Na. Angela Msimbira SONGEA
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Selemani Jafo ameridhishwa na utekelezaji wa Miradi ya maendeleo katika Halmashauri ya Manispaa ya Songea, Mkoani Ruvuma
Akikagua miradi ya maendeleo leo katika Halmashauri ya Wilaya ya Manispaa ya Songea Mkoani Waziri Jafo amesema miradi iliyotekelezwa katika Halmashauri hiyo imesimamiwa kwa weledi na viwango vinavyohitajika na Serikali
“Nimeridhishwa na miradi ya maendeleo inayotekelezwa na Halmashauri ya Manispaa ya Songea kwa kuwa imesimamiwa kwa weledi mkubwa na imejengwa kwa viwango ninavyoridhisha,” ameseisistiza waziri Jafo
Amewaagiza viongozi wa Mkoa wa Ruvuma kuhakikisha wanaimarisha ulinzi na kutunza miundombinu hiyo iliyojengwa kwa gharama kubwa ili miundombinu hiyo idumu kwa muda mrefu.
Akifafanua zaidi wakati akiongea na wanachi wa Kata ya Majengo
Waziri Jafo amesema Mji wa Songea kipindi cha nyuma kulikuwa na miundombinu mibovu , hata hivyo Serikali ya awamu ya awamu ya Tano iliweza kujenga barabara kwa kiwango cha lami katika manispaa, Miji , majiji na Halmashauri.
Amesema kuwa Ofisi ya Rais Tamisemi inaendelea kufanya tathmini ya miradi ambayo itaweza kutekelezwa katika kipindi kingine cha miaka mitano, hivyo ujenzi mwingine wa miundombinu utafanyika ambapo kwa sasa kuna mpango wa kuboresha miundombinu katika miji 45
Aidha Waziri Jafo ametembelea stendi ya mabasi uliogharimu kiasi cha shilingi bilioni 6.887 machinjio ya kisasa pamoja na barabara yenye urefu wa kilometa 10 zilizojengwa kwa gharama ya shilingi bilioni 13.548 katika Halmashauri ya Manispaa ya Songea.
Post A Comment: