunahitaji kampuni za kibiashara za kushindana ambazo zitakazofanya kazi kibunifu kwa mifumo ya chakula ambayo inafanya kazi kwa wote” alisema Dkt. Waized.

Alibainisha kuwa mkutano huo wa kisayansi pamoja na mambo mengine unalenga kujibu maswali ya aina gani ya mifumo ya sera inahitajika kusukuma mfumo endelevu wa chakula kwenye bara letu hasa Tanzania.

Katibu huyo wa AGERST alisema mkutano huo umevutia washiriki 80 kutoka sehemu mbalimbali za Tanzania wakiwakilisha wanataaluma, watafiti, maafisa wa Serikali, mashirika yasiyo ya kiserikali na washiriki binafsi ambapo zaidi ya tafiti za kisayansi 30 zitawasilishwa.

“ Mkutano huu pia unawapa nafasi  wanasayansi  wachanga kupata uzoefu namna ya kuandaa na kuwasilisha tafiti zao za kisayansi” alisema Waized.

Katika mkutano huo wanachama hao walimpatia Pinda zawadi mbalimbali ikiwemo Kinyago cha mnyama Tembo pamoja vitenge kwa ajili yake na mke wake lakini pia AGREST walitoa zawadi kwa mwana AGREST mkongwe kwenye chama chao zawadi ambayo ilikwenda kwa Profesa, Aida Isinika kutoka Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA).


Reply, Reply All or Forward
Share To:

Post A Comment: