MGOMBEA Ubunge wa Jimbo la Tanga (CCM) Ummy Mwalimu akiwahutubia wananchi wa Kata ya Mabawa Jijini Tanga wakati wa mkutano wake wa kampeni
MGOMBEA Ubunge wa Jimbo la Tanga (CCM) Ummy Mwalimu akiwahutubia wananchi wa Kata ya Mabawa Jijini Tanga wakati wa mkutano wake wa kampeni
Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Tanga Meja Mstaafu Hamisi Mkoba akizungumza wakati wa mkutano huo ambapo aliwataka wananchi kumchagua Ummy Mwalimu
MGOMBEA Ubunge wa Jimbo la Tanga (CCM) Ummy Mwalimu katikati amkifuatilia matukio mbalimbali kwenye mkutano huo kulia ni Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Tanga Meja Mstaafu Hamisi Mkoba kulia ni Katibu wa CCM wilaya ya Tanga Salim Kidima
MSANII wa Mziki wa Bongofleva Jijini Tanga Mwandey akitumbuiza kwenye mkutano huo wa kampeni
Msanii wa mziki wa Bongofleva Kassim Mganga akitumbuiza kwenye kampeni hizo
Msanii wa Mziki wa Bongofleva Mchina Mweusi akitumbuiza kwenye mkutano huo
Msanii wa mziki wa Bongofleva Kassim Mganga akitumbuiza kwenye kampeni hizo
Sehemu ya wananchi wakimsikiliza Ummy Mwalimu wakati akinadi sera zake
MGOMBEA Ubunge wa Jimbo la Tanga (CCM) Ummy Mwalimu akipandisha bendera ya CCM mara baada ya kuzindua shina la Wakereketwa Wajasiriamali Womens Group

MGOMBEA Ubunge wa Jimbo la Tanga (CCM) Ummy Mwalimu amehaidi iwapo akichaguliwa atawawezesha kiuchumii wakina mama wajasiriamali wadogo wadogo na watu wenye ulemavu kupatiwa mikopo isiyo na riba ili waweze kufanya shughuli zao za kuzalisha mali.

Huku akiwahaidi pia vijana nao pia watapatiwa mikop  na vitendea kazi ikiwemo pikipiki alimaarufu bodaboda ili waweze kufanya biashara za bodaboda bila kulipa fedha nyingi ambazo wanapaswa kulipa

Ummy ambaye pia ni Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto alitoa ahadi hiyo wakati akizungumza na wananchi wa Kata ya Mabawa Jijini Tanga ambapo alisema atafanya kazi usiku na mchana ili kuweza kutatua changamoto za wananchi.

Alisema dhana hizo ni kuwapatia pikipiki ili wafanya biashara ya bodaboda ambayo itawasaidi waweze kujiingizia kipato ambacho kitawasaidia kujikwamua kimaendeleo na hatimaye kukuza kipato chao.

“Ndugu zangu wafanyabiashara na wajasiriamali wadogo wadogo,watu wenye ulemavu tuwapa mikopo muweza kuongeza kipato chenu na hii itawasaidia kuinuka kiuchumi kwenye biashara zenu”Alisema Ummy Mwalimu.

Aliwataka wampigia kura za ndio ili wamuweze kuwa mbunge wa Jimbo hilo ili aweze kuhakikisha anawatumikia wananchi hao ili waweze kupiga hatua kubwa ya kimaendeleo.

“Lakini pia niwaombe tume kura nyingi za ndio Rais Dkt John Magufuli aendele kwani kazi yake kwenye Jiji la Tanga inaonekana kwenye sekta ya elimu amewezesha utoaji wa elimu bure,ujenzi wa madarasa nyumba vya maabara”Alisema

Hata hivyo alisema pia kazi ya Rais Dkt Magufuli kwenye sekta ya afya kwenye kata ya mabawa imeonakana kwani hamkuwa na kituo cha fya lakini leo  kumejenga majengo ya upasuaji wodi za watoto na wakina mama.

“Kwa heshima na taadhima nawaomba msifanya makosa mpeni kura za ndio Rais Dkt John Magufuli kwenye uchaguzi mkuu mwezi Octoba mwaka huu lakini pia naombeni kura zenu zote za ndio niweze kuchochea kasi ya ukuaji wa uchumi kwenye Jiji la Tanga”Alisema

Hata hivyo alisema kwamba hakuna mgombea Urais ambaye anaweza kufikia kazi zilizofanywa na Rais Dkt Magufuli hata kwa asilimia 1 .

Share To:

TANGA RAHA BLOG

Post A Comment: