Na Heri Shaaban


MBUNGE wa Jimbo la Ilala Mussa Zungu Leo ametatua kero ya kufunga Barabara Mtaa wa Maliki Upanga Wilayani Ilala.


Akizungumza wakati wa kutatua kero hiyo Zungu alisema kufungwa kwa barabara hiyo kumekwamisha shughuli za uzalishaji kiuchumi kutokana na Barabara hiyo kubwa inaunganisha mawasiliano Muhimbili ambapo kwa sasa magari yanazunguka umbali mrefu.


Katika ziara hiyo Mbunge wa Ilala Zungu  aliongozana na Mkurugenzi wa Manispaa ya Ilala, Jumanne Shauri, Wataalam WA TARURA na Mhandisi wa manispaa ya Ilala.


"Mkandarasi wa ujenzi wa Dawasa miundombinu ya DAWASA alifunga barabara hii ya maliki mda mrefu tunaomba uharakishe ujenzi Barabara iweze kutumika " alisema Zungu. 



Zungu alisema kufungwa kwa Barabara hiyo kumepelekea wafanyabiashara kukosa wateja wao wa kila siku


Zungu alimpongeza Mkurugenzi wa manispaa ya Ilala  kwa kutatua kero hiyo ambapo Mkurugenzi wa Ilala ametoa siku tatu Mkandarasi wa miuondombinu ya DAWASA kampuni  ya BUCICO  awe amefungua njia.


Kwa upande wake Mkurugenzi wa Manispaa ya Ilala Jumanne Shauri amezitaka Kampuni za ujenzi pindi wanapoomba tenda mbalimbali kuzingatia utaratibu na sheria za ujenzi.


Katika ziara hiyo Mbunge   Musa Zungu aliongozana na Watalaam wa TARURA ,Mhandisi wa manispaa ya Ilala na Meya wa Ilala Omary Kumbilamoto 


Mkandarasi wa miundombinu ya DAWASA kampuni ya BUCICO Yuda Maseru alisema Jumatano Desemba 30/2020 Barabara ya Mtaa Maliki iitafunguliwa. 


Mwisho

Share To:

msumbanews

Post A Comment: