DODOMA:

Bodi ya Nishati Vijijini (REB) katika kikao kilichofanyika Desemba 20, 2020 imemteua Mhandisi Amos William Maganga kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kuanzia tarehe 16 Desemba 2020 kwa mujibu wa kifungu cha 25(1) cha Sheria Namba 8 ya Nishati Vijijini ya mwaka 2005.

Kabla ya uteuzi huu, Mhandisi Maganga alikuwa Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa REA. Mhandisi Maganga ana uzoefu wa zaidi ya miaka 20 katika sekta ya nishati. Aidha, ameshika nyadhifa mbalimbali toka alipokua ameajiriwa na Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO).

Bodi inaomba ushirikiano kutoka kwa wadau wote ili kumuwezesha Mhandisi Maganga kufanikisha utekelezaji wa majukumu ya Wakala.

Kind regards Alex Mathias Sonna Chief Editor Fullshangwe Blog Email:alexsonna915@gmail.com Cellphone:+255653257072 Twitter:@ALEXSonna Instagram:@sonnaalex
Share To:

TANGA RAHA BLOG

Post A Comment: