Job Ndugai amechaguliwa kuwa Spika wa Bunge la 12 la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Uchaguzi wa Spika, umefanyika leo Jumanne tarehe 10 Novemba 2020 bungeni jijini Dodoma katika Kikao cha kwanza, Mkutano wa kwanza wa Bunge la 12.

Mkutano huo wa uchaguzi, umesimamiwa na Mwenyekiti wa muda, William Lukuvi ambaye ni mbunge mteule wa Ismani kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Akitangaza matokeo ya uchaguzi huo, Katibu wa Bunge, Stephen Kagaigai amesema, kura 345 zilipigwa, na Ndugai ameshinda kwa kupata kura 344 huku kura moja ya hapana, hivyo kuibuka kwa ushindi wa asilimia 99.7.

Baada ya kumaliza kutangazwa matokeo hayo, Ndugai aliapishwa na Katibu wa Bunge, Stephen Kagaigai.

Share To:

msumbanews

Post A Comment: