Kaimu Afisa Vijana Mkoa wa Singida, Frederick Ndahani, akikabidhi vyeti  katika Mahafali ya Elimu ya Awali ambapo alimwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt.Rehema Nchimbi jana.
Kaimu Afisa Vijana Mkoa wa Singida, Frederick Ndahani, akikabidhi vyeti.
Mtoto akionesha cheti baada ya kukabidhiwa.
Mkuu wa Shule hiyo Sister Malietha, akisoma risara katika mahafali hayo.
Picha ya pamoja na mgeni rasmi.
Kaimu Afisa Vijana Mkoa wa Singida, Frederick Ndahani, akihutubia katika mahafali hayo.
 


Na Dotto Mwaibale, Singida


KAIMU Afisa Vijana Mkoa wa Singida, Frederick Ndahani amewataka wazazi na walezi kujenga tabia ya kuwapa watoto wao mlo kamili  badala ya chipsi.

Ndahani alitoa ombi hilo jana katika mahafali ya Elimu ya Awali ambapo alimwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt.Rehema Nchimbi.

"Nawaombeni wazazi na walezi waleeni watoto katika maadili mema, mkizingatia mlo kamili  kuliko kuwapa chipsi" alisema Ndahani.

Aidha Ndahani aliwaambia wazazi hao wajenge tabia ya kuwashirikisha watoto hao katika michezo mbalimbali kwani inawajenga kiakili na kiafya.

Akizungumza suala la matumizi ya TV kwa watoto aliwaambia wazazi hao wawe wakiwatafutia vipindi vya kuwajenga watoto badala ya kuangalia  katuni zinazofundisha tabia mbaya ikiwemo wizi,ukorofi,ugaidi, uchoyo na hata ngono.

" Kuweni makini na hizi katuni ambazo hazina maadili kwa watoto ni bora watoto waangalie katuni zetu za kitanzania zilizodhibitishwa na  Taasisi ya Elimu Tanzania na si hizo za nje ambazo hazina maadili ya kwetu" alisema Ndahani.

Ndahani aliwaomba wazazi hao kuwajenga watoto wao katika uzalendo na kupenda Taifa na wazazi wao.

 Akizungumzia tabia za  watoto waliokosa maadili alisema katika baadhi ya familia  wamekuwa wakiwaendesha wazazi wao kwa kupanga kila kitu na kipi akifanye na kipi asikifanye huku wazazi wakiwaangalia tu.

Mkuu wa Shule hiyo Sister Malietha aliwaomba wazazi hasa wakina baba kujenga tabia ya kukagua kazi za shuleni za watoto wao badala ya kuwaachia wakina mama pekee kwani malezi ya mtoto lazima yawashirikishe wazazi wote.

Share To:

Post A Comment: