Dkt. Devotha Kilave Mtafiti akiwasilisha matokeo ya utafiti wa Kilimo Shadidi cha Mpunga mbele ya waandishi wa habari.
Waandishi wa habari kutoka vyombo mbalimbali vya habari nchini wakifuatilia uwasilishwaji wa matokeo hayo ya utafiti ili wayafikishe kwa jamii.
Waandishi wa habari wakochukua vipeperushi na machapisho mbalimbali ya matokeo ya Tafiti zilizofanhwa na Mradi wa APRA Tanzania.

Mkuu wa Mradi wa APRA Tanzania Profesa. Aida Isinika akichangia neno kwenye uwasilishwaji wa matokeo ya utafiti wa Kilimo Shadidi cha mpunga uliowasioishwa na Dkt. Devotha Kilave.

Waandishi wa habari wakifuatilia uwasilishwaji wa matokeo hayo ya utafiti wa Mradi wa APRA Mkoani Morogoro kwenye ukumbi wa ICE - SUA.
Mwandishi wa habari wa Gazeti ka the Citizen Jacob Mosenda akiuliza swali kwa watafiti ili kupata ufafanuzi zaidi.
Waandishi wa habari wakifuatilia uwasilishwaji wa matokeo hayo ya utafiti wa Mradi wa APRA Mkoani Morogoro kwenye ukumbi wa ICE - SUA.
 


Na Calvin Gwabara, Morogoro


WATAFITI wa Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA)  kupitia Utafiti wao wamependekeza Sera za kilimo kuhimiza mafunzo ya Kilimo Shadidi cha Mpunga nchi nzima ili kuongeza mavuno na kuboresha maisha ya wakulima wa zao hilo nchini.

Mapendekezo hayo yametokewa na Mtafiti kutoka SIA Dkt. Devotha Kilave  kwenye warsha ya siku moja kwa waandishi wa habari wa vyombo mbalimbali  iliyoandaliwa na Mradi wa kutafsiri Sera za Kilimo Barani Afrika (APRA) kwa lengo la kufikisha matokeo ya utafiti wao kwa jamii.

“ Sambamba na hilo Wizara ya Kilimo, Chakula na Ushirika inatakiwa kutengeneza mkakati wa nchi nzima wa kutoa mafunzo ya kilimo hicho bora cha mpunga ili kuwafanya wakulima kuipenda teknolojia hiyo na kuifanyia kazi.” alisema Dkt. Devotha.

Ameongeza kuwa jitihada zozote za kupunguza gharama za uzalishaji na za masoko kama voor kuboresha miundombinu na kupeleka umeme zitasaisia sana kukufanya kilimo cha mpunga kuwa na faida kubwa kwa jamii.

“Katika utafiti wetu tumebaini kuwa mafunzo yana mchango mkubwa sana kwenye kuongeza tija kwenye kilimo, mfano wakulima waliopata mafunzo ya kilimo shadidi cha mpunga wamepata asilimia 8.7 zaidi ya wale ambao hawa kupata mafunzo ya Kilimo hicho” alifafanua Dkt. Devotha.

Mtafiti huyo alisema kwenye msimu wa Kilimo wa Mwaka 2016/2017 asilimia 45.8 wakulima  walianza kulima kilimo hicho lakini mbinu hiyo baadae ilisambaa kutoka kwenye vikundi vilivyo pata mafunzo ambao ni asilimia 61.6 na kufikia vikundi vingine 36 ambavyo havikupata mafunzo lakini vikaanza kilimo hicho.

Dkt. Devotha amebainisha kuwa wakulima waliolima kilimo shadidi cha mpunga walipata mavuno mengi ya tano 2.9 kwenye hekta moja wakati ambao hawakutumia mbinu hiyo walipata tani 2.9 kwa hekta moja.

Akizungumzia faida nyingine za kilimo hicho,  mkuu wa mradi huo Professa. Aida Isinika alisema kinasaidia kuokoa  upotevu wa maji na uharibifu wa mazingira ikizingatiwa kuwa Kilimo hicho cha mpunga kinafanyika jirani na ardhi oevu ya RAMSA ambayo inatunzwa.

Profesa. Isinika pia alisema endapo mbinu hiyo inatumika vizuri kwenye eneo hilo itasaidia kutoharibu mazingira kwani sehemu kubwa ya maji yanayotumika kuzalisha umeme kwenye Bwawa la Kidatu yanatoka kwenye bonde hilo.

Kilimo Shadidi cha Mpunga (SRI) ni mbinu unayotumia maji kidogo, mbegu kidogo lakini kwa kufuata kanuni bora za kilimo kama voor kulima kwa wakati, kupandikiza miche ikiwa na siku saba hadi kumi kutoka kwenye kitalu na kupanda kwa nafasi na mistari na kupata mavuno makubwa kuliko kilimo cha mazoea.

Share To:

Post A Comment: